Posts

Showing posts from April 14, 2016

Msalaba wa ajabu wamshangaza mama Kanumba

Image
Mama wa staa wa sinema za Bongo, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa akiwa makabulini. DAR ES SALAAM:   Jambo limezua jambo! Baada ya hivi karibuni barua yenye ujumbe mzito kukutwa kaburini kwa aliyekuwa staa wa sinema za Bongo, marehemu Steven Kanumba, limezuka  jipya ambapo kitu kilichopo kaburini kinachodaiwa ni msalaba (kilichozungushiwa duara pichani) kimemshangaza mama wa Kanumba, Flora Mtegoa. Kitu hicho cha chuma chenye umbo la pembe tatu katikati kikiwa na alama ya msalaba, kwa juu kuna picha ya Kanumba, chini kuna maandishi ya DJ na katikati maandishi ya RIP SCK kilizua gumzo hivi karibuni kwenye kumbukumbu ya marehemu kutimiza miaka 4 ambapo baadhi ya watu waliohudhuria Makaburi ya Kinondoni alikozikwa walipigwa butwaa. Baadhi yao walisema chuma hicho kilitengenezwa kwa mfano wa alama mojawapo ya imani ya Freemason ambayo baada ya kifo chake, kuna watu walihusisha kifo hicho na imani hiyo. Muonekano wa msalaba huo ukiwa juu ya kabuli la marehemu Kanumba.

BREAKINGNEWS Breaking: Mahakama Dar imewaachia huru aliyekuwa Mkurugenzi wa Tanesco William Mhando na mkewe

Image
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, William Mhando (kushoto) akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Jana , ambapo alisomewa shitaka la matumizi mabaya ya madaraka. (Picha na Maktaba)   Kesi iliyokuwa ikiwakabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),   William Mhando , mke wake   Eva Mhando,   wameishinda leo katika  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam ambapo walikuwa wakituhumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka, kughushi na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu. Mhando alikuwa anatuhumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka kwa kuipa zabuni Kampuni ya Santa Clara Supplies Ltd huku akijua ana maslahi nayo na kwamba anaimiliki yeye, mke na watoto wake.  April 14 2016   Mahakama ya Hakimu mkazi kisutu Dar es salaam imewaachia huru baada ya kuona hawana hatia kwa kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kuthbitisha juu ya matumizi mabaya ya ofisi na ughushaji wa nyaraka ambao inadaiwa na maafisa wa ser

BREAKIN NEWZZZ!!!:- MFANYABIASHARA MAARUFU NCHINI MWENYE UTATA WA MKATABA NA POLISI ADAIWA KUKIMBIA LIVE!!

Image
Lugumi atoroka nchi *Adaiwa kupanda ndege usiku wa manane, haijulinani alikokwenda *Ni yule anayetajwa kwenye mkataba tata uliohusisha vigogo wa Serikali, Jeshi la Polisi MFANYABIASHARA anayemiliki Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd, Said Lugumi, ametoroka nchi, MTANZANIA limebaini. Lugumi ambaye anatajwa kuwa na ukwasi wa kupindukia katika kipindi kifupi, aliingia mkataba tata na Jeshi la Polisi mwaka 2011, kwa ajili ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchi nzima kwa gharama ya Sh bilioni 37. Taarifa za kutoroka nchi kwa mfanyabiashara huyo, zilielezwa na baadhi ya maofisa wa vyombo vya dola, ambapo inadaiwa kuwa aliondoka nchini Jumatatu wiki hii, siku ambayo Jeshi la Polisi lilitakiwa kuwasilisha mkataba huo Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa mujibu wa sheria. Chanzo kimoja kiliiambia MTANZANIA kuwa mfanyabiashara huyo ambaye amekuwa akitembea na msafara mkubwa wa magari ya kifahari, huku akilindwa na walinzi maalumu wa kuko

