Posts

Showing posts from February 26, 2018

Breaking News: Sugu, Masonga Wahukumiwa Jela kwa Kumkashifu JPM

Image
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga, wamehukumiwa kifungo cha miezi mitano jela kila mmoja baada ya kukutwa na hatia ya  kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Mahakama imetoa uamuzi huo leo Jumatatu, Feb. 26, 2018 na hakimu wa mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mhakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, Maiko Mteite,  baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa upande wa mashtaka. Pia mahakama hiyo imemhukumu kifungo cha miezi mitano Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini,  Emmanuel Masonga,  kwa kosa hilo. Washtakiwa hao wanatajwa kutenda kosa hilo Desemba 30, 2017 katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya wakati wakiwahutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara.

Shy-Rose Bhanji Akanusha Kupinga Utawala wa JPM

Image
ALIYEWAHI kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shy-Rose Bhanji amekanusha taarifa ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikidai kuwa anapinga utawala wa Rais Dkt. John  Magufuli. Taarifa hiyo ilionekana imeandikwa kwenye akaunti yake rasmi ya Instagram lakini  amesema ilikuwa imedukuliwa na watu wasiojulikana ambao wali-post ujumbe huo wenye nia ya kumchonganisha na Rais. “Account yangu ya Instagram ilikuwa hacked na watu wasiojulikana ambao walipost vitu ambavyo sihusiki navyo. Naomba radhi kwa Rais wangu JPM na wote waliokerwa na jambo hilo,” ameandika ShyRose.

TAUSI AFUNGUKA KUACHA ‘NIDO’ NJE

Image
KOMEDIANI mwenye jina kubwa Bongo, Tausi Mdegela amefungukia ishu ya kuacha matiti ‘nido’ zake nje kisha kutupia picha kwenye ukurasa wake wa Instagram alipokuwa akiogelea kwenye jakuzi kuwa, ni hali ya kawaida kwa maana hawezi kuogelea akiwa amevaa suti, bali lazima avae nguo za kuogelea. Akizungumza na Over Ze Weekend Tausi alisema kuwa, hakuona cha ajabu kama watu walivyochukulia, lakini ni jambo la kawaida kwani mtu hawezi kuogelea akiwa amevaa vitenge na ndivyo ilivyokuwa kwake na hakuna na maana nyingine.   “Nilivaa mavazi ya kuogelea, nisinge-weza kuvaa vitenge au suti nikaogelea maana watu wanachunguza sana,” alisema Tausi asiyeishiwa na vituko. Imelda Mtema, Ijumaa Wikienda.

ZAMARADI AWA MTANGAZAJI WA KWANZA KUINGIA WASAFI RADIO NA TV

Image
BREAKING NEWS : WASAFI TV wamefanikisha Kumchukua @zamaradimketema ….pichani wakiwa Zanzibar kwaajili ya usaili wa watangazaji wa kituo hichO    

ANGALIA PICHA ZARI THE BOSS LADY ALIVYOTIKISA VALENTINE PARTY JIJINI LONDONI

Image
Mrembo Zari The Bosslady wikiendi hii alikuwa mmoja wa wageni katika sherehe ya Valentine Party ambayo ilifanyika katika klabu ya usiku ya Rio Nightclub, iliyopo katika wilaya ya Wood Green, Kaskazini mwa mji wa London. Zari alitokelezea akiwa na gauni lake fupi na viatu virefu vyote vikiwa na rangi nyekundu. Zari alikuwa ameambatana na muandaji wa sherehe hiyo, Lady Naaa huku Naj akiwa miongoni mwa wageni wengine waliohudhuria sherehe hiyo. Katika sherehe hiyo Rayvanny na Barakah The Prince walitumbuiza.