Posts

Showing posts from December 16, 2013

BREAKING NEWS:" MANCHESTER CITY YAPANGWA DHIDI YA BARCELONA 16 BORA CHAMPIONS LEAGUE"

Image

MGOMO WA MADAKTARI KENYA WAKITHIRI

Image
Maafisa wa afya wanaowakilisha madaktari na wauguzi wamesisitiza kuwa hawatasitisha mgomo wao hadi serikali itakapotimiza matakwa yao. Hii ni licha ya mahakama kutoa agizo kwa madaktari hao kusitisha mgomo wao ifikapo tarehe 24 Disemba.Lakini wamesema kuwa wako tayari kuendelea na mazungumzo na serikali kutafuta kusuluhisha kwa mgomo huo unaohusu wao kupokea mishahara yao kutoka kwa serikali za majimbo wala sio serikali kuu. Jumatano iliyopita waziri wa afya James Macharia alitaka mahakama kutoa agizo la kusitisha mgomo wa madaktari ambao alisema unakiuka katiba na sheria za kazi. Wagonjwa kote nchini Kenya wameachwa bila huduma za afya kufuatia mgomo wa madaktari na wauguzi ambao umekuwa ukiendelea kwa siku sita sasa. Hali hii imesababishwa na kutokuwepo maelewano kati ya serikali na chama cha madaktari nchini kuhusu serikali kuamuru madaktari walipwe na serikali za majimbo. Madaktari wanataka mishahara yao iendelee kulipwa na wizara ya afya kupitia

Kufuru, ndege ya watu 150, Malkia wa Nyuki apanda peke yake

Image
Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharoosi 'Malkia wa Nyuki'. MLEZI wa Simba, Rahma Al Kharoosi, ametua jijini Dar es Salaam akiwa kwenye ndege kubwa yenye uwezo wa kubeba watu 150, lakini yeye akiwa ndiye abiria pekee ndani ya ndege hiyo. Rahma, maarufu kama Malkia wa Nyuki, ametua na ndege hiyo aina ya Airbus 320 inayomilikiwa na Serikali ya Oman na anaitumia yeye kupitia cheo chake cha Balozi wa Heshima wa Oman nchini Morocco. Ndege hiyo ilikuwa imebeba watu 17, kati ya hao 16 ni wafanyakazi ndani ya ndege ambao ni daktari mmoja, walinzi wanne, waliobaki ni marubani na wahudumu. Akizungumza dakika chache kabla ya kuondoka nchini jana, saa 10 alfajiri, Malkia wa Nyuki alisema alishuka nchini kwa ajili ya mapumziko ya siku moja, pia kuzungumza na baadhi ya viongozi wa Simba. “Nimepita tu, tumepumzika kidogo hapa na baada ya hapo ninakwenda Comoro kwa ajili ya kuzungumza na kumchukua R

ANGALIA DRAW YOTE YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

Image
  Round of 16 Man. City (ENG) vS  Barcelona (ESP) Olympiacos (GRE) vS Man. United (ENG) Milan (ITA) vS Atlético (ESP) Leverkusen (GER) vS Paris (FRA)   Galatasaray (TUR) vS Chelsea (ENG) Schalke (GER) vS Real Madrid (ESP)   Zenit (RUS) vS Dortmund (GER) Arsenal (ENG) vS Bayern (GER)

BREAKING NEWS: ANDRE VILLAS BOAS AFUKUZWA KAZI TOTTENHAM

Image
Siku moja baada ya kupokea kipigo cha kihistoria cha 5-0 kutoka kwa Liverpool wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani, klabu ya Tottenham Hotspur imemtimua kocha mkuu wa timu hiyo Andre Villas Boas. Tottenham ambao walikuwa ndio timu iliyotumia fedha nyingi kufanya usajili wakati wa dirisha la usajili, wakitumia zaidi ya paundi millioni 100, wameanza vibaya msimu huu na hivyo kufikia maamuzi ya kumtimua AVB ambaye alijiunga na timu hiyo miezi takribani 18 iliyopita. Majina ya Luis Enrique na Fabio Capello yameanza kutajwa kuja White Hart Lane kuchukua nafasi inayoachwa wazi na kocha huyo wa zamani wa Chelsea na Porto.

BAADA YA KUPONA KATIKA UTEJA, RAY C AAMUA KUJIACHIA KIHASARA HASARA ... MTAZAME ANAVYOACHIA MAUNGO

Image
JE, HUYU NDIO YULE BINTI KIUNO BILA MFUPA?  TUPIA MAONI YAKO A USISAHAU KULIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK/TWITTER

FAHAMU JINSI YA KUONGEZA MVUTO KWA MPENZI WAKO

Image
Kama umeshushwa thamani unakuwa kwenye hatari ya kuachwa. Hata kama mwenzako alikuwa ameshafikiria suala la kuingia kwenye ndoa na wewe lakini kwa sababu ameshakushusha thamani ndoa inaweza kuyeyuka. Ukiwa kwenye ndoa ni hatari zaidi maana mwenzako hukuchukulia wa kawaida – mazoea huzidi na hapo ndipo uhitaji wa kuwa na mwingine wa pembeni unapoanzia. Haoni cha muhimu tena kwako, ndiyo maana wazo hilo huvamia ubongo wake kwa kasi sana. Itafikia hatua, kama upo ndani ya ndoa, mwenzako atagoma kuongozana na wewe na kama ikitokea hivyo mkikutana na rafiki zake njiani hatakutambulisha. Hisia kwamba hamuendani humwingia. UNAFANYAJE SASA? Kubwa unalotakiwa kufahamu rafiki yangu mpendwa, suala la kupanda au kushuka thamani lipo mikononi mwako. Yapo mambo ambayo ukiyazingatia, mwenzako hawezi kukuchoka na kufikia hatua ya kukushusha thamani. Tayari tumeshaona athari zake lakini hapa sasa nataka kukupa mbinu ambazo ukiwa nazo makini basi itakuwa rahisi kwako kubaki na

UNAHISI NI KWANINI HOTUBA YA JK KUMUAGA MANDELA ILIKUWA BORA?

