Posts

Spika Wa Bunge Apokea Barua Ya Kujiuzulu Kwa Mbunge Wa Monduli

Image
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai amepokea barua ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiuzulu Ubunge wa Jimbo la Monduli kutoka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Julius Kalanga.

Shamsa: Akinipenda Chidi Inatosha!

Image
Shamsa Ford STAA mwenye mvuto Bongo Muvi, Shamsa Ford amesema kuwa hata kama leo watu watamchukia kwa jinsi alivyo au kwa kuzungumza ukweli hawezi kuumia hata siku moja kwa sababu anaamini aliyempenda kwa dhati ambaye ni mumewe Chidi Mapenzi yupo, inatosha. Staa huyo alizungumza na gazeti hili la Amani baada ya watu wengi kumshambulia kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kutokelezea na nguo fupi kwenye 40 ya mtoto wa Zamaradi, na kusema kuwa ni ngumu kumridhisha kila mtu kwenye maamuzi yako. “Mimi Mungu kanijalia maneno sijali kabisa na isitoshe Chidi akinipenda na akakubaliana na maamuzi yangu kwangu inatosha kabisa siwezi kumridhisha kila mtu,” alisema Shamsa.

MKUU WA WILAYA YA ARUMERU, JERRY MURO AFANYA ZIARA ARUSHA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Jerry Muro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Meru na Arusha.  MKUU wa Wilaya ya Arumeru, Mheshimiwa Jerry Muro jana tarehe 01 Agosti, 2018 alifanya ziara ya kikazi pamoja utambulisho kwa watumishi wa Halmashauri Mbili za Meru yenye kata 26 na Arusha  yenye kata 27 zilizo katika Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha. Akiwa katika halmashauri hizo, Mhe. Muro aliwataka watumishi kufanya kazi kwa kuzingatia mahitaji ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo ndio anasimamia Utekelezaji wake katika halmashauri zote mbili zenye kata 53.  Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Jerry Muro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Meru na Arusha.  Katika Ziara Hiyo, Mhe Muro aliambatana na Mkuu wa wilaya ya Monduli, Mhe Iddi Hassan Kimanta aliyekuwa akikaimu Wilaya ya Arumeru, pamoja na Katibu Tawala, Bwana Timotheo Mzava pamoja na baadhi ya viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya

Picha ya Gadner na Mwanae Yazua Gumzo Mitandaoni

Image
 Kuna picha  aliweka Gadner akiwa amerepost kutoka katika akaunti ya binti yake Karen ikiwa inaonyesha akiwa amemkumbatia mtoto wake  huku wakiwa wamelala kwenye kochi, na kwa jinsi wao walivyochukulia ilikuwa ni kama mapenzi ya baba na mtoto. Lakini baada ya picha hiyo kwenda katika mitandao ya kijamii ilileta gumzo na kusemewa maneno mengi sana huku wadau na baadhi ya mashabiki wakisema kuwa hayo sio maadili ya kitanzania hasa kwa baba na binti yake. Huku wengine wakimtuhumu sana gadner na kusema kuwa hawamuamini sana kutokana na ukweli kwamba amekuwa akitoka kimapezni na wasichana wenye umri kama wa binti yake , hivyo hiyo inaleta picha mbaya kwa mashabiki wanaomuona akiwa anafanya hivyo. ==>>Tazama baadhi ya maoni hapo chini

Mke wa Babu Tale: Nina wivu kwa mume wangu akitoka bila mimi lakini

Image
Wiki weekend iliyopita kwa mara ya kwanza meneja wa Diamond Babu Tale alitoka na mama watoto wake na kwenda kwenye arobaini ya mtoto wa Zamaradi iliyofanyika huko Bunju B. Bongo5 ilifanya mahojiano na mke wa Babu Tale na kumuuliza anajisikiaje pale anapomuona mume wake akipiga picha na warembo mbalimbali wakati akiwa kwenye shughuli zake za kikazi. “Wivu upo lakini unategemea upo kwa kiwango gani na wivu ukiuendekeza mtakwama,” alisema mama watoto huyo wa Tale. Kwa upande wa Babu Tale alidai kwa kuwa yupo kwenye tasnia ya burudani kwa muda mrefu amejifunza hawezi tembea na mke wake kila sehemu. “Leo sijaja kazini nimekuja kwenye shughuli ndio maana unaona niko na mke wangu,” alisema Babu Tale.

