Posts

Showing posts from May 23, 2018

Tende, Maji Zinavyofaa Wakati wa Mfungo wa Ramadhani

Image
V YAKULA vinavyofaa kuliwa wakati huu wa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni vingi, leo tutaanza kuchambua kimoja baada ya kingine, Mbali na Waislamu, uchambuzi huu unawafaa pia wale ambao siyo Waislamu. Chakula kilichozoeleka zaidi kwa futari ni tende. Baada ya kushinda kutwa nzima na Swaumu, kiwango cha sukari ya mwili hupungua na hivyo, kuhitaji kujazilizwa tena. Aina ya kwanza ya sukari itumikayo mwilini na hasahasa ubongoni ni glukosi. Mshuko wa sukari walioupata wale ambao hawakula au kunywa kwa kipindi kirefu, unaweza kusababisha ulegevu wa mwili. Pindi sukari inapoliwa kwa njia ya chakula au kinywaji, viwango vya glukosi ya mwili hujisawazisha vyenyewe na kumfanya mtu aliyefunga asijihisi kuchoka sana na huwa na nuru zaidi ya macho. Ingawaje tende, mara nyingi, si chakula kinachopendelewa sana na watu wenye njaa, lakini ndicho chakula kisicho na mafuta, na ni chanzo madhubuti cha sukari. Nusu ya sukari zitolewazo na tende ni kwa aj

Hamisa Mobetto afunguka kuhusu kupigwa na mama Diamond

Image
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amefunguka kuhusu taarifa zilizodai kuwa amepigwa na mama mzazi wa Diamond Platnumz, Sanura Kassim ‘Sandra’. Hapo jana katika uzinduzi wa kipindi cha Nyumba ya Imani cha Wasafi TV, Hamisa alipata time ya kuzungumza na waandishi wa habari na kusema jambo hilo ni binafsi zaidi ila kugombana kwa binadamu ni kitu cha kawaida. “Hilo siwezi kuliongelea, yeah!. is too person, is too private, is too family. Hata vikombe kwenye kabati vinagong’ana, so sisi binadamu vinaweza kutokea,” amesema. Alipoulizwa iwapo kwa sasa yeye na mama Diamond wana maelewano mazuri, alijibu; ‘Sina kinyongo na mtu, sina bifu na mtu, mimi am just fine, may be yeye mwenyewe sio upande wangu wa kuweza kuelezea,’. Taarifa za Hamisa kupigwa na mama Diamond zilianza kusambaa Jumatatu ya wiki iliyopita, May 14, 2018 ambapo usiku ya jana yake Hamisa na Diamond walihudhuria katika uzinduzi wa filamu ya Aunt Ezekiel ‘Mama’ na baada ya hapo anadaiwa waliongozana hadi Madale

HEKO RAIS JPM TUKO NYUMA YAKO

Image

Wanaowania Tuzo za Ligi Kuu Bara Msimu wa 2017/18 Yaanikwa

Image
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeanika majina ya wachezaji wanao wania tuzo za Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (VPL) msimu wa mwaka 2017/18 ambazo zitatolewa Juni 23, 2018 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. TFF imesema kuwa mwaka huu wameongeza tuzo ya mwamuzi bora msaidizi ambayo haikuwepo hapo awali ikiwa na lengo la kuthamini nafasi na mchango wa waamuzi wasaidizi katika mchezo wa soka hapa nchini. Tuzo zitakazotolewa ni za Timu Bingwa, Mshindi wa Pili, Mshindi Tatu, Wanne, Mfungaji Bora, Timu yenye nidhamu, ‘ Under Twenty Player ’, mchezaji bora chipukizi, Mwamuzi bora msaidizi, Mwamuzi bora, Kipa bora na kocha bora, Goli Bora, ‘VPL Best Eleven’, Mchezaji wa heshima huku zawadi zikitarajiwa kutangazwa siku za huvi karibuni. Kamati ya tuzo ya TFF imekamilisha orodha ya wachezaji 30 watakao wania tuzo hizomsimu huu wa mwaka 2017/18. Kwenye majina ya wachezaji 30 waliyo orodheshwa kuwania tuzo hizo watachujwa mpaka kufikia 10 kisha watatu na kuta

Ashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kulawiti watoto watatu mtwara

Image
Mwanaume mmoja anayejulikana kwa jina la Mohamedi Kaisi Hamisi mwenye miaka 47 mkazi wa kijiji cha Kawawa mkoani Mtwara, anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa tuhuma za ulawiti. Akizungumza na www.eatv.tv, Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara Lucas Mkondya amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema kwamba mwanaume huyo anatuhumiwa kulawiti watoto watatu wenye miaka 13, 14 na 15, wa shule ya msingi Kawawa, walipokuwa wanatafuta Nazi kwenye minazi iliyopo vichakani baada ya kutoka Kamanda Mkondya amesema kwamba baada ya kuwakuta watoto hao mtuhumiwa aliwatishia maisha kabla ya kufanya kitendo hicho cha kinyama katika eneo la Nambonde. Hata hivyo baadhi ya wananchi waliokuwepo baada ya mtuhumiwa kukamatwa (Nassoro Abdala Nyoya, Sharifa Hassani na Julieta Athanas) kwa masikitiko makubwa wameiomba serikali ichukue hatua kali kwa mtuhumiwa ili iwe fundisho kwa wengine.

