Posts

Showing posts from November 29, 2016

Rais Magufuli Afanya Ziara ya Kushtukiza Gereza la Ukonga Dar

Image
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini kitabu cha wageni akiwa na  Kamishna Mkuu wa Magereza John Casmir Minja kabla ya kuongea na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam leo Novemba 29, 2016        Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipewa muhtasarai wa kazi  na Kamishna Mkuu wa Magereza, John Casmir Minja kabla ya kuongea na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam leo Novemba 29, 2016 Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na baadhi ya maafisa na askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo Novemba 29, 2016. Askari wakiwa na shauku ya kutoa kero zao mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli alipoongea  na  

Pedeshee Ndama Kortini Kwa Kugushi Nyaraka na Kutakatisha Bil 1.77

Image
DAR ES SALAAM: Mfanyabiashara wa jijini Dar, Ndama Shaaban Hussein almaarufu Pedeshee Ndama Mutoto ya Ng’ombe, aliyewahi kuwa mfadhili wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ leo amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa kosa la utapeli wa dola za Kimarekani 540, 390 sawa na zaidi ya shilingi bilioni 1.18. Ndama amesomewa mashtaka sita mbele ya Hakimu Victoria Nongwa na Mwendesha Mashtaka Leonard Msigwa akisaidiana na Christopher Challo kuwa, mnamo Februari 20, 2014 mkoani Dar, Ndama alitengeneza nyaraka feki, zikionesha kupata kibali cha kusafirisha sampuli za madini ya dhahabu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC). Shtaka la pili, tatu na nne pia yalikuwa ya kugushi nyaraka, ikiwemo iliyotoka Umoja wa Mataifa, iliyoisafisha kampuni yake ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Ltd kuwa imeruhusiwa kusafirisha maboksi manne ya dhahabu. Nyaraka hizo zililenga kuiaminisha Kampuni ya Trade TJL DTYL Lt

Wananchi wa Cuba Watoa Heshima za Mwisho Kwa Mwili wa Rais Fidel Castro

Image
HAVANA, CUBA: Maelfu ya raia wa Cuba wanatoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi mwanamapinduzi Fidel Castro, aliyeaga dunia Ijumaa iliyopita akiwa na umri wa miaka 90. Ikiwa ni siku ya kwanza ya kipindi cha siku tisa za maombelezi rasmi ya kifo chake, misafara mirefu imeshuhudiwa katika uwanja wa Revolution Square katika Mji Mkuu Havana, sehemu ambayo waombolezaji wameweka picha ya kiongozi huyo akiwa ameshika bunduki. Siku za maombolezi zitakamilika baada ya majivu ya mwili wake kuzikwa siku ya Jumapili. Majivu ya Castro yalitazamiwa kuwasilishwa kwa umma katika uwanja wa Revolution Square lakini yamewekwa katika sehemu tofauti. ‘Roho ya Cuba’ Wananchi wengi wa Cuba walikuwa katika milolongo hata kabla ya alfajiri kuwadia ili kuhakikisha wako miongoni mwa watu wa kwanza kutoa heshima zao. Tania Jimenez, mwenye umri wa miaka 53, mwanahisabati, ameliambia shirika la habari la AP kwamba Fidel ni kila kitu kwao, na ni kiungo muhimu kwa nchi hiyo

Daktari Feki Afanya Upasuaji Wagonjwa 9 na Kufariki Mmoja, Apewa Ofa ya Kujiendeleza Kielimu

Image
KENYA: Kamati ya maswala ya afya nchini Kenya imependekeza daktari feki aliyekamatwa nchini humo aruhusiwa kujiendeleza na masomo ya udaktari badala ya kutumikia kifungo gerezani. Kauli hiyo imetolewa baada ya kubainika kuwa daktari huyo feki alifanikiwa kufanya upasuaji kwa wagojwa tisa ambao kati ya yao wanane walipona na mmoja ambae alikuwa mjamzito ndiye aliyepoteza maisha huku akifanikiwa kumuokoa mtoto aliyekuwemo tumboni mwa mjamzito huyo.