Image
NOTHING can come from NOTHING. Wamesema hili Wanafalsafa wa Uyunani ya Kale . Nimemwona na kumsikiliza Rais wetu Jakaya Kikwete akizungumza kwenye siku muhimu ya kumuaga kwa mara ya mwisho Mzee wetu Nelson Mandela. Muda wote wa hotuba yake, JK alibaki kwenye mstari kwa namna ile ile ya kuweka bayana kwa ulimwengu, kuwa ' msione vinaelea'. Hakika alichofanya JK leo ndicho haswa alipaswa kukifanya, na amekifanya kwa kutumia weledi wake kwenye diplomasia na kuchanganya uzoefu wake kwenye uongozi wa kisiasa na dola kwa ujumla. Ni kuitumia fursa ile ambapo macho na masikio ya dunia yalielekezwa Quni, kwa yeye rais kuiambia dunia, na si kuisubiri CNN au vyombo vya habari vya Kimagharibi kuifanya kazi hiyo, juu ya mchango wa Tanzania katika harakati za ukombozi wa bara la Afrika ikiwamo mchango wa Tanzania kumfanya Mandela na viongozi wengine wa Kiafrika kuonekana kama walivyoonekana kwenye macho ya dunia. Hakika, JK anastahili pong

UKITAKA KUJUA MADEMU WA KIBONGO NI BALAA, NI HATARI, NI SHIDA TUPU .... TAZAMA PICHA HIZI ZA AINA YAKE

Image

REGNAND MENGI AJIBU TUHUMA ALIZOZUSHIWA

Image
1.      Nafurahi kwa nafasi ya kuwa nanyi leo kwa kuwa sekta binafsi itapata nafasi ya kipekee  kesho tarehe 16 Desemba 2013, ya kuwa na mkutano chini ya Mhe. Rais Kikwete kama mwenyekiti. 2.     Mimi binafsi nitapata heshima ya kushiriki kama kiongozi wa sekta binafsi chini ya TPSF. Lakini limekuwepo tatizo la mambo yaliosemwa na Mhe. Profesa Muhongo kunihusu ambayo ningependa niyafafanue ili nisiende kwenye kikao cha kesho zikiwepo fikra kwamba mambo hayo ni ya kweli. 3.     Katika tarehe za mwanzo wa mwezi Septemba mwaka 2013 Mhe. Profesa Muhongo alinukuliwa akisema kwamba:  “Mengi hana uzawa bali ubinafsi. Anataka kufanya udalali wa vitalu vya raslimali zetu. Waelezeni Watanzania ukweli huu.” 4.   Ukweli ni kwamba mimi siyo mbinafsi na pili sijawahi kuomba upendeleo wa kupewa kitalu cha gesi bali ninapigania Watanzania kwa ujumla. 5.   Tarehe 8 Desemba 2013, alipok

WEMA AFUMANIWA TENA NA MARTIN KADINDA WAKIWA HOTELINI KWENYE MAPOZI YA UTATA ... WAPATWA NA KIGUGUMIZI

Image
Wema na Kadina

Angalia Picha Aliyekuwa Mwenyekiti CCM wa mkoa wa Mwanza na Diwani wa Kata ya Kisesa, Mhe. Clement Mabina Auwawa na Wananchi Kwa Mawe

Image
Mwili wa Aliyekuwa Mwenyekiti CCM wa mkoa wa Mwanza na Diwani wa Kata ya Kisesa, Mhe. Clement Mabina baada ya kushambuliwa  Mwili wa Aliyekuwa Mwenyekiti CCM wa mkoa wa Mwanza na Diwani wa Kata ya Kisesa, Mhe. Clement Mabina baada ya kufikishwa  hospitali ya rufaa Bungando. Aliyekuwa Mwenyekiti CCM wa mkoa wa Mwanza na Diwani wa Kata ya Kisesa, Mhe. Clement Mabina enzi za uhai wake ---  Aliyekuwa Mwenyekiti CCM wa mkoa wa Mwanza na Diwani wa Kata ya Kisesa, Mhe. Clement Mabina  ameuwawa na wananchi wenye hasira kwa kupigwa na mawe na silaha za jadi mwendo wa saa saba mchana. Imeelezwa kuwa sababu ya kumwuua Mabina inatokana na ugomvi wa ardhi ambapo kesi ya eneo hilo ilikuwa ikiendelea mahakamani, lakini mchana wa leo, marehemu Mabina alionekana akipanda miti na kuweka mawe ya msingi katika eneo lenye ugomvi na wananchi walipomhoji kuhusu kibali cha mahakama cha kufanya hivyo, inaripot