Posts

Showing posts from May 7, 2017

Gwajima ataka Bunge lisimame kuombeleza vifo vya wanafunzi 32

Image
Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephath Gwajima amemtaka Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge siku ya kuaga miili ya watoto waliofariki kwa ajali ya jana. Amesema kama Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliamuru viongozi kusimama kwa kuwakumbuka watoto hao itakuwa ajabu kwa bunge kuendelea na vikao vya Bunge Amesema Spika akiahirisha Bunge kwa siku moja itatoa nafasi kwa wabunge hao kwenda Arusha ili kuomboleza pamoja.

NJAA YAMNYIMA SUBIRA MBUNGE WA CCM AFUNGUKA MBELE YA POLEPOLE

Image
Mbunge wa Mbulu Vijijini, Mh. Flatei G. Massay  Mbunge wa Mbulu Vijijini, Flatei Massay amemuomba Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole kufikisha kilio cha wananchi kwa Serikali ili wapatiwe chakula cha njaa. Massay amesema hayo leo baada ya Polepole kufanya ziara ya siku mbili wilayani Mbulu ya kukagua uhai wa chama,  kusikiliza kero na kuzungumza na Halmashauri Kuu ya CCM, Wilaya ya Mbulu. Amesema hivi sasa wananchi wana wakati mgumu kutokana na bei kubwa ya vyakula wanavyonunua kutokana na ukame uliotokea msimu uliopita hivyo Serikali iwapatie chakula cha bei nafuu. Amesema wananchi wa eneo hilo ni hodari kwa kulima mazao mbalimbali ya chakula na biashara, ila kutokana na ukame uliotokea msimu uliopita hivi sasa wanakabiliwa na upungufu wa chakula. “Kwa sababu chama ndiyo kinasimamia Serikali, kilio hiki cha wananchi tunakifikisha kwako ili tatizo lao limalizike, kwani wanataka chakula cha bei nafuu na siyo kile chakula cha bure,”

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Kuongoza Kuaga Wanafunzi Waliofariki Arusha Kesho

Image
  Makamu wa Rais, Samia Suluhu kesho saa mbili asubuhi ataongoza wakazi wa Arusha katika Uwanja wa Sheikh Abeid Karume kuaga miili ya wanafunzi waliofariki katika ajali ya gari Arusha ambapo serikali imegharamia sanda  na majeneza kwa wanafunzi wa shule Lucky Vincent waliopoteza maisha jana kwenye ajali. Akitoa taarifa hiyo leo Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro,  amesema taarifa za awali zinaonyesha tayari serikali imekwishalipia gharama za majeneza na sanda za kuhifadhia miili ya marehemu ambao kesho wanatarajiwa kufanyiwa ibada katika Uwanja wa heikh Amri Abeid. Mazingira ya shule hiyo. Aidha Lazaro amesema viongozi mbalimbali wakiwemo mawaziri na wabunge bado wanaendelea kukusanyika katika eneo la shule ya Lucky Vincent  kwa ajili ya kikao.

BREAKING: AJALI NYINGINE DUMILA MOROGORO YAACHA MASWALI

Image
Ikiwa bado watanzania tukiomboleza kutokana ajali ya jana mkoani A rusha iliyoondoka na wanafunzi 32, na kuacha majonzi kwetu na TAIFA ZIMA. Habari za hivi punde toka Morogoro Dumila Eneo la Kutoka mvomelo ukipita matuta ya mwanzo kabla hujafika Makunganya   kuna Gari ya abiria aina ya Eicher imegongwa na lori na inariportiwa kuwa hali mbaya sana.. Bado hakuna ripot ya kifo wala majeruhi @afande Anna Job kajulishwa   Tumwombe  Mungu atupiganie Tarifa kamili baada ya muda mfupi ujao.. Tayari AKISI TV iko njiani kuelekea eneo la tukio kukupa habari zaidi. Pia Tunarajia kupata taarifa kamili kutoka  jeshi la polisi.

HUMPHFEREY POLEPOLE AFUNGUKA HAYA KUHUSU MANGE KIMAMBI

Image
Baada ya Pole pole kuandika hiyo post hapo juu ikiwa imemtaja Mange Kimambi, Mange akaamua kumtolea  uvivu kama ifuatavyo : . #Regrann from #mangekimambi_ - : "PolePole Tokea uwe katibu uenezi wa CCM ile brain ya kuongea mapoint mazito mazito imetoweka kabisa Yani. Hivi PolePole unakumbuka ulivyokuwaga unawa-inspire watanzania kwa jinsi ulivyokuwaga unaongea mapoint mazitoooooo. Siku hizi unaongea kama Bashite. Huna point, unajibu vitu bila busara, unajibu mambo kiwepesi wepesi... Hivi Kweli Polepole kweli kati ya yote niliyosema point kubwaaaaa uliyoiona wewe ni Mimi kusema Kinana ameacha kufanya kazi za Chama???? And it's 100% true kinana amegoma kufanya mambo ya chama mpaka Baba Bashite A.k.a mwenyekiti wa CCM akamueleze why alimuitia TISS. Kinana alishikiliwa Na TISS nyumbani kwake for over 2 weeks... Kwa issue ya Kinana alivyokaaa vibaya kwa Sasa ilibidi nyinyi kama chama muwatoe hofu wana CCM Na watz kwa ujumla kwa kuweka wazi data kuw

BREAKING NEWS: WANAFUNZI 32 WAFARIKI KWA AJALI KARATU

Image
Saturday, May 06, 2017 Arusha. Wanafunzi zaidi ya 20 wanahofiwa kupoteza maisha  katika ajali ya basi iliyotokea wilayani Karatu leo asubuhi. Habahari zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa basi hilo lilikuwa likitokea Arusha Mjini kuelekea katika Mbuga za wanyama.  Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Therezia Mahongo amethibitisha tukio hilo. Tutaendelea kukujuza zaidi kuhusu taarifa hii.