Posts

Showing posts from August 12, 2015

FAHAMU HUU UMUHIMU WA MASSAGE KWA MWILI WAKO

Image
Je, kuna siku umewahi kuamka asubuhi na kujikuta ukiwa mchovu sana kupita kiasi? hivi ulihisi nini baada ya kuamka hivyo? Je, ulihisi una kahoma kidogo? au uliwaza huenda ni uchovu wa kazi za jana yake? naamini kuna mengi ulijiuliza na huenda hukupata jibu la uhakika. Kwa kawaida huwa kuna sababu nyingi za mtu kuamka akiwa mchovu wa mwili, miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na uchovu wa kazi, michezo n.k. Lakini unaweza kuepukana na hili suala la kuamka na uchovu endapo tu utajenga utaratibu wa kupata huduma ya kukandwa ( massage ) mwili kila baada ya muda fulani. Huduma hii ni vyema ukafanyiwa na mwezi (mke au mume) wako nyumbani ikiwa unahitaji kufanya kwa lengo la kuweka mwili wako sawa  sawa tu. Mtaalam wa masuala ya 'massage' kutoka Mandai Herbalist Clinic Mathayo Masinema Bahebe anasema kuwa massage husaidia kupunguza na kuondoa maumivu yote ya mwili pamoja na kurekebisha mzunguko wa damu mwilini na kuweka sawa sehemu zote za maungio ya mifupa 

TONTO DIKEH AOLEWA, ABADILI JINA INSTAGRAM

Image
Muigizaji kiwango kutoka Nigeria, Tonto Dikeh. Lagos ,NIgeria MUIGIZAJI kiwango kutoka Nigeria, Tonto Dikeh ameolewa rasmi na aliyekuwa mpenzi wake, Churchill Olakunle Oladunni wiki iliyopita.Tarifa za kuolewa zilianza kuzagaa mapema wiki iliyopita baada ya staa huyo kubadili jina lake kwenye Mtandao wa Kijamii wa Instagram na kujiita, Mrs Tonto Wigo Dikeh-Churchill. Lakini wikiendi iliyopita zilizagaa picha mitandaoni zikimuonyesha staa huyo akiwa na mumewe huyo mpya lakini kubwa zaidi ni ile ambayo amepiga na bibi yake wakiwa wanapongezwa kwenye sherehe hiyo. Tayari inadaiwa kuwa Tonto ni mjamzito na bibi yake huyo ameonekana kuumia zaidi baada ya kudai kuwa anamuacha peke yake kwani alizoea kuishi naye lakini amemtakia maisha mema na mumewe huyo.

BREAKING NEWZZ..BAADA YA KAMATI KUU CCM KUFUTA MATOKEO MAJIMBO MATANO,HII NDIYO KAULI NZITO YA MEYA JERRY SILAA WA UKONGA

Image
Mungu hamtupi mtu mwenye dhamira ya kweli, hawezi shindwa hawezi kata tamaa... Wana CCM jimbo la Ukonga tukutane kwenye matawi ya CCM kesho kutwa tarehe 13 tuchague Mbunge wa CCM tunayemtaka NINI MAONI YAKO NDUGU

KAMATI KUU YA CCM LEO MJINI DODOMA

Image
  Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akifungua kikao cha Kamati Kuu ya CCM, leo Agosti, 11, 2015 katika ukumbi wa Jengo la White House Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.     Kikao cha Kamati Kuu ya CCM, leo Agosti, 11, 2015 katika ukumbi wa Jengo la White House Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.    Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Steven Wasira na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Adam Kimbisa wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza kikao cha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma.   Wajumbe wa Kamati Kuu, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Adam Kimbisa na Dk. Emmanuel Nchimbi, wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza kikao cha Kamati Kuu ya CCM leo mjini Dodoma.   Wajumbe wa Kamati Kuu, Dk. Maua Daftari na Samia Suluhu Hassan, wakibadilishana mawazo ukumbini,

Wema Aibu mpya! Anaswa na mwanaume hotelini

Image
Wem Sepetu ‘Madam’ akidendeka na mwanaume  mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wakiwa kwenye Mgahawa wa hoteli  iliyopo Msasani jijini Dar. Mwandishi wetu Licha ya kudai kwamba skendo za ngono sasa basi, staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amekwaa aibu mpya baada ya picha zake kunaswa akiwa na mwanaume mwingine kwa mara nyingine, mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wakiwa kwenye Mgahawa wa hoteli iliyotajwa kwa jina la Cape-town Fish Market iliyopo Msasani jijini Dar. Wakiendelea kufanya yao. MADAI MAZITO Chanzo chetu ambacho ni makini kilipenyeza kuwa, katika tukio hilo la hivi karibuni, staa huyo alikuwa hafahamiani na mwanaume huyo, lakini kuna kijana mmoja ambaye mara nyingi anawakuwadia mastaa wa Bongo kwa matajiri, alidaiwa kumtonya Wema kuwa kuna ‘mchati’ anataka kutoka naye. Kilifunguka kwamba, baada ya Wema kung’atwa sikio juu ya Mkongomani ambaye ana ‘hela chafu’, alidaiwa kuonekana kuchach

MWENYEKITI WA CHADEMA AONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KUELEZEA AFYA YAKE

Image
  Mbowe akiongea na Waandishi wa habari leo Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mwenyekiti mwenza wa UKAWA Freeman Mbowe, ameongea na vyombo vya habari na Kuelezea maendeleo yake kiafya baada ya jana kuugua gafla na kukimbizwa Hospitali.  BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI