Posts

Showing posts from August 4, 2016

Taarifa za ndani ya familia… Diamond ‘mchafu’

Image
Diamond Platnumz Imelda Mtema na Musa Mateja Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amejikuta akiwatibua baadhi ya ndugu zake huku wengine wakimuita mchafu kutokana na kitendo cha kumpachika mimba mpenzi wake Zarinah Hassan ‘Zari’ kisha kuwepo madai kuwa ‘amewajaza’ pia mamodo Hamisa Hassan ‘Mobeto’ na Irene Hilary ‘Lynn’. Mmoja wa ndugu wa karibu wa Diamond aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema kuwa, familia imeshtushwa na madai kuwa kijana wao huyo mbali na kwamba Zari a.k.a Mama Tiffah ni mjamzito, amewapa mimba tena Mobeto na Lynn.   Zari. ILIKUWAJE? Miezi kadhaa nyuma, yaliibuka madai kuwa Zari ni mjamzito lakini Diamond amekuwa mgumu kulizungumzia hilo licha ya hivi karibuni mazazi mwenziye huyo kutundika picha akionesha kitumbo chake kilichodhihirisha kuwa ndani yake kuna kiumbe. Lynn LYNN NAYE Huku mashabiki wa Zari ‘Team Zari’ wakionesha furaha ya staa wao ‘kumshika’ mwanamuziki huyo kwa kumbebea ujauzito mwingine, zikaibuka taarifa

Ray C full kicheko

Image
MSANII mkongwe wa Muziki wa Kizazi Kipya aliye katika majaribu makubwa ya matumizi ya madawa ya kulevya, hivi sasa anadaiwa kuwa full kicheko kufuatia mabadiliko makubwa ya afya yake tangu alipoanza kupata matibabu katika kituo cha wahanga wa ‘sembe’, Sober House kilichopo Bagamoyo mkoani Pwani. Kwa mujibu wa bosi wa kituo hicho, Karim Bhanji, Ray C hivi sasa yupo vizuri tofauti na zamani na kwamba kwa jinsi anavyoendelea, hali yake inazidi kutengemaa. “Unajua tatizo kubwa kwa Ray C ilikuwa kwamba alikuwa anapatiwa matibabu bila uangalizi wa kutosha. Ingawa alikuwa akinywa dawa, lakini kilichokuwa kinatokea ni kuwa anakwenda Mwananyamala kunywa dawa halafu anarudi nyumbani, huko mtaani anakutana tena na watu walewale anaendelea kutumia. “Lakini kwa kuja hapa, baada ya dawa anadhibitiwa, hatoki hivyo hapati nafasi ya kujaribu tena kutumia unga, nina imani hali yake itaimarika kadiri muda unavyoenda,” alisema Bhanji na kuongeza kuwa akiwa kituoni, Ray C amesh

Tundu Lissu Akamatwa na Polisi… Msigwa Ahutubia Iringa

Image
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amekamatwa na polisi muda mfupi baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa Ikungi, Singida. Wakati Lissu akiwa mikononi mwa polisi, Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa jana alifanya mkutano wa hadhara na kusema hakuna wa kumpangia cha kuzungumza kwenye mikutano yake. Kukamatwa kwa Lissu  Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema ndiye aliyetoa taarifa za kukamatwa kwake kwenye mtandao akisema: “Wakubwa sana salaam. Ninawaandikieni maneno haya nikiwa chini ya ulinzi wa polisi Singida. ” Nimemaliza kuhutubia mkutano wa hadhara mji mdogo wa Ikungi ambao ni makao makuu ya Jimbo langu la Singida Mashariki. Mara baada ya kushuka jukwaani nimefuatwa Regional Crimes Officer (RCO) wa Mkoa wa Singida aliyejitambulisha kwa jina la Babu Mollel na kunitaarifu kuwa ameelekezwa na Regional Police Commander (RPC) Singida nikamatwe apparently (dhahiri) kuna amri ya kunikamata iliyotoka Dar es Salaam.

