Posts

Showing posts from August 21, 2015

SHUHUDIA DK. MAGUFULI ALIVYORUDISHA FOMU ZA URAIS NEC LEO

Image
  Mgombea urais kupitia CCM Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damiani Lubuva, wakati alipowasili ofisi hizo. …Akiwa na mgombea mwenza, Samiah Hassan Suluhu. Viongozi wa CCM waliomsindikiza mgombea wao wa urais. Lubuva (kulia) akizungumza jambo wakati wa kurudisha fomu hizo. Magufuli akionyesha fomu wakati wa kurudisha. Mgombea urais kupitia CCM Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wanahabari baada ya kurudisha fomu. Wanahabari wakiwa kazini katika hafla hiyo. Magufuli akitoka ofisi za NEC baada ya kukamilisha zoezi hilo. MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, John Pombe Magufuli, leo amerudisha fomu ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). NEC iliwataka wagombea wote wa urais kupitia vyama vyote vya siasa kurudisha fomu leo Agosti 21 baada ya kuzunguka mikoa ya Tanzania kutafuta wadhamini, ambapo vyama vyote hivyo viwili vimeonekana kukidhi vigezo na kurudisha fomu hizo. (PICHA: DENIS MTIMA/GP

LOWASSA, DUNI WARUDISHA FOMU TUME YA UCHAGUZI LEO, SASA NI WAGOMBEA RASMI

Image
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva akizungumza mara baada ya kupokea Fomu zilizorudishwa na Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni baada ya kukamilisha mchakato wa kutafuta wadhamini katika Mikoa 10 ya Tanzania na kutimiza masharti yote ya Uchaguzi, leo Agosti 21, 2015 kwenye Ofisi za Tume hiyo, Jijini Dar es salaam. Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva akimkabidhi, Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, nyaraka mbalimbali zitakazotumika wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu, kwenye Ofisi za Tume hiyo, Jijini Dar es salaam leo Agosti 21, 2015. Kushoto ni Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni.CHANZO OTHMANI MICHUZI Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowas