Posts

Showing posts from August 2, 2018

Spika Wa Bunge Apokea Barua Ya Kujiuzulu Kwa Mbunge Wa Monduli

Image
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai amepokea barua ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiuzulu Ubunge wa Jimbo la Monduli kutoka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Julius Kalanga.

Shamsa: Akinipenda Chidi Inatosha!

Image
Shamsa Ford STAA mwenye mvuto Bongo Muvi, Shamsa Ford amesema kuwa hata kama leo watu watamchukia kwa jinsi alivyo au kwa kuzungumza ukweli hawezi kuumia hata siku moja kwa sababu anaamini aliyempenda kwa dhati ambaye ni mumewe Chidi Mapenzi yupo, inatosha. Staa huyo alizungumza na gazeti hili la Amani baada ya watu wengi kumshambulia kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kutokelezea na nguo fupi kwenye 40 ya mtoto wa Zamaradi, na kusema kuwa ni ngumu kumridhisha kila mtu kwenye maamuzi yako. “Mimi Mungu kanijalia maneno sijali kabisa na isitoshe Chidi akinipenda na akakubaliana na maamuzi yangu kwangu inatosha kabisa siwezi kumridhisha kila mtu,” alisema Shamsa.

MKUU WA WILAYA YA ARUMERU, JERRY MURO AFANYA ZIARA ARUSHA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Jerry Muro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Meru na Arusha.  MKUU wa Wilaya ya Arumeru, Mheshimiwa Jerry Muro jana tarehe 01 Agosti, 2018 alifanya ziara ya kikazi pamoja utambulisho kwa watumishi wa Halmashauri Mbili za Meru yenye kata 26 na Arusha  yenye kata 27 zilizo katika Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha. Akiwa katika halmashauri hizo, Mhe. Muro aliwataka watumishi kufanya kazi kwa kuzingatia mahitaji ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo ndio anasimamia Utekelezaji wake katika halmashauri zote mbili zenye kata 53.  Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Jerry Muro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Meru na Arusha.  Katika Ziara Hiyo, Mhe Muro aliambatana na Mkuu wa wilaya ya Monduli, Mhe Iddi Hassan Kimanta aliyekuwa akikaimu Wilaya ya Arumeru, pamoja na Katibu Tawala, Bwana Timotheo Mzava pamoja na baadhi ya viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya

Picha ya Gadner na Mwanae Yazua Gumzo Mitandaoni

Image
 Kuna picha  aliweka Gadner akiwa amerepost kutoka katika akaunti ya binti yake Karen ikiwa inaonyesha akiwa amemkumbatia mtoto wake  huku wakiwa wamelala kwenye kochi, na kwa jinsi wao walivyochukulia ilikuwa ni kama mapenzi ya baba na mtoto. Lakini baada ya picha hiyo kwenda katika mitandao ya kijamii ilileta gumzo na kusemewa maneno mengi sana huku wadau na baadhi ya mashabiki wakisema kuwa hayo sio maadili ya kitanzania hasa kwa baba na binti yake. Huku wengine wakimtuhumu sana gadner na kusema kuwa hawamuamini sana kutokana na ukweli kwamba amekuwa akitoka kimapezni na wasichana wenye umri kama wa binti yake , hivyo hiyo inaleta picha mbaya kwa mashabiki wanaomuona akiwa anafanya hivyo. ==>>Tazama baadhi ya maoni hapo chini

Mke wa Babu Tale: Nina wivu kwa mume wangu akitoka bila mimi lakini

Image
Wiki weekend iliyopita kwa mara ya kwanza meneja wa Diamond Babu Tale alitoka na mama watoto wake na kwenda kwenye arobaini ya mtoto wa Zamaradi iliyofanyika huko Bunju B. Bongo5 ilifanya mahojiano na mke wa Babu Tale na kumuuliza anajisikiaje pale anapomuona mume wake akipiga picha na warembo mbalimbali wakati akiwa kwenye shughuli zake za kikazi. “Wivu upo lakini unategemea upo kwa kiwango gani na wivu ukiuendekeza mtakwama,” alisema mama watoto huyo wa Tale. Kwa upande wa Babu Tale alidai kwa kuwa yupo kwenye tasnia ya burudani kwa muda mrefu amejifunza hawezi tembea na mke wake kila sehemu. “Leo sijaja kazini nimekuja kwenye shughuli ndio maana unaona niko na mke wangu,” alisema Babu Tale.

AUNT ACHOMOA NDOA NA IYOBO

Image
Aunt Ezekiel MUIGIZAJI wa kitambo kwenye tasnia ya filamu, Aunt Ezekiel, ambaye pia ni mzazi mwenzie na dansa maarufu wa Wasafi Classic Baby (WCB), Moses Iyobo, amesema kuwa hana mpango wa kufunga ndoa na dansa huyo japokuwa wameshakaa wote zaidi ya miaka mitatu kwani kikubwa wanachokiangalia ni kulea mtoto wao Cookie. Aunt Ezekiel akiwa na mzazi mwenzie na dansa maarufu wa Wasafi Classic Baby (WCB), Moses Iyobo Akizungumza na Amani, Aunt alisema kuwa siyo kwamba mtu akifunga ndoa ndiyo anaweza kuishi vizuri na mwanaume wake, bali ni kwamba anachojua kuishi vizuri ni sifa moja kubwa ya kuendelea kuwa pamoja ni kupeana heshima na kila mmoja kutambua anachokifanya. “Mimi sitaki hata kukuficha wala sijawahi kufikiria kufunga ndoa na Iyobo leo wala kesho kikubwa tunaishi vizuri na tunalea mtoto wetu ipasavyo hilo ndilo ninalolitaka na si vinginevyo kwani kuolewa siyo ishu kikubwa malezi ya mtoto tu,” alisema Aunt. STORI NA IMELDA MTEMA | GPL