Posts

Showing posts from August 4, 2015

ZITTO KABWE AWAPONDA LOWASSA NA MAGUFULI

Image
Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe. Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema hakuna tofauti kati ya mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliyechukua fomu ya kugombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kutokana na wote kutokuwa na ubavu wa kupambana na ufisadi. Zitto alisema hayo jana katika mkutano mkuu wa ACT- Wazalendo Jimbo la Kigoma Mjini, uliokuwa maalum kwa ajili ya kupiga kura ya maoni ili kupata mgombea wa ubunge wa chama hicho Jimbo la Kigoma Mjini. Alisema katika mazingira ya sasa ya kisiasa nchini, ni ACT-Wazalendo pekee ambacho kinaweza kusimama na kusema kinapambana na ufisadi. Alisema kutokana na chama hicho kuchukia rushwa ndiyo maana kimetoa msimamo kuwa hakiwezi kushirikiana na chama chochote ambacho maadili ya viongozi wake yanatia shaka. Zitto alisema uchaguzi mkuu wa mwaka huu utakuwa mgumu na ushindani m

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya August 4

Image

Diamond Platnumz ashinda tuzo mbili katika tuzo hizi kubwa za Nigeria

Image
Diamond Platnumz anazidi kuupaisha muziki wake baada ya kushinda tuzo mbili kubwa za Nigeria zijulikanazo kama NollyWood & African People Choice Awards. Diamond Platnumz ameshinda katika Kipengele cha FAVOURITE SONG OF THE YEAR (Nana) pamoja na FAVOURITE ARTIST OF THE YEAR. Katika Mtandao wa Instagram Diamond Platnumz ameandika “ Thanks alot to my all Fans around the World, for your unconditional love and Support that you been Giving me… i can’t even explain how grateful i am… two awards on NollyWood & African People Choice Awards @Africannafca FAVOURITE SONG OF THE YEAR (Nana) FAVOURITE ARTIST OF THE YEAR thanks alot @Africannafca (Naomba nitumie Muda huu kuwashkuru Mashabiki zangu wote kwa Mapenzi na Sapoti yenu ya Dhati mnayoendelea kunipa…ningependa niwataarifu kuwa kijana wenu mmeniwezesha kushinda tunzo mbili ambazo ni MSANII ANAEPENDWA AFRICA na NYIMBO INAYOPENDWA AFRICA (#NaNa ) kwenye Tunzo za NollyWood & African people Choice Awards @Africannaf

MTOTO WA SOKOINE AFUNIKA JIMBO LA LOWASSA

Image
Namelock Sokoine.    Kwa ufupi Namelock ambaye ni mbunge wa Viti Maalumu (CCM) alipata kura 29,582 akifuatiliwa na Loota Sanare aliyepata kura 8,809 na nafasi ya tatu, ilichukuliwa na Lolinyu Mkoosu aliyepata kura 235 na Payani Leyani akipata kura 226. Linkwithin By Waandishi Wetu, Mwananchi Arusha. Binti wa Waziri mkuu wa zamani, Edward Sokoine, Namelock Sokoine ameshinda kura za maoni kugombea ubunge Jimbo la Monduli kupitia CCM huku mkwe wa Lowassa, Siyoi Sumari akishindwa Jimbo la Arumeru Mashariki. Namelock ambaye ni mbunge wa Viti Maalumu (CCM) alipata kura 29,582 akifuatiliwa na Loota Sanare aliyepata kura 8,809 na nafasi ya tatu, ilichukuliwa na Lolinyu Mkoosu aliyepata kura 235 na Payani Leyani akipata kura 226. Arumeru Mashariki:  Sumari aliyewania jimbo hilo kwa mara ya kwanza baada kifo cha baba yake Jeremia Sumari na kushindwa na Joshua Nassari wa Chadema alipata kura kura 3,664 dhidi ya 12,071 za John