WEMA SEPETU AMWAGA IDRIS SULTANI KISA MILIONI 98,MENGI MAZITO YAFICHUKA

Image
  Wema akiwa na Idris. Waandishi wetu, Habari ya mtoto mzuri Wema Sepetu ‘Madam’ kumwagana na mpenzi wake, Idris Sultan si ngeni masikioni mwa wapenda ubuyu, imetapakaa kwenye mitandao ya kijamii lakini Amani limenasa sababu kubwa inayodaiwa kusababisha penzi hilo kuvunjika, twende pamoja. Mwishoni mwa wiki iliyopita, wawili hao waliripotiwa kumwagana rasmi ambapo haikubainika mara moja sababu. TUJIUNGE NA CHANZO Iliposambaa habari hiyo, mapaparazi wetu waliingia kazini kuchimba zaidi ubuyu huo ambapo walifanikiwa kuzungumza na mmoja wa marafiki wa Wema ambaye alieleza siri ya wawili hao kumwagana. “Kilichomfanya Wema amwagane na Idris si kingine ni shilingi milioni 98. Unajua Madam anadaiwa fedha hizo ili alikomboe lile gari lake (Range Rover Evoque) linaloshikiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Sasa akamuomba Idris amlipie, jamaa akazingua. Hapo ndipo penye sababu kubwa iliyomfanya Wema amaindi hadi wakamwagana na Idris,” alisema shosti huyo wa Wema. Idris Sult

MWIGULU,SENDEKA WASHIRIKI MAZISHI YA CHRISTINA LISSU MKOANI SINGIDA

Image
 Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh.Mwigulu Nchemba akitoa heshima zake za mwisho mapema leo kabla ya mazishi, kwa aliyekuwa Mbunge wa CHADEMA (Viti maalum),Marehemu Christina Lisu,Wilayani Ikungi mkoani Singida.  Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida,Bi Martha Mlata akitoaa heshima zake za mwisho mapema leo kabla ya mazishi, kwa aliyekuwa Mbunge wa CHADEMA (Viti maalum),Marehemu Christina Lissu,Wilayani Ikungi mkoani Singida.  Msemaji wa chama cha CCM,Ole Sendeka, Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh.Mwigulu Nchemba wakimpa pole Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA),Mh Tundu Lissu,ambao waliwasili wilayani Ikungi mkoani Singida kushiriki Mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa CHADEMA (Viti maalum),Marehemu Christina Lissu.  Msemaji wa chama cha CCM,Ole Sendeka akimpa pole Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA),Mh Tundu Lissu kwa kufiwa na dada yake  Msemaji wa chama cha CCM,Ole Sendeka akitoa neno la pole kwa Wafiwa,ndugu,jamaa na marafiki kabla ya kufanya maziko, kwa aliye

KUBENEA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA NJE CHA MIEZI MITATU

Image
Hatimaye  hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Jamhuri dhidi ya Saed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo  akidaiwa kumtolea lugha ya matusi Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kindononi imefika tamati. Thomas Simba, Hakimu Mkazi Mkuu katika Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam amesema, mahakama hiyo imemtia hatiani Kubenea na kumpa adhabu ya kutofanya kosa linalofanana na hilo ndani ya miezi mitatu. “Mahakama imejiridhisha kuwa, hilo ni kosa lako la kwanza na kwa kuzingatia nia uliyoenda nayo ya kutatua mgogoro wa wafanyakazi, lakini pia imejiridhisha kwa kutumia ushahidi wa upande wa mashtaka, hivyo inakutaka usifanye kosa linalofanana na  hilo na kuletwa tena mahakamani” amesema hakimu.   Amesema kuwa, kila upande upo huru kukata rufaa endapo wataona kuwa hukumu iliyotolewa hawaridhiki nayo, ambapo pale pale jopo la mawakili wa Kubenea likiongozwa na Peter Kibatala, waliiambia mahakama kuwa wanaweka nia ya kukata rufaa kwa sababu ushahidi uliotumika kuhukumu umeacha mas

BAYERN YASONGA NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA KWA SARE DHIDI YA BENFICA

Image
  Bayern Munich imeambulia sare ya mabao 2-2 dhidi ya Benfica na kufanikiwa kusonga hadi nusu fainali kwa jumla ya mabao 3-2. Katika mechi ya kwanza ikiwa nyumbani, Bayern ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 ambalo limewabeba kufuzu leo kwa kuwa mechi ilikuwa ngumu kwao huku Wareno hao wakiwa vizuri zaidi.
Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati ya Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa nchi ya Jamhuri ya Czech hapa nchini    Pavel Rezac, tukio hilo lilifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Ikulu jijini Dar es Salaam Balozi Mteule wa nchi ya    Jamhuri ya Czech hapa nchini    Pavel Rezac.     Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Balozi Mteule wa nchi ya Jamhuri ya Czech hapa nchini    Pavel Rezac mara baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi mteule kutoka nchi ya    Jamhuri ya Sudani Kusini Mariano Deng Ngor aliyefika Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha hati yake za utambulisho.   .    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Balozi Mteule wa n