Posts

Showing posts from August 22, 2013

POLISI FEKI 7 WANASWA TENA....

Image
SIKU chache baada ya kukamatwa kwa askari feki wa usalama barabarani, Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imewakamata watuhumiwa saba wa ujambazi, wakiwa na sare za Polisi, huku mwingine akijifanya ofisa Usalama wa Taifa.   Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaa, Suleiman Kova alisema watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na sare za Polisi jozi mbili. Watuhumiwa hao ni Khamis Mkalikwa (40), Magila Werema (31), Nurdin Bakari (46), Materu Marko (32), Louis Magoda (34), Amos Enock (23) na Amiri Mohammed (45), wote wakazi wa jijini Dar es Salaam.   Sare hizo, kwa mujibu wa Kamanda Kova, ni zenye cheo cha Sajenti wa Kituo, huku jozi moja ikiwa na jina linalosomeka SSGT A.M Mduvike.   Watuhumiwa hao walikamatwa jana katika eneo la Kiluvya, baada ya askari kuweka mtego, ambao ulifanikiwa kuwanasa.  Alisema watu hao walikuwa wakitumia silaha, sare za jeshi la Polisi na redio ya mawasiliano katika u

RWANDA NA UGANDA WAJITOA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Image
Chama cha Wasafirishaji wa Mafuta Tanzania (Tatoa), kimesema Rwanda na Uganda zitajitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaam kuanzia Septemba Mosi, mwaka huu. Katibu Mtendaji wa Tatoa, Zacharia Hanspope aliwaambia waandishi wa habari jana baada ya kukutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuwa nchi hizo zinajitoa kutokana na matatizo mbalimbali ambayo kwa muda mrefu zimekuwa zikiyalalamikia lakini Serikali haikuchukua hatua. Hanspope alisema ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ni baadhi ya vikwazo ambavyo vimekuwa vikilalamikiwa kwa muda mrefu na wafanyabiashara mbalimbali wa nchi hizo. “Serikali ipunguze gharama za ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ili kuwa na ushindani sawa na bandari nyingine na hivyo kuzivutia kutumia Bandari ya Dar es Salaam,” alisema Hanspope. Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omary Chambo alikataa kuzungumzia lolote kuhusu suala hilo akisema halina mantiki yoyote kwake.... “Hivi hilo jambo unaloniuliza lina sense (mant

MFANYABIASHARA ALIYEJIREKODI AKIMLAWITI MFANYAKAZI WA DUKANI AKAMATWA

Image
JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro limemkamata mfanyabiashara mashuhuri wa mjini Moshi, Totolii Kimath anayedaiwa kurekodi mkanda wa video ukimwonyesha akimlawiti mfanyakazi wake wa dukani.   Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, aliliambia Tanzania Daima kuwa kijana huyo ambaye anamiliki maduka ya kuuza na kutengeneza CD katika kituo kikuu cha mabasi cha mjini Moshi, alikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), akitokea Dubai.   Alisema Jeshi la Polisi lilikuwa likifanya uchunguzi kwa muda mrefu wa picha zilizosambaa katika mitandao ya kijamii na simu ambazo zinaonyesha mwanaume na mwanamke wakifanya mapenzi kinyume cha maumbile.   “Tulikuwa tunafanya uchunguzi wa picha zilizosambaa kwenye mitandao pamoja na simu kwenye Whatsapp ambazo zinaonyesha watu wakifanya mapenzi kinyume cha maumbile, kimsingi ni kosa la jinai mwanamke kumruhusu mwanaume amuingilie kinyume cha maumbile ama mwanaume amuingilie