Wabunge 3 kesi ya rushwa mil.30/- waachiwa

Image
Kangi Lugola, Mbunge wa Mwibala. MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imewaachia huru wabunge watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka ya kuomba rushwa ya Sh milioni 30. Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage aliwaachia huru washitakiwa hao baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kuwasilisha hati ya kuwafutia mashitaka. Pichani kutoka kushoto ni Mbunge wa Mwibara, Mhe. Kangi Lugola, Mbunge wa Mvomero Mhe.Sadiq Murad pamoja na Mbunge wa jimbo la Lupa, Mhe.Victor Mwambalaswa. Wabunge hao na majimbo yao katika mabano ni Kangi Lugola wa Mwibara mkoani Mara maarufu kama ‘Nyoka wa Shaba,’ Suleiman Saddiq ‘Murad’ (Mvomero – Morogoro) na Victor Mwambalaswa (Lupa – Songwe). Awali Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi akisaidiwa na Wakili Emmanuel Jacob kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), waliieleza mahakama kuwa kesi hiyo imetajwa kwa ajili ya washitakiwa kusomewa maelezo ya awali. Kishenyi alidai

MCHUNGAJI AFARIKI BAADA YA KUFUNGA SIKU 30 AKITAKA KUVUNJA REKODI YA YESU

Image
AFRIKA KUSINI: Mchungaji mmoja amefariki baada ya kufunga usiku na mchana siku 30 akitaka kuvunja rekodi ya Yesu aliyefunga kwa siku 40. Mchungaji huyo aliondoka nyumbani kwake na kuelekea nyikani kwa ajili ya kufunga na kuomba, huku akiweka nia kwa Mungu ya kujitenga na anasa za ulimwengu.

Breaking News: Evans Aveva akamatwa na Takukuru, pesa za Okwi zatajwa

Image
Rais wa Klaabu ya Simba, Evans Aveva anashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru). Taarifa zinaelezwa kuwa Takukuru wanamshikilia Aveva kwa tuhuma za rushwa ingawa haijaelezwa ni tuhuma zipi. Habari za uhakika zinaeleza, Aveva amekamatwa jana na amelala katika moja ya vituo vya polisi jijini Dar es Salaam. Saa chache baada ya Evans Aveva kushikiliwa na Takukuru, kumeibuka sababu kadhaa ambazo zinazungumzwa kuwa ni chanzo. Kumekuwa na taarifa ambazo si rasmi kuwa Aveva aliingiza fedha za Okwi zaidi ya Sh milioni 450 kwenye akaunti yake binafsi kuhofia zichukuliwe na TRA kwa kuwa Simba inadaiwa. Simba inadaiwa zaidi ya Sh milioni 650, hali hiyo imesababisha kuonekana kama vile alikuwa akikwepa kodi. Malipo ya fedha hizo, zaidi ya Sh milioni 450 ni malipo ya ununuzi wa mshambuliaji Emmanuel Okwi ambazo Simba ilimuuza katika klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia. Taarifa hizo zimeeleza kwamba waliamua kuzificha ili waweze kujenga uw

MANJANO FOUNDATION WAKUTANA NA WANAWAKE WA KUJADILI CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI

Image
Meneja Rasilimali watu Kutoka Benki ya NMB Dada   Edith Mwiyomela   akitoa Mada kwa Wanawake Wa Mkoa wa Dar es Salaam  walionufaika na Mradi Kutoka Taasisi ya Manjano waliokutana kujadili na Kuangalia namna ya Kutatua changamoto wanazokutana nazo kwenye Biashara yao ya Upambaji na Uuzaji wa Vipodozi, Ambapo wameaswa Kuwafanya Kazi kwa Bidii,kuwa na Nidhamu na Pia kuweka akiba Pamoja na Kuwa na uvumilivu kwenye kazi zao za kila siku ili kuweza  Kufikia Malengo waliyojiwekea.    Washiriki wakisikiliza kwa makini mada mbalimbali kwenye mkutano huo Afisa Mtendaji Mkuu wa wa Shear Illusions na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Manjano Foundation Mama Shekha Nasser (kushoto) Akimsiliza Mmoja wa Wanawake aliyekuwa akieleza namna anavyopambana na Changamoto zinzowakabili Wanawake wengi kwenye  Biashara zao.Kwa Upande Mwingine Mama Shekha Nasser Amawataka Wanawake   waliohudhuria namna gani ya kuweza kutofautisha faida na mtaji. Biashara nyingi za kina mama hufa baada