AUNT ACHOMOA NDOA NA IYOBO

Image
Aunt Ezekiel MUIGIZAJI wa kitambo kwenye tasnia ya filamu, Aunt Ezekiel, ambaye pia ni mzazi mwenzie na dansa maarufu wa Wasafi Classic Baby (WCB), Moses Iyobo, amesema kuwa hana mpango wa kufunga ndoa na dansa huyo japokuwa wameshakaa wote zaidi ya miaka mitatu kwani kikubwa wanachokiangalia ni kulea mtoto wao Cookie. Aunt Ezekiel akiwa na mzazi mwenzie na dansa maarufu wa Wasafi Classic Baby (WCB), Moses Iyobo Akizungumza na Amani, Aunt alisema kuwa siyo kwamba mtu akifunga ndoa ndiyo anaweza kuishi vizuri na mwanaume wake, bali ni kwamba anachojua kuishi vizuri ni sifa moja kubwa ya kuendelea kuwa pamoja ni kupeana heshima na kila mmoja kutambua anachokifanya. “Mimi sitaki hata kukuficha wala sijawahi kufikiria kufunga ndoa na Iyobo leo wala kesho kikubwa tunaishi vizuri na tunalea mtoto wetu ipasavyo hilo ndilo ninalolitaka na si vinginevyo kwani kuolewa siyo ishu kikubwa malezi ya mtoto tu,” alisema Aunt. STORI NA IMELDA MTEMA | GPL

BETHIDEI YA TIFFAH KUFURU

Image
DAR ES SALAAM: Maandalizi ya pati ya kuzaliwa (birthday) ya bintiye ambaye ndiye uzao wake wa kwanza, Latifah Nasibu ‘Tiffah Dangote’ (3), yamemfanya baba’ke ambaye ni staa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kutoa kiapo kizito kuwa itakuwa ni shughuli ya kufuru, Risasi Jumamosi linakupa exclussive. Agosti 6, mwaka huu, Tiffah atatimiza umri wa miaka mitatu tangu alipozaliwa Agosti 6, 2015, lakini sherehe hiyo imesogezwa mbele ambapo sasa itafanyika Agosti 17 hadi Agosti 20, mwaka huu. DIAMOND NA RISASI JUMAMOSI Akizungumza na Risasi Jumamosi juu ya pati hiyo ya Tiffah ya kutimiza umri wa miaka mitatu, Diamond alisema kuwa, yupo tayari kufilisika, lakini ahakikishe mwanaye huyo ana furaha kwa kumfanyia pati hiyo ambayo itakuwa ya kihistoria. “Nimepanga iwe sherehe kubwa sana, acha nifilisike, lakini mwanangu afurahi,” ndivyo alivyoanza Diamond kwenye mahojiano hayo maalum na Risasi Jumamosi na kuongeza: “Nipo tayari kutumia sehemu ya pesa za

TAGCO NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZAPONGEZWA KWA UTENDAJI

Image
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando akisisitiza kuhusu namna Halmashuri hiyo ilivyojipanga katika kuimarisha mawasiliano ya kikakati hasa kutangaza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali. Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando akisisitiza jambo kwa ujumbe wa chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO wakati wa ziara ya ujumbe huo katika Halmashauri hiyo kukagua na kujionea jinsi maafisa Habari wanavyotekeleza jukumu la kuisemea  Serikali katika Mikoa na Halmashuri zao. Kiongozi wa Ujumbe wa Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Gaudensia Simwanza akisisitiza jambo kwa  Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando wakati wa ziara ya ujumbe huo katika Halmashuri hiyo uliolenga kukagua na kuweka mikakati ya pamoja katika

