Posts

Showing posts from January 20, 2014

HAFLA FUPI YA KUWAAPISHA MAWAZIRI WAPYA IKULU DAR LEO

Image
Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dr. Gharib Bilal wakiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri Mbalimbali wapya mara baada ya kuwaapisha kwenye viwanja vya ikulu leo ambapo viongozi mbalimbali wa serikali na waalikwa wamehudhuria na kushuhudia Picha na OMR Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimpongeza Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akiwa na mkewe aliyewahi kuwa Miss Tanzania, Faraja Kotta na  familia yake, baada ya kuapishwa katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam, leo. Kulia kwa Makamu ni Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba.  Picha na OMR Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Adam Malima, kuwa Naibu Waziri wa Fedha, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo. Picha na OMR Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri Mbalimbali wapya na wanaohamia katika wizara nyingine mara baada ya kuwaapisha kwenye viwanja vya ikulu

ANGALIA PICHA ZA MWANAJESHI FEKI ALIYEKAMATWA LEO TANGA AKIMTAPELI DC

Image
'Koplo' feki wa JWTZ akiwa ofisini kwa mkuu wa wilya.  'Koplo' feki akijiandaa kupanda  kwenye gari kupelekwa kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi  'Koplo' feki akiwa na pamoja na Luteni Yahya Wangwe na Mteule daraja la pili Albano Semfuko Na Mashaka Mhando,TANGA VIKOSI vya Ulinzi na Usalama Wilayani hapa,vinamshikilia Edwin John Mponji (31) kufuatia kwenda ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tanga na kujitambulisha kwamba yeye ni koplo wa jeshi la Wananchi JWTZ akitaka kijana wake afanyiwe mpango wa kuingizwa Jeshi la kujenga Taifa. "Koplo" Mponji alikwenda ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tanga,Halima Dendego Januari 16 mwaka huu siku ambayo Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilayani hapa ilikuwa katika zoezi la kuwafanyia usaili vijana wanaotakiwa kujiunga na jeshi la kujenga Taifa (JKT). Akiwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya,Mponji alijitambulisha kuwa yeye ni afisa wa JWTZ ambaye kwa sasa yupo kikosi cha 36 KJ Mkoani Pwani ambapo aliambatana na k

ANGALIA PICHA YA AJALIA YA NOAH ILIYOPOTEZA MAISHA YA ABIRIA 13 SINGIDA

Image
    Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Isuna tarafa ya Ikungi wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, wakitoa miili ya abiria wa Noah T.730 BUX waliofariki baada ya gari hilo kugongwa na lori aina ya Scania T.687 AXB kwenye barabara kuu ya Singida – Dodoma leo. Noah hiyo ilikuwa ikitoea Itigi wilayani Manyoni akienda Singida mjini.(Picha na Nathaniel Limu).  Gari aina ya Noah T,730 BUX linavyoonekana baada ya kugongwa na Lori.      ABIRIA 13 wakiwemo watatu wa familia moja wamefariki dunia mkoani Singida leo, baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Noah T.730 BUK, kugongwa na Lori aina ya Scania. NA  MATUKIO NA VIJANA Ajali hiyo ya kusikitisha imetokea leo saa 1.32 asubuhi katika barabara kuu ya Singida-Dodoma eneo la kijiji cha Isuna tarafa ya Ikungi wilaya ya Ikungi mkoani Singida.  Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP ,Geofrey Kamwela, amesema gari hilo aina ya Noah lilikuwa likitokea Itigi wilaya ya Manyoni na lilikuwa na safari ya kuja Singida mji