Posts

Showing posts from March 3, 2015

WATU WANNE MBARONI AKIWEMO M/KITI WA KIJIJI KWA TUHUMA ZA MAUAJI YAKIHUSISHA IMANI ZA KISHIRIKINA MKOANI DODOMA

Image
Watu watatu wameuawa Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma katika matukio mawili tofauti yanayohusisha imani za kishirikina. Akizungumzia matukio Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME – SACP amesema tukio la kwanza limetokea tarehe 01/03/2015 majira ya saa 01:00hrs katika kitongoji cha Golani, kijiji cha  Masinyeti, kata ya Iduo, tarafa ya Mlali Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la SAIDIA S/O CHAKUTWANGA mwenye miaka 80, kabila Mkaguru, Mkulima Mganga wa kienyeji aliuawa na watu waliojichukulia sheria mkononi kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na kutobolewa macho. Kamanda MISIME amesema uchunguzi wa awali unaonyesha chanzo cha mauaji hayo ni imani za kishirikina wakimtuhumu marehemu kuwa anazuia mvua kunyesha katika eneo hilo. Pia Kamanda MISIME amesema katika tukio lingine limetokea tarehe 01/03/2015 majira ya saa 02:00hrs katika kitongoji cha Majengo, kijiji cha Ihanda, Kata

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AWASILI MKOANI RUVUMA KUSHIRIKI MAZISHI YA MAREHEMU KAPTENI KOMBA

Image
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na   akisalimiana na Katibu wa CCM mkoa wa Ruvuma Helena Shumbusho  mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Songea mkoani humo tayari kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya Kada wa CCM na Mbunge wa jimbo la Mbiga Magharibi Marehemu Kapteni John Damiano Komba aliyefariki hivi karibuni katika hospitali ya TMJ jijini Dar es salaam, mwili wa Kapteni John Komba unazikwa leo huko kijijini kwao Lituhi mkoani Ruvuma.     Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na   akisalimiana na viongozi mbalimbali wa chama na serikali mkoani Ruvuma wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Songea.     Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Ndugu Mwigulu Nchemba  na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakisalimiana na wananchi wa Songea  baada ya kuwasili mkoani humo tayari kwa mazishi ya Marehemu Kapteni Komba.    Msanii wa TOT Khadija Omary Kopa akiwasili uwanjani hapo

MAONYESHO YA SIKU YA WANAWAKE YA MKOA WA MOROGORO YAINGIA DOSARI BAADA YA MVUA KUBWA KUNYESHA

Image
  M kurugenzi wa manispaa ya Morogoro, Bi. Theresia  Muhongo akisikiliza maelezo kutoka kwa Haji Sajilo ambaye ni Kiongozi msimamizi wa Mipango wa NGO,s ya MOYODEI wakati alipotembelea kwenye mabanda yaliyoharibwa vibaya na mvua iliyonyesha jana jioni. Haya mabanda yalikuwa ni kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani iliyotakiwa kuanza leo jumanne lakini kutokana na maafa hayo maonyesho hayo yamesogezwa mpaka tarehe 5/03/2014 kwa ajili ya ukarabati wa mabanda hayo.(Picha na Pamoja Blog)  M kurugenzi wa manispaa ya Morogoro, Bi. Theresia  Muhongo akipata maelezo kutoka kwa mama kuhusu mabanda yaliyoezuliwa na mvua iliyokuwa na upepo mkali     Baadhi ya Mabanda yakiwa yameharibika vibaya 

RAy C-KIUNO NDICHO KILICHO NIINGIZA KATIKA MADAWA HARAMU

Image
Kama ulikuwa hujui kwanini Ray C alijikuta kwenye madawa ya kulevya chukua hiii...Mwenyewe amefunguka na kusema kiuno ndio kiliumiza wengi na wenye roho mbaya kumtupia pepo la madawa ya kulevya kumpoteza....Soma hapa alivyofunguka : "Haka kademu kaliumiza wengi na hako kakiuno dah kalikuwa homa ya jiji na ndio maana kakarushiwa pepo la madawa maana kalikuwa kanasumbua sana kimuziki na kimvuto!ndio maana hakuna hata msanii mwinzie aliempa hata pole mwee!tatizo kanyota kake ndo kalimletea majanga maana kanyota kake kalin"gara sana ndio maana kakapewa mtihani mgumu ili kaadhirike na pengine kapotee kabisa lakini kana bahati mungu nae alikapenda sana na ndio sababu kamepewa nafasi nyingine ya kuishi na kutimiza mallengo yake!tatizo wabaya wake wana hasira ile mbaya kwanini kamerudi tena?kwanini kabishi kufa kama paka?kwanini kamerudi tena kwenye muzikj?kwanini hakajafa!!!kwanini ziko nyiiiiiiiingi?????kwanini kaliokolewa na mkubwa wa nchi????kwanini Rais alik

MUME ALIVYOMCHOMA KISU HAWARA,NAYE AJICHOMA UTUMBO WAMWAGIKA NJE,DAMU CHAPAPA

Image
Hawara akipelekwa hospitali baada ya kuchomwa kisi. Habari zilizolitikisa Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita ni pamoja na ile ya mkazi wa Chamazi, Hussein Mfaume, kumchoma visu hawara yake, Ester Thomas Ungele (30), naye kujichoma mpaka kujitoa utumbo, Uwazi limeichimba kwa kina. Mume akiwa taabani baada ya kujichoma kisu. Habari zilidai kuwa, kisa hasa cha mwanaume huyo kujichukulia uamuzi huo wa kikatili ni madai ya mwanamke huyo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine anayedaiwa kuwa ni dereva wa teksi. Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo ambaye ni mtoto wa Ester, Sarah siku hiyo, yeye na mama yake walikuwa kwenye eneo lao la biashara ya Mama Lishe, nje ya Ukumbi wa Vijana, Amana uliopo Ilala, Dar. “Ghafla nilimwona Hussein akija huku usoni akionekana mtu mwenye hasira. Alimfuata mama alipokuwa na kumuuliza ni kwa nini anamfanyia dharau MALUMBANO YAANZA, WAKIMBIZANA Sarah anaendelea: “Niliona kama malumbano ya kawaida n

MAMIA YA WATU WAMUAGA KOMBA SONGEA

Image
Mwili wa marehemu kapt.John Komba, wakati ukishushwa kwenye ndege katika uwanja wa ndege wa Songea mkoani Ruvuma tayari kwa kusafirishwa kijijini kwake Lituhi Wilayani Mbinga kwa mazishi. Mwili wa marehemu kapt.John komba, ukiwasili katika uwanja wa michezo wa majimaji mjini Songea tayari kwa ajili ya kuagwa na Wananchi mbalimbali mjini humo. MAMIA ya wananchi wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, jana walijitokeza kuuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga-Magharibi, Kapteni John Komba ambao uliwasili majira ya saa 10.25 katika Uwanja wa Ndege wa Ruhuwiko, mjini hapa. Baada ya mwili huo kuwasili kwa ndege ya kukodi mkoani hapa, ulipokelewa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mark Mwandosya pamoja na baadhi ya wabunge wa Mkoa wa Ruvuma huku baadhi yao wakiangua vilio kiwanjani hapo. Baadaye mwili huo lipelekwa