WAZEE WA NITUMIE PESA KWA NAMBA HII’… WANASWA

Image
I RINGA: Yawezekana wewe ni kati ya watu ambao walishawahi kutumiwa meseji za kitapeli kutoka kwa watu hao (pichani) ambao huandika hivi; ‘ile pesa nitumie kwenye namba hii, jina litatokea…, simu yangu ina tatizo’. Kama jibu ni ndiyo basi habari ikufikie kwamba, watuhumiwa wengine wapatao saba wa utapeli huo hivi karibuni wamenaswa mkoani Iringa baada ya kuwaliza watu wengi kwa muda mrefu. Watu hao wamekuwa wakiwatumia watu meseji na kuwaelekeza kuwa watume pesa, mazingira ambayo baadhi huenda walikuwa na watu ambao ilikuwa wawatumie pesa hivyo hutuma na kujikuta wametuma kwa matapeli hao. POLISI WATANGAZA VITA Kufuatia kushamiri kwa utapeli huo katika mikoa mbalimbali, jeshi la polisi kupitia kwa makamanda wa mikoa hivi karibuni lilitangaza vita dhidi ya uhalifu huo na kufanikiwa kuwanasa baadhi ya watu huku tahadhari ikitolewa kwa wananchi kuwa makini wanapokumbana na meseji za aina hiyo. WALIONASWA IRINGA Mbali na wale 15 wa hivi karibuni waliokamatw

MWANAMKE KUKOSA MSISIMKO WA TENDO LA NDOA

Image
T ATIZO hili la mwanamke kukosa msisimko wa tendo la ndoa kitaalamu tunaita ‘Female Sexual arousal disorder’. Mwanamke akiwa na hali hii huwa hajihisi hamu wala haja ya kuhitaji tendo hilo na wakati mwingine huona kama usumbufu endapo atakuwa katika mahusiano. Mwanamke wa aina hii kama yupo mwenyewe au ‘single’ haoni umuhimu wa kuwa na mpenzi au mwenza na hasa kama anajimudu kiuchumi. Wapo baadhi ya wanawake wenye hali hii ambao hawana watoto au wengine wanamtoto mmoja au zaidi na aidha wameachana na wenza wao au wenza wao walishafariki. Msisimko hupatikana baada ya hamu ya tendo la kujamiiana kuwa juu ya kiwango na kusababisha mabadiliko mwilini na kusaidia mwili uwetayari kwa tendo. Hali ya msisimko kwa mwanamke haina tofauti na hali ya mwanaume kusimamisha uume wake. Mwanamke aliyepoteza msisimko huwa hajisikii chochote wakati wa ’ Romance’ au maandalizi ya tendo la ndoa, wengine huwa hawapati hamu na wengine hupata hamu kwa kiasi kidogo lakini hawapati mguso au

Diamond azuiwa na Basata kwenda kufanya shoo nje

Image
BARAZA la  Sanaa Tanzania (BASATA) leo limemzuia mwanamuziki, Nassib Abdul ‘Diamond Platnumz’ kwenda kufanya shoo nje ya nchi akiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam  kwa sababu msanii huyo hakuwa na kibali. Kaimu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) Onesmo Mabuye alipokuwa akizungumza na TBC, kuhusiana na sintofahamu hiyo kuwa ni kutokana na msanii huyo kukosakibali cha Basata. BASATA wamesema kwa sasa hivi kuna utaratibu mpya ni kuwa msanii akitaka kwenda kufanya shoo nje ya nchi ni lazima apitie kwa BASATA wampe kibali na kisha akirudi pia anatakiwa kuripoti kwao BASATA wamesema kumzuia Diamond wanataka iwe fundisho kwa wasanii wengine ili wanapoenda nje ya nchi wafuate taratibu zilizowekwa.

