Posts

Showing posts from May 24, 2018

‘Vita’ ya Alikiba na Samatta Imefika Pabaya

Image
NAHODHA wa Timu ya Soka ya Tanzania, Taifa Stars na Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji, Mbwana Ally Samatta ameingia kwenye vita ya ki-sport na msanii wa Bongo Fleva, Alikiba inayotarajiwa kufanyika Juni 9, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhamasisha uchangiaji wa vifaa na miundombinu katika mashule. Samatta amesema mechi hiyo itakuwa itamuhusisha yeye na marafiki zake dhidi ya Alikiba na marafiki zake pia. “Itakuwa mechi ya hisani kama zilizo nyingine ambazo zimekuwa zikifanywa na wachezaji wakubwa, hii ni kati ya Samatta 11 na Alikiba 11, nitachagua marafiki zangu na Kiba atachagua marafiki zake. Nataka nifanye moja lakini itakuwa na radha tofauti, kwani timu pinzani itakuwa ya Alikiba. “Ok, nimepewa jukumu la kuandaa jeshi la maangamizi mchezaji gani ungependa kumuona siku iyo awe wa sasa au wa zamani?” amesema Samatta. Alikiba amesema amefurahi urafiki wake na Samatta kuzalisha kitu hicho kizuri huku akiwaomba wapenzi n

DKT ABBASI: MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO IMARISHENI USHIRIKIANO NA WATENDAJI WA KADA TOFAUTI KUTANGAZA MAFANIKIO YA SERIKALI

Image
MAAFISA Habari na Mawasiliano Serikalini  wametakiwa kujenga timu ya ushirikiano wa pamoja na Wataalamu wa kada mbalimbali waliopo katika maeneo yao ya kazi ili kutangaza vyema mafanikio ya miradi na program zilizotekelezwa na zinazotekelezwa na Serikali. Hayo yamesemwa jana Mkoani Arusha na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi wakati wa mwendelezo wa ziara yake ya siku tano ya kutembelea na kujionea utendaji kazi wa Vitengo vya Habari na Mawasiliano Serikalini katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali za Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro. Dkt. Abbasi alisema malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kuwa watendaji wote wa Serikali wanakuwa mstari wa mbele katika kuwaletea maendeleo ya haraka  wananchi wake kwani Serikali inajenga nyumba moja, hivyo ni wajibu wa watumishi wote kuungana pamoja katika kusukuma mbele gurudumu hilo hususani katika maeneo ya Mikoa na Halmashauri ambapo Serikali hupeleka kiasi kikubwa

MAGAZETI YA TANZANIA LEO ALHAMISI, MEI 24, 2018

Image