Posts

Showing posts from April 1, 2018

Mpenzi wa Cristiano Ronaldo ametumia Kiswahili leo

Image
Lugha ya Kiswahili inaonekana kuzidi kukuwa na kuwavutia watu mbalimbali dunia kuitumia, leo April 1 2018 moja kati ya post za mitandao ya kijamii zilizochukua headlines ni post ya mwanamitindo  Georgina Rodríguez ambaye ni mpenzi wa staa wa soka wa Real Madrid Cristiano Ronaldo. Georgina Rodríguez ni mwanamitindo na ndio mpenzi wa sasa wa Ronaldo na wamefanikiwa kupata mtoto mmoja anayejulikana kwa jina la Alana Martina , hivyo katika insta story yake amepost picha yake na Ronaldo na kuandika ‘Hakuna Matata’ Msemo wa hakuna matata ni msemo wa Kiswahil i ambao umeonekana kupendwa na umekuwa msemo maarufu sana kwa wageni wanaopenda kujua lugha ya Kiswahili, huo huwa ni msemo wao wa kwanza kujifunza lakini haijajulkana bado  Georgina Rodríguez ameujulia wapi msemo huo.

PRETTY KIND AWAIBUA WABONGO TENA,KISA MABADILIKOYA AJABU

Image
Mrembo Suzan Michael ‘Pretty Kind’ aliyekuwa Bingwa wa picha za utupu mtandaoni ameonesha kubadilika kitabia hasa katika mitandao ya kijamii na hilo limeonekana baada ya kuanza kuutumia mtandao wake wa kiijamii wa Instagram. _ Ikiwa ni siku chache za msanii huyo kuwa huru baada ya kusamehewa kwa adhabu yake ya kifungo cha kutojihusisha na masuala ya muziki kwa muda wa miezi sita kutokana na hatua za Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo dhidi ya kukiuka maadili kupitia Naibu wa wizara hiyo Mhe. Juliana Shonza mwezi Januari mwaka huu.   Hizi ni picha baadhi za Msanii huyo ambazo anaonekana kubeba kitabu kitakatifu ‘Biblia’ na kuandika kuwa Mwenyezi Mungu kwa sasa anaweka sawa mambo ya kila kilichotoka katika mstari wake.

Rais Magufuli Aungana na Wakristo Kuadhimisha Misa ya Pasaka Kanisa la Mt. Joseph Dar

Image
Rais Magufuli leo ameungana na Wakristo wote Tanzania katika maadhimisho ya Misa Takatifu ya sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Joseph, Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakilakiwa kwa furaha na Paroko Msaidizi Venance Tegete walipojumuika na waumini wengine katika Maadhimisho ya Misa ya Sikukuu ya Pasaka katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam leo Jumapili Aprili 1, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli na waumini wengine wakisikiliza kwa makini mahubiri ya Paroko Msaidizi Venance Tegete katika Maadhimisho ya Misa ya Ibada ya sikukuu ya Pasaka katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam leo Jumapili Aprili 1, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoa sadaka katika Maadhimis

Meli ya abiria ya Uingereza iliyozamishwa mwaka 1942 yaondolewa baharini

Image
Meli ya abiria ya Uingereza iliyozamishwa wakati ilishambuliwa kwa bomu na ndege za Japan wakati wa vita vya pili vya dunia, imeinuliwa kutoka baharini pwani mwa Sri Lanka baada ya miaka 75. SS Sagain, ambayo abiria wake wengi na mizigo iliokolewa mwaka 1942, imeinuliwa na kundi la wapiga mbizi kutoka kwa jeshi la wanaji wa Sri Lanka, Ilikuwa karibu umbali wa futi 35 chini ya bahari katika bandari ya Trincomalee. Shughuli ya kuiinua meli hiyo ilichukua miezi kadhaa na ilifanywa na kikosi cha wanamaji cha Mashariki mwa Sri Lanka.

RAY C ATIBUKA VIBAYA,ATOA MANENO TATA KISA LADY JAY DEE,ASEMA BORA ATIWE MIMBA AZAE

Image
Muimbaji Ray C amefunguka mazito kwa kile anachoona kinaenda ndivyo sivyo katika muziki wa Bongo Flava kwa sasa. Ray C amefikia hata hatua ya kutumia maneno makali kueleza hisia zake kwa yale ambavyo hakubaliani nayo kwenye tasnia hiyo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika; Kuna muda huwa nafikiria mambo mengi sana! kuna muda najiskia kuamua kutiwa mimba, nizae niwe tu mama wa nyumbani! maana kuna muda nikiangalia wasanii wenye maendeleo kwenye Bongo Flava ni wachache saaaaana! na sijiongelei mimi maana mimi mwenyewe kuna wakati nilivurunda mwenyewe! Nakubali nilibugi na nikagundua nimebugi haswa na ndio maana nimepambana mpaka hapa niliko baada ya kugundua baraka tele nilizozawadiwa na Mungu ni kubwa mno kuliko starehe za muda za ndogo na za kibwege!!! Ila huwa nakaa najiuliza miaka kama sita ambayo nilipotea kwenye industry! kuna wasanii nilianza nao na wana vipaji vya ajabu maskini lakini wengi wao wamezimwa kama taa!!! Namkumbuka Nature, Joseline, B

Halima Mdee Akamatwa na Polisi Akitokea Afrika Kusini

Image
Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee. Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee. Mdee amekamatwa leo alfajiri uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea nchini Afrika Kusini inakoelezwa alilazwa kwa matibabu. Meya wa Ubungo, Boniface Jacob amethibitisha kukamatwa kwa Halima Mdee ambapo amesema; “Ni kweli amekamatwa leo Saa 9 alfajiri Airport, akitokea Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu na sasa yupo Central.” Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) huenda akaunganishwa na vigogo wengine sita akiwamo Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe katika kesi inayowakabili. Vigogo hao wengine tayari wamekwisha kupandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, Dar es Salaam na kusomewa mashtaka nane. Kukamatwa kwa Mdee kunafikisha watuhumiwa saba kati ya nane ambao wamekwisha kuhojiwa mwingine ambaye bado na huenda anatafutwa na jeshi hilo ni mbun

ZARI THE BOSS LADY AKINUKISHA KUTUA BONGO NA KUTOENDA MADALE.MAMA YAKE DIAMOND ATIBUKA

Image
DAR ES SALAA: Zarinah Hassan ‘Zari The Boss lady’, aliyekuwa baby mama wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu abdul ‘Diamond Platnumz’, amekinukisha ile mbaya baada ya kutua Bongo na kutokwenda nyumbani kwa jamaa huyo, Madale-Tegeta jijini Dar, risasi Jumamosi limenyetishiwa. ATUA USIKU WA MANANE, AFIKIA HOTELINI Zari alitua Dar usiku wa manane wa Jumanne iliyopita na kufikia katika Hoteli ya Hyatt Regency The Kilimanjaro, zamani Kempinski iliyopo Posta, Dar na mapema kesho yake (Jumatano iliyopita), alisaini dili nono na Kampuni ya Softcare. Zari alisaini dili hilo la mamilioni, tukio lililofanyika mbele ya vyombo vya habari kwenye ukumbi wa hoteli hiyohiyo na sasa akawa ndiye balozi mkuu wa pampers za watoto zinazosambazwa na kampuni hiyo. Zari The Boss lady akiwa na Diamond. AULIZWA KUHUSU DIAMOND Katika zoezi hilo la kusaini dili hilo, ulipofika muda wa maswali, Zari aliulizwa juu ya uhusiano wake na Diamond ambapo ‘aliwaka’ na kusema kwamba, kilichomleta Bongo ni dili