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU AGAWA BAISKELI KWA WALEMAVU

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndg. Hudson Kamoga ametoa msaada wa baiskeli sita kwa ajili ya walemavu ili kuwasaidia katika maisha yao ya kila siku. Kamoga amewashukuru marafiki zake waliochangia katika kuboresha maisha na kuwasaidia wananchi wanyonge wanaoishi katika mazingira magumu. Kamoga amesema “Serikali hii inawajali wanyonge na sisi kama viongozi lazima pia tufikiri zaidi ya ukomo wa kazi zetu za kila siku katika kuwahudumia wananchi wa hali ya chini. Nafasi hii niliyopewa na Mungu kupitia kwa Mh. Rais Dr. John Pombe Magufuli ni kwa ajili ya kuwatumikia na kuwasaidia watanzania hasa wanyonge,Nafasi hii ni kwa ajili ya watu ninaotakiwa kuwatumikia na si kwa ajili yangu binafsi,ndio maana ya utumishi”alisema Kamoga. Baiskeli hizo zimetolewa na marafiki wa mkurugenzi huyo wanaotambua mchango wake katika kulitumikia taifa na kuwajali watu wanaoishi kwenye mazingira magumu, Wadau hao wameahidi kutoa vifaa vingine kila watakapokuwa

Hatua 5 za kuzungumza na mpenzi wako aliyekasirika

Image
Kwenye mapenzi kuna nyakati za kutofautiana, kukasirishana. Katika hali ya kawada kipindi hiki huwa ni za hatari kwa sababu husababisha nyufa kubwa za uhusiano na kulifanya penzi kukosa ladha. Sote tunajua, watu hupigana, huachana, hujeruhiana, hutukanana, hudhalilishana wakiwa na hasira. Hata hivyo si wote wanaojua wafanye nini wanapojikuta wameingia kwenye hatua hiyo mbaya. Msomaji wangu, hebu jaribu kukumbuka ugomvi mmoja uliotokea kati yako na mpenzi wako na ikiwezekana jikumbushe mlivyoanza! Utabaini kuwa mlianza kama utani na mkajikuta mmefura kwa hasira, mkatwangana makonde, mkatamkiana maneno makali ya kuudhi na pengine mkaamua kuachana. Yote hii ni kwa sababu mlikosa elimu ya mazungumzo. Ingekuwa mmoja wenu hasa yule aliyekuwa wa pili kukasirika anafahamu hatua za kuzungumza na mtu aliyekasirika angechukua jukumu la kutuliza machafuko na kuleta amani kwenye mapenzi. Tazama hatua tano za kuzungumza na mpenzi aliyekasirika. MPUNGUZE MHEMKO Hasira hujaz

Zari Awapiga Stop Wema, Aunt: Sitaki Kunichafulia Nyumba, Kaeni Hukohuko

Image
IKIWA ni saa chache baada ya mwanamuziki Diamond Platnumz kualika watu takribani 50 kuuhudhuria sherehe ya kuzaliwa mtoto wake  Tiffah, mzazi mwenzake, Zari Hassan amepiga marufuku ugeni huo. Jana wakati wa sherehe ya kufikisha siku 40 ya mtoto wa mtangazaji Zamaradi Mketema, Diamond alialika wanakamati zaidi ya 10 kuhudhuria sherehe hiyo ya Tiffah, Sauzi hukuakisema atalipia tiketi za watu 30 kwa ajili ya kuhudhuria sherehe na kuwalipia watoto 10 na wazazi wao. Hata hivyo, Zari amemjibu kupitia mtandao wa Instagram aliandika kuwa hautaki ugeni huo akihofia kuchafuliwa nyumba yake:  “Sitaki kunichafulia nyumba kaeni hukohuko.” Miongoni mwa wanakamati walioalikwa ni Wema Sepetu ambaye amewahi kuwa mpenzi wa mwanamuziki Diamond Platnumz na mwigizaji Aunty Ezekiel. Tiffah ambaye jina lake halisi Latiffah alizaliwa Agosti 6, 2015. Hata hivyo sherehe za kuzaliwa binti huyo zitafanyika siku tatu mfululizo kuanzia Agosti 17- 19 mwaka huu.

