Posts

Showing posts from January 25, 2018

Mwalimu atiwa mbaroni kwa kumuua mtoto wa miezi 7

Image
Mwalimu wa sekondari Stephen Wachira Wangara mwenye umri wa miaka 43, amefikishwa Mahakamani kwa kosa la kumuua mtoto wake wa miezi 7 kwa kumchinja na panga nchini Kenya. Mashahidi watano wa tukio hilo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Jimbo la Kirinyaga, Maina Muriuki wamemweleza Jaji Lucy Gitari wa Mahakama Kuu ya Kerugoya, jinsi mtuhumiwa alivyoua mtoto wake, Maina ameieleza Mahakama kuwa mwili wa mtoto huyo ulikuwa umewekwa ndani ya gunia ukiwa na damu, nje ya nyumba ya Wangara na pembeni ya mwili huo kuliwa na panga ambalo lilitumiwa kumuua mtoto huyo. Shahidi mwingine Joseph Muriithi amesema wakati wa tukio hilo alikuwa shambani kwa Wangara akifanya kibarua na alimwona mtuhumiwa akiwa na madoa ya damu na muda mfupi baadaye alisikia kelele kutoka kwenye nyumba ya mwalimu huyo. Mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi March 1, 2018, ambapo itasikilizwa tena. Wangara ambaye ni mtuhumiwa ni baba mwenye watoto wawili na mwalimu katika shule

AMBAKA ASKARI MWENZAKE ‘AKIMRINGISHIA’ UUME MREFU

Image
  Luteni-Kanali Chris Davies anayeshitakiwa kumbaka askari mwanamke baada ya kupiga vileo na wenzake huko Canada. ASKARI wa Uingereza aliyewahi kuwa shujaa wa vita nchini Afghanistan, hivi majuzi alimbaka askari mwenzake wa kike baada ya kujigamba kwamba alikuwa na uume mrefu. Haya yalisema mahakamani ambapo Luteni-Kanali Chris Davies anashitakiwa kwa kumbaka askari ambaye ni mama wa watoto wawili na  umri wa miaka 53 katika tukio linalodaiwa kufanyika huko Kingston, Ontario,  Canada. Davies anasemekana kumwambia mwanamke huyo kwamba: “Nina uume wenye urefu wa inchi nane (sentimita 20.3) ambao unaweza kuubomoa ulimwengu wako.” Davies anadaiwa kumwambia mwanamke huyo kwamba: “Nina uume wenye urefu wa inchi nane (sentimita 20.3) ambao unaweza kuubomoa ulimwengu wako.”  Jina na utambulisho wa mwanamke huyo vimehifadhiwa. Mwanamme huyo anadaiwa alimfuata mwanamke huyo hadi hotelini kwake baada ya mwanamkehuyo ‘kubugia’ pombe mbalimbali za kutosha walipokuwa

MWANAMKE AMWAMBIA MUMEWE ANATAMANI WANAUME WENGINE

Image
ANITA CASSIDY (40) mwanamke ambaye amekuwa katika ndoa kwa miaka ipatayo kumi, alimwambia mumewe aitwaye Marc (46) kwamba anaona maisha na ndoa ya mume na mke yamemchosha na alitaka kuwa na wenza wengine wa kufanya nao mapenzi. Katika mazungumzo ya wawili hao ambao ni raia wa Italia, mumewe alikubali kwamba wote wawili kila mmoja angekuwa na wapenzi wengine.    Lakini, je, katika ndoa moja panawezekana kuwa na watu zaidi ya wawili? Anita Cassidy (katikati) akiwa na mpenzi wake wa kiume Andrea (kushoto) na mumewe Marc (kulia) wakichangia penzi la watu watatu. “Mwaka mmoja uliopita niliweka kila kitu bayana kwenye mtandao wa Facebook kwa picha niliyokuwa na mume wangu na watoto wetu wawili.  Marafiki zangu wakaanza kuniuliza kwamba mwanamme mwingine aliyekuwa katika picha alikuwa nani.  Niliwaambia alikuwa Andrea – mpenzi wangu wa kiume. … Watatu hao wakiwa pamoja kando ya bahari wakipunga upepo. “Nafahamu wengi watashangaa kwani walijua Marc ndiye mume w

Akukumiwa Kwa kumwingilia mwanaume kinyume cha maumbile

Image
Mahakama ya Mkoa wa Mwera imemuhukumu mshtakiwa Simai Khamis Salum mwenye umri wa miaka 30 mkaazi wa Uzini wilaya ya kati Mkoa wa Kusini Unguja baada ya kutiwa hatiani kwakosa lakumuingilia mwanamme mwenziwe kinyume na maumbile. Imedaiwa Mahakamani hapo namuendesha mashtaka Rahima Kheir mbele ya hakimu Muhammed Ali Muhammed kwamba mnamo tarehe 2/3 /2015 huko Uzini bila ya ridhaa kwamakusudi amefanya kitendo hicho kwakijana mwenye umri wa miaka 20 jinalimehifadhiwa na kumsababishia maumivu makali huku akijua jambo hilo ni kosa kisheria. Akisoma hukumu Hakimu Muhammed amesema Mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa kwa upande wa mashtaka na kumuona nimkosa wakosa hilo ndipo Mahakama hiyo ilipomtia hatiani kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka saba pamoja na kumlipa fidia mtendewa yashilingi Milioni mbili ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia kama hiyo.

Mawakili wa Sugu wajiondoa kwenye Kesi

Image
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi-Mbeya, Michael Mteite, amegoma kujitoa katika kusikiliza kesi inayowakabili Mbunge Joseph Mbilinyi na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga. Mapema leo Alhamisi Januari 25,2018 Sugu na Masonga waliwasilisha ombi mahakamani wakimkataa hakimu huyo wakitaka ajitoe kusikiliza kesi kwa maelezo kuwa hawana imani naye. Hakimu Mteite amesema sababu zilizotolewa na akina Sugu hazipo kisheria na hazimfanyi kujitoa. Baada ya hakimu kukataa kujitoa, mawakili Boniface Mwabukusi, Hekima Mwasipu na Sabina Yongo wanaowawakilisha washtakiwa walitangaza kujitoa katika shauri hilo. Sugu, mwenzake wamkataa hakimu Sugu na Masonga wameiomba Mahakama kuwapatia wiki mbili za kutafuta mawakili wengine. Hakimu Mteite ameahirisha kesi hadi Februari 2,2018 na ameamuru washtakiwa kurejeshwa rumande.

Lowassa, Membe Uso kwa Uso Nyumbani kwa Gwajima

Image
Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa akiteta na Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani, Bernard Membe walipokutana leo katika msiba wa mama mzazi wa Askofu Josephat Gwajima nyumbani kwake Salasala, Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni  Mbunge wa Vunjo, James Mbatia;  Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema,  Bernard Membe  na Lowassa wakiwa kwenye msiba huo. WAZIRI Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa wamekutana na kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani, Bernard Membe leo katika msiba wa mama mzazi wa Askofu Josephat Gwajima nyumbani kwake Salasala jijini Dar es Salaam. Lowassa na Membe ni miongoni mwa viongozi waliochukua fomu kusaka ridhaa ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa 2015, ambapo jina la Lowassa lilienguliwa huku Membe akiingia hatua ya tano licha ya kushindwa katika hatua ya tatu bora.  Baada ya jina lake kuen