Njama 638 za Mauaji Alizoepuka Rais Fidel Castro

Image
Njama ya kutumia sigara kumuua Fidel Castro ambayo ilitibuka inajulikana sana, lakini njama nyengine 637 dhidi ya maisha yake ni zipi? Shirika la kijasusi nchini Marekani CIA na watu waliotoroka Cuba wakati wa uongozi wa Castro walitumia nusu ya karne moja kufanya njama za kumuua kiongozi ambaye taifa lake lina athari kubwa kwa Marekani, kulingana na balozi wa Marekani nchini Cuba Wayne Smith. Wakati mmoja kiongozi huyo wa Cuba alinukuliwa akisema, iwapo kuepuka majaribio ya mauaji kungekuwa miongoni mwa michezo ya Olimpiki ningejishindia medali ya dhahabu. Mpenzi wa zamani wa Castro, Marita Lorenz alipewa dawa za sumu kumwekea katika kinywaji chake Hatahivyo baadhi ya njama hizo hazikutekelezwa, kulingana na aliyekuwa mlinzi wa zamani wa Fidel Castro, Fabian Escalante. Stakhabadhi zilizofichuliwa wakati wa utawala wa Bill Clinton zilionyesha kuwa CIA wakati mmoja walianza kuwafanyia utafiti konokono wa eneo la Carebean. Njama, ilikuwa kutafuta konokono mmoja

Chanjo Dhidi ya Ukimwi Kuanza Kufanyiwa Majaribio Kesho Jumatano

Image
AFRIKA KUSINI: Chanjo mpya dhidi ya virusi vinavyosababisha Ukimwi itaanza kufanyiwa majaribio nchini Afrika Kusini Jumatano wiki hii. Wanasayansi wanasema huenda ikawezesha binadamu kukabiliana na virusi hivyo iwapo itafanikiwa, Shirika la Habari la AP linasema. Wakati wa majaribio hayo, ambayo yamepewa jina HVTN 702, wanasayansi wanatarajiwa kuwatumia wanaume na wanawake 5,400 ambao wanashiriki ngono kutoka maeneo 15 nchini Afrika Kusini. Washiriki hao watakuwa wa umri wa kati ya miaka 18 na 35. Majaribio hayo yatakuwa makubwa zaidi na ya kina zaidi ya chanjo ya Ukimwi kuwahi kufanyika nchini Afrika Kusini ambapo zaidi ya watu “Ikitumiwa pamoja na silaha tulizo nazo sasa za kuzuia maambukizi, chanjo hiyo inaweza kuwa msumari wa mwisho katika jeneza la Ukimwi,” Anthony Fauci, mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Maradhi ya Kuambukizana na Mzio ya Marekani (NIAID) amesema kupitia taarifa. “Hata kama mafanikio yake yatakuwa ya kadiri, hilo linawez

Kesi ya Mke wa Bilionea Msuya Yaahirishwa Tena

Image
DAR ES SALAAM: Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imeahirisha kutoa uamuzi wa maombi ya Miriam Msuya aliyekuwa mke wa bilionea jijini Arusha, marehemu Erasto Msuya, kuhusu kufutiwa mashitaka ya madai ya kumuua wifi yake, Anethe Msuya yaliyotokea Mei 25, mwaka huu, Kigamboni, Dar. Miriam Msuya akitoka mahakamani baada ya kesi kuahirishwa. Uamuzi huo ungetolewa leo lakini kesi imeahirishwa kwa kuwa, Hakimu Mkazi Magreth Bankika anayesikiliza kesi hiyo, hakuwepo mahakamani. Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Victoria Nongwa, alisema kesi ilitajwa kwa ajili ya kutolewa uamuzi lakini hakimu anayeisikiliza hakuwepo hivyo uamuzi utatolewa Desemba 8, mwaka huu. NA DENIS MTIMA/GPL