Katibu Tawala Mkoa Mtwara wa Awaasa Maafisa Habari Kutekeleza Majukumu Yao Kwa Weledi

Image
Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara Bw. Alfred Luanda akisisitiza jambo kwa  Mwakililishi wa Idara ya Habari MAELEZO Bw. Casmir Ndambalilo wakati wa ziara iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa kushirikiana na Idara ya Habari MAELEZO katika Mkoa wa Mtwara leo kuona utendaji wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini pamoja na changamoto zilizopo ili kuweka mikakati ya pamoja ya  kuzitatua hali itakayoimarisha Mawasiliano Serikali kwa umma katika mkoa huo. kurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara  Bw. Omari Kipanga akisisitiza jambo wakati wa ziara iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa kushirikiana na Idara ya Habari MAELEZO katika Mkoa wa Mtwara leo kuona utendaji wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini pamoja na changamoto zilizopo ili kuweka mikakati ya pamoja ya  kuziondoa hali itakayoimarisha Mawasiliano Serikali kwa umma katika Halmashuri hiyo

HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI YAJIDHATITI KUIMARISHA MAWASILIANO NA WANANCHI

Image
Kiongozi wa ujumbe kutoka Chama cha maafisa Habari na Mawasiliano  Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO  Bi. Gaudensia  Simwanza akisisistiza jambo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi.  Changwa Mkwazu      wakati wa ziara ya ujumbe huo katika halmashauri hiyo uliolenga kuona utendaji kazi wa Maafisa  Habari na Mawasiliano na namna wanavyokabiliana na changamoto mbalimbali ili kuweza kuisemea Serikali kimkakati. Kiongozi wa ujumbe kutoka Chama cha maafisa Habari na Mawasiliano  Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO Bi. Gaudensia Simwanza akisisitiza jambo kwa Afisa Habari na Mawasiliano wa Halmashuri ya Wilaya ya Masasi Bi mara baada ya ziara ya ujumbe huo katika Halmashuri hiyo. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi. Changwa Mkwazu akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya  ujumbe  wa viongozi wa Chama cha maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Ha

Nyumba mbili zachomwa Moto Mwanza kisa wizi

Image
Na Paschal D.Lucas, Mwanza Wananchi waliojichukulia sheria mkono wamechoma nyumba mbili za familia moja na nyingine kuziharibu katika mtaa wa Nyakabungo "A" kata ya Isamilo wilayani Nyamagana Mkoani Mwanza  baada ya kuona watoto wa familia zile wanajihusisha na uhalifu hapo mtaani hapo mara kwa mara. Maamuzi hayo yamekuja baada ya wananchi kudai kuwa watoto hao wamekuwa wakikamatwa na kupelekwa mahakamani kushitakiwa lakini mara nyingi wamekuwa wakiachiwa kwa dhamana na kurudi mtaani kuendelea tena na tabia hiyo kitendo ambacho kimekuwa ni kero kubwa  kwa wananchi wa eneo hilo. Tukio hilo lilitokea majira ya saa 3 usiku wa tarehe 25,Julai 2018 ambapo katika tukio hilo nyumba mbili zilizoharibiwa ni mali ya Selina Francis (50) na Abdallah Mwita wote wakiwa ni wakazi wa Nyakabungo mkoani humo. Vile vile nyumba moja mali ya Manka Francis James iliharibiwa vibaya na kundi hilo kwa kuvunjwa milango na madirisha na kuharibu vitu mbalimbali vilivyokuwemo ndan