BREAKING NEWS: KESI YA BABU TALE YAAHIRISHWA, ARUDISHWA MAHABUSU

Image
Mkurugenzi wa Kampuni ya Tip Top Connection ya jijini Dar es Salaam na Meneja wa mwanamuziki Naseeb Abadul ‘Diamond’, Hamis Taletale ‘Babu Tale’, leo amefikishwa katika Mahakama Kuu jijini Dar ambako baada ya hakimu aliyetoa amri ya kumkamata kutokuwepo kesi imeharishwa na Babu Tale atarudishwa mahabusu ya Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam. Kipindi cha nyuma mahakama hiyo ilimwamuru Babu Tale alipe Sh. milioni 250 Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kiasi hicho baada ya kupatikana na makosa ya ukiukwaji wa haki za hakimiliki kwa kutumia masomo yake kibiashara bila ridhaa yake kinyume cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki. Hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Agustine Shangwa, Februari 18, mwaka juzi, katika kesi ya madai namba 185 ya mwaka 2013, iliyofunguliwa na Sheikh Mbonde aliyewalalamikia ndugu hao kutumia mahubiri yake kibiashara bila ridhaa yake.

Mambo 8 Usiyoyajua Ndoa ya Kifalme ya Meghan na Prince Harry

Image
Prince Harry Akiwa na Mkewe Rachel Meghan Markle SI kipindi kirefu kimepita tangu watu wengi duniani wajiulize itakuwaje siku ya ndoa ya mwanadada ambaye ni muigizaji maarufu Marekani, Rachel Meghan Markle na mtoto wa Mfalme wa Wales, ambaye pia ni mjukuu wa Malkia Elizabeth II, aitwaye Prince Harry. Wengi walijiuliza ukubwa wa harusi hiyo, mastaa watakaohudhuria watakuwa wamevaa vipi, maharusi watakuwa kwenye muonekano upi, vituko gani vitatokea na mengine mengi! Lakini hayawihayawi hatimaye yamekuwa! Kila kitu kimejulikana baada ya Jumamosi iliyopita, watu kutoka sehemu mbalimbali duniani kusimamisha shughuli zao kushuhudia tukio hilo la kihistoria, ambapo ndoa ilifungwa kwenye Kanisa la Kifalme la St. George la Anglican na kuhudhuriwa na watu wengi mashuhuri Kama yalivyokuwa mategemeo ya wengi, yapo mambo mengi yaliyojiri kwenye ndoa hiyo. Inawezekana umeyasikia tu lakini huyafahamu kiundani au hujayasikia kabisa. Basi usijali, Risasi Vibes inakumegea kwa

RIPOTI MPYA AFYA YA MZEE MAJUTO INDIA

Image
Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ ZIKIWA zimepita siku 19 tangu mkongwe wa vichekesho Bongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ apelekwe nchini India kwa matibabu, ripoti mpya ya afya yake imetoka, Risasi Mchanganyiko linayo. Akizungumza na Risasi Mchanganyiko , Ashraf ambaye alijitambulisha kuwa ni mtoto wa Mzee Majuto alieleza kwamba, kwa sasa afya ya Mzee Majuto inaendelea vizuri, tofauti na alivyokuwa hapa nchini licha ya kwamba bado anaendelea na matibabu. “Kwa sasa baba anaendelea vizuri kwa kweli, tumewasiliana na waliopo naye kule hospitalini India, wanasema hali yake imeanza kutengemaa tofauti na alivyokuwa hapa Bongo. Kwa sasa ni hayo tu, mengine familia itazungumza zaidi baadaye,” alisema Ashraf. MKE WA MAJUTO AFANYA SIRI Risasi Mchanganyiko liliwasiliana na mke wa Mzee Majuto, Aisha Yusuf ambaye yupo hospitalini na mumewe huko India na kumuuliza kuhusu maendeleo ya mgonjwa ambapo mahojiano yalikuwa hivi; Risasi Mchanganyiko: Habari mama, vipi Mzee Majuto

Mkuu wa Wilaya amwaga machozi kwa kipigo walichopata Wananchi wake

Image
Mkuu wa Wilaya ya Rombo Agnes Hokororo ametoa machozi baada ya kukuta wananchi wa eneo la Samanga katika eneo la Useri kulalamikia jeshi la polisi kushirikiana na majambazi katika kuwapiga pamoja na kuwadai rushwa ili waweze kuachiwa pale wanapokamatwa. DC Hokororo amelaani pia kitendo cha wananchi kujichukulia sheria mikononi na kumuua jambazi anayetuhumiwa kuwaibia wananchi kijijini hapo.

