Posts

Showing posts from December 29, 2017

Faida 10 za kutumia Mafuta ya Nazi

Image
1. Mafuta ya nazi kwa afya ya Moyo: Mafuta ya nazi yana asidi mhimu sana kwa afya ya moyo iitwayo ‘lauric acid’ ambayo ina uwezo mkubwa kuuweka moyo wako katika hali ya afya na furaha kwa kuidhibiti kolesteroli/lehemu mbaya katika moyo na mwili kwa ujumla. Lauric acid huongeza uwepo wa kolesteroli nzuri mwilini ijulikanayo kwa kitaalamu kama High Density Lipoprotein (HDL) huku ikiishusha ile kolesteroli mbaya ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama Low Density Lipoprotein (LDL) jambo ambalo ni mhimu kwa afya ya moyo kama anavyosema Lovisa Nilsson, mtaalamu wa lishe wa Lifesum. 2. Mafuta ya nazi huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula: Hii ndiyo moja ya faida ya mafuta ya nazi niipendayo zaidi. Ndiyo mafuta ya nazi yanayo uwezo kusaidia kudhibiti uzito uliozidi kwa sababu mafuta haya ni mepesi kumeng’enywa na hayagandi kama yalivyo mafuta mengine mazito (fatty acids) jambo linalosaidia kuuondoa uzito uliozidi mwilini. Kutokana na kitendo hiki cha kuongeza uwezo w

EBITOKE AANIKA UTAJIRI WAKE

Image
Msanii wa vichekesho hapa bongo Ebitoke, amesema kazi anayoifanya ya kuchekesha imempa mafanikio makubwa kwa muda mfupi, ikiwemo kumiliki mali zake mwenyewe. Ebitoke amesema kupitia sanaa hiyo ameweza kumiliki nyumba yake mwenyewe pamoja na gari ya kutembelea. “Hii kazi ninayofanya imenipa mafanikio sana, ingawa watu wananiona mpaka mafuta, mpaka sasa hivi nina nyumba yangu mwenyewe, na nyumba sio peke yangu ipo ya kwangu na ya bwana mjeshi ndio zipo tayari mpaka sasa, na tutazitambulisha hivi karibuni, pia nina gari yangu mwenyewe, aina gani na ya thamani gani mtaambiwa siku vitakapotambulishwa”, amesema Ebitoke. Sambamba na hilo pia Ebitoke amesema anaushukuru uongozi alionao kwa kumfikisha hapo alipo, kwani siku zote alikuwa na ndoto za kufikia malengo yake na wao ndio wamehakikisha anafikia malengo hayo.

STAA ZARI AMJIA JUU HAMISA.

Image
Bado majina ya baby mama’s wake  Diamond Platnumz  yanazidi kuchukua headlines kila kukicha katika mitandao ya kijamii, ambapo  Zari   na  Hamisa Mobetto  wamekuwa wakirushiana vijembe katika mitandao ya kijamii toka  Zari  afahamu kuwa  Hamisa   amezaaa na  Diamond . Zari  anaonekana kuendelea kurusha vijembe kupitia instagram yake na kujiita kuwa yeye ni mchepuko wa  Diamond Platnumz  kutokana na vijembe ambavyo  Hamisa Mobetto  alivirusha kwake siku chache zilizopita, Kupitia mtandao wa snapchat wa  Zari  alipost picha 7 ambazo kwa kila picha alindika caption na kusemekana kuwa kwa kile alichokiandika amemjibu  Hamisa Mobetto  juu ya vijembe vyake. “mdogoo, kila siku mdogo!! Mdogo na mzuri lakini huwezi kupata mwanaume wako….mwanamke gani haujiamin……kama unajiamini na uzuri na akili basi tuone ni mwanaume gani atakutaka baada ya hizi drama….baba wa mtoto wa tatu anakuja na atakuacha tu” “unaweza kuendele kupost picha zako za zamani na kila kitu nimetengenez

Babu Seya, Papii Kocha ‘Wapigana’ Kumuona Magufuli

Image
WASANII wa muziki wa dansi Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanawe Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ ambao kwa sasa wapo mapumzikoni wanahangaika kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili waweze kumshukuru. Msemaji wa familia hiyo ambaye pia ni msanii mkongwe wa muziki wa dansi nchini Mzee King Kiki amefunguka na kusema kuwa wasanii hao Babu Seya na Papii Kocha kwa sasa wapo mapumzikoni na kuwa wanahangaika kupata nafasi ya kuonana na Rais ili waweze kumshukuru kutokana na kuweza kuwapa msamaha mnamo Disemba 9, 2017 uliowafanya kuwa huru baada ya kutumikia jela kwa zaidi ya miaka 10.  “Saizi Nguza na Papii wapo kwenye mapumziko lakini wanapaswa kurudi nyumbani Congo kwenda kutekeleza mambo ya kimila, hivyo hawapaswi kufanya jambo lolote lile kwa sasa mpaka wakamilishe hilo suala la kimila, ila kabla ya wao kuondoka tumekuwa tukiomba kama tunaweza kupewa nafasi ya kuonana na Mhe. Rais kumshukuru na kumpa ahsante