Tambwe Afunguka Mazito Yanga

Image
MSHAMBULIAJI wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe ameibuka na kusema wanaumizwa na hali inayoendelea katika timu hiyo lakini haiwafanyi washindwe kupigana huku wakiwaomba mashabiki kuwa kitu kimoja kabla ya mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gor Mahia ya Kenya. Yanga inatarajiwa kurudiana na Gor Mahia Jumapili ya wiki katika mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar baada ya ku­fungwa mabao 4-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa nchini Kenya. Akizungumza na Championi Jumatano , Tambwe alisema kwa sasa bado wanapita katika kipindi kigumu lakini hawezi kuwafanya washindwe kufanya vizuri katika mchezo huo wa maru­diano huku akiwaomba mashabiki wasichoke kuwasapoti. “Tunajua matokeo hayakuwa mazuri kwetu katika mchezo wa kwanza kwa sababu hakuna ambaye alitege­mea tutapoteza tena kwa idadi kubwa ya mabao lakini kwa kuwa wenzetu walitumia mapungufu yetu kupata ma­tokeo. “Nadhani huu ni wakati wa kuende­lea kushikamana, mashabiki wetu hawa­paswi kuendelea kuka

Mbelgiji Aanza Kukiunga Kikosi Upya

Image
KOCHA Patrick Aussems raia wa Ubelgiji ameanza kutoa mafunzo ya mfumo anaotaka kuutumia katika msimu wa 2018/19 akiwa na Simba. Simba imeweka kambi ka­tika mji mdogo wa Kartepe ambao uko mlimani kabisa, sehemu maalum kwa ajili ya kambi za timu. Aussems ameanza kukinoa kikosi chache akiwafundisha mifumo na namna ya uchezaji katika masuala mbalimbali. Kocha huyo amekuwa aki­waonyesha wachezaji wake namna ya kulinda lakini pia kushambulia kwa tahadhari. Wakati Simba ilipotua hapa, kocha huyo alianza kutoa mafunzo ya kawaida, zaidi wachezaji wakioneka­na kupasha misuli kawaida. Inaonekana ame­kuwa akiongeza mazoezi taratibu huku akichanganya na aina ya uche­zaji. Makocha wengi huanza kufundisha mifumo baada ya timu zao kupata mazoezi ya kuto­sha. Lakini Mbelgiji huyo anaonekana kuwa tofauti ki­dogo akienda anachangan­ya mazoezi ya kawaida na mifumo, taratibu.

Beki Simba atua Singida United kwa mkopo

Image
Klabu ya soka ya Singida United imethibitisha kuwa imemsajili mchezaji Jamaly Mwambeleko kutoka Simba kwa usajili kamili tofauti na taarifa zilizoeleza kuwa wamemchukua kwa mkopo, huku wakiweka wazi kuwa wamemwongeza mwaka mmoja na sasa ni mchezaji wao kwa miaka miwili. Mkurugenzi wa Singida United Festo Sanga ameeleza kuwa walifanya mazungumzo na Simba na kumalizana nao kisha kumpa mkataba wa mwaka mmoja Jamaly Mwambeleko lakini baadae walimwongeza mwaka mmoja na kuwa miwili. ''Tumemsajili Mwambeleko kwa usajili kamili wala hajaja kwetu kwa mkopo, ila awali mazungumzo yalikuwa hivyo lakini kocha Hemed Morocco akapendekeza tuwe naye kwa muda mrefu ndio akasaini mkataba wa kuitumikia Singida United kwa miaka miwili'', - amesema. Jamaly Mwambeleko ambaye anacheza nafasi ya mlinzi wa kushoto ni sehemu ya wachezaji walioachwa na Simba katika usajili huu kwa kile kilichoelezwa ni kutokuwa na nafasi ya kucheza hususani nafasi yake pale Simba kuwa na w