BABU TALE ARUDISHWA MAHABUSU KISA MIL 250

Image
Mkurugenzi wa Kampuni ya Tip Top Connection ya jijini Dar es Salaam, Hamis Taletale. Mkurugenzi wa Kampuni ya Tip Top Connection ya jijini Dar es Salaam na Meneja wa mwanamuziki Naseeb Abadul ‘Diamond’,  Hamis Taletale ‘Babu Tale’,  jana alikamatwa kwa amri ya mahakama na kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambako baada ya hakimu aliyetoa amri ya kumkamata kutokuwepo, alirudishwa mahabusu ya Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam ili kufikishwa tena katika mahakama hiyo leo. Kipindi cha nyuma mahakama hiyo ilimwamuru Babu Tale alipe Sh. milioni 250 Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kiasi hicho baada ya kupatikana na makosa ya ukiukwaji wa haki za hakimiliki kwa kutumia masomo yake kibiashara bila ridhaa yake kinyume cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki. Hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Agustine Shangwa, Februari 18, mwaka juzi,  katika kesi ya madai namba 185 ya mwaka 2013, iliyofunguliwa na Sheikh Mbonde aliyewalalamikia ndugu hao kutu

DAWA ZAVUSHWA KUPITIA MTO WENYE MAMBA MKOANI RUVUMA

Image
  Wakazi wa vijiji vilivyopo kandokando ya mto Ruvuma wilayani Nyasa mkoani Ruvuma na wafanyakazi wa Bobari ya Dawa (MSD), wakisaidia kushusha maboksi yenye dawa na kuyaingiza kwenye mtumbwi baada ya kupelekewa na MSD Kanda ya Iringa leo na baadae kuyapeleka katika Zahanati ya Kijiji cha  Mitomoni .   Maboksi ya dawa yakiingizwa kwenye mtumbwi.   Wakazi wa Kijiji cha Mitomoni wakisubiri mtumbwi ili kuwavusha upande wa pili wa mto Ruvuma.   Dawa zikipelekwa Zahanati ya Mitomoni   Maboksi ya dawa kutoka MSD yakishushwa   Wananchi wakishusha maboksi hayo kutoka katika mtumbwi.   Mkazi wa Kijiji cha Mitomoni Khadija Salum, akizungumzia upatikanaji wa dawa kutoka MSD.   Mkazi wa kijiji hicho, Mbwana Koloma, akizungumzia changamoto ya miundombinu ya barabara na jinsi wanavyopokea dawa kutoka MSD.   Mwenyekiti wa kamati ya Afya wa Kijiji cha Mitomoni Omar Hassan akizungumza wakati wa kupokea dawa hizo. Mmoja wa viongozi wa Kiji

Huu ndio umri sahihi wa kufunga ndoa

Image
Kwa mujibu wa utafiti wa Chuo Kikuu cha Utah kilichopo nchini Marekani imebainisha kwamba watu ambao wamefunga ndoa kati ya umri wa miaka 28 mpaka 32 wamekuwa na ndoa yenye mafanikio zaidi. Utafiti huo umebainisha kwamba ndoa ambazo zipo katika hatari ya kuvunjika ni zile ambazo mmoja wa wanandoa ana umri wa chini ya miaka 20 na wale waliofunga ndoa wakiwa na umri wa miaka zaidi ya 45 na kuongeza kuwa ndoa hizo hazijadumu zaidi ya miaka mitano. Taarifa za utafiti huo umeongeza kuwa kwa watu ambao wanasubiri kufika umri wa miaka 30 ili kufunga ndoa wanahatari ya kupata shida sana katika miaka mitano ya mwanzo ya ndoa yao Awali ilijulikana kwamba watu wanaofunga ndoa katika umri mkubwa ndiyo wananafasi ndogo ya kuachana, lakini utafiti huu umeonesha kwamba watu wanaofunga ndoa katika umri wa miaka 45 uwezekano wa kupeana taraka unaongezeka kwa asilimia 5 kila baada ya mwaka mmoja. Sababu kubwa inayosababisha watu walio katika umri mkubwa kupeana taraka ni histori