Posts

Showing posts from February 17, 2017

Uwoya ni Gusa Unate!

Image
DAR ES SALAAM: Msanii maarufu wa filamu Bongo, Irene Uwoya (pichani)  anatajwa kuwa kati ya mastaa wa kike Bongo aliyewahi kutoka na mastaa na vigogo mbalimbali huku ikidaiwa kuwa, kila aliyekuwa naye alimuacha yeye na si kuachwa. Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Uwoya aliyeomba hifadhi ya jila lake, staa huyo mwenye shepu na mvuto wa kudatisha kimahaba amekuwa akipapatikiwa sana na wan aume lakini mwisho wa siku huishia kuwaliza kwani yeye ndiye anayeamua kuendelea na wewe au akuache. “Uwoya namjua vizuri sana, yule ni hatari kwa wanaume. Kwanza anajijua kuwa ni mzuri hivyo amekuwa akiwadenguliwa wanaume wengi sana na orodha ya wanaomtokea kila siku ni kubwa. “Lakini akitokea kukupenda atakupenda kweli hadi unaweza kuona kero. Kwa kifupi anajua kupenda, kujali na kubembeleza kiasi kwamba ukinasa kwake ni vigumu kutoka ndiyo maana wapo wanaosema kwamba, Uwoya ni gusa unate! “Ila sasa, anaweza kukuchanganya kwa mahaba mazito lakini siku akiamua kukuacha, anaku

BREAKING NEWZZ:MMILIKI WA HANDAKI LA CD ZA UJANJA UJANJA ATIWA MBARONI NA POLISI

Image
Mmiliki wa hoteli ya Butterfly iliyopo maeneo ya Kariakoo, Phili Ulaya Mdolo maarufu kwa jina la Dotto ametiwa mbaroni kutokana na tuhuma za kumiliki duka kubwa la CD lililopo mafichoni ndani ya hoteli yake hiyo bila kufuata utaratibu wa serikali. Dotto amekamatwa Ijumaa hii katika operesheni iliyoongozwa na Waziri Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye ya kukagua maduka yanayouza CD kinyume na sheria pamoja na maeneo yanayozalisha CD feki. Waziri Nape amesema kuwa huyo ni mmoja kati ya wafanyabiashara wakubwa jijini Dar es Salaam ambao wanafanya biashara hiyo bila kufuata taratibu za serikali huku akiliamuru jeshi la polisi kumshikilia mtuhumiwa huyo kwa ajili ya kutoa maelezo zaidi huku akiahidi kukutana naye siku ya Jumatatu. Tazama picha zaidi hapa chini za tukio hilo. Waziri Nape akiongoza kukagua baadhi ya vyumba vilivyopo chini ya ardhi katika hoteli ya Butterfly Kufuli ikivunjwa katika sehemu zilizohifadhiwa CD haramu katika hotel

PICHA: WAZIRI NAPE AFANYA ZIARA YA KUSHITUKIZA KARIAKOO, AKAMATA KAZI FEKI ZA WASANII

Image
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye leo ameongoza timu yake katika operesheni maalumu ya kufanya msako mkali wa wauzaji wa kazi za wasanii bila vibali vya Bodi ya filamu ya Tanzania.  Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiangalia bidhaa za filamu na muziki zilizofeki leo hii. Waziri huyo amevamia maduka yanayouza CD FEKI pamoja na ofisi ambayo inajihusisha na kurudufu kazi za wasanii kutoka ndani na nje ya nchini. Hii ni ziara ya Pili kuifanya Kariakoo. Ziara ya kwanza ya kushitukiza aliifanya July 15, 2016 ambapo aliwataka wauzaji wa CD kote nchini kufuata sheria ya kuuza CD zenye stika huku akisema mtu yoyote ambaye atakutwa na CD ambayo haina stika mnunuaji na muuzaji wote watakamatwa. Operesheni hizi zinafanywa kwa lengo la kutokomeza uharamia wa bidhaa za filamu na muziki kwa kuokoa pato la TAIFA Amesema Seikali itawachukulia hatua za kisheria ikiweemo kuwafutia leseni wauzaji na wasambazaji wa fila

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Amadou Hott aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Amadou Hott Ikulu jijini Dar es Salaam.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Amadou Hott mara baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) nchini Jean Pierre Tshampanga  Mutamba Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi huyo wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) nchini Jean Pierre Tshampa

KAMANDA MPINGA AONGELEA WITO WA DIAMOND PLATNUMZ KITUO CHA POLISI

Image
Moja kati ya vitu ambavyo vilimake headlines kinoma noma siku ya jana ni pamoja na hii ya picha iliyosambaa ikimuonyesha msanii wa Bongo Fleva  Diamond Platnumz  akiwa kituo cha Polisi akifanyiwa mahojiano. Kitu ambacho kilizua maswali mengi sana kwa watu na wengine kuhisi kwamba huenda ni lile sakata la madawa ya kulevya linaloendelea kutikisa jiji la Dar es Salaam. Perfect255  ikaona isiwe kesi, ikapiga story na mkuu wa kikosi cha usalama barabarani  Kamanda Mpinga  ili atusanue kuhusu mkanda mzima uliokuwa ukiendelea hapo jana kituo cha Polisi. “Ni kweli nilikuwa nimemwita Diamond aripoti hapa kwangu toka Jumanne, baada ya kuiona ile clip ambayo ilikuwa imesambaa kwenye mitandao ya kijamii, ambayo ilifanana na yule kijana ambaye alikuwa akiimba wimbo wa Darassa, tukaona kuna haja ya sisi kuchukua hatua kwasababu tuliona jinsi alivyokuwa akiendesha alikuwa anavunja sheria za usalama barabarani.”

MBUNGE RIDHIWAN KIKWETE AFUNGUKA KUHUSU UTAJILI WAKE

Image
Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete amefunguka kuhusu madai ya baadhi ya watu kuwa ana utajiri wa kutisha na kwamba anamiliki mali nyingi, jambo ambalo limekuwa likifanya watu hao watilie shaka njia aliyotumia kupata utajiri huo. Kikwete akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast ndani ya EA radio, amesema kuwa anashangazwa na dhana hiyo potofu inayojengwa na watu bila kujua ukweli wa mambo, ambapo ameweka wazi kuwa yeye ni kijana mpiganaji na mwenye kupenda mafanikio, lakini hana umiliki wa mali nyingi kama ambavyo imekuwa ikisemwa. Ridhiwan ambaye ni mtotot wa Rais wa awamu ya nne wa Tanzania, Jakaya Kikwete, amesema mali zake ni za kawaida na amezipata kwa njia halali, huku akisimulia jinsi alivyowahi kuwakuta watu wakimjadili yeye kuhusu mali zake, bila watu hao kujua kuwa yeye ndiye Ridhiwan Kikwete.

MAJALIWA ATETA NA MBUNGE WA SIMANJIRO

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia kwaya ya Wamasai wa Simanjiro wakati alipowasili kwenye uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjairo mjini Orkesimet Februari 16, 2017. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joel Bendera.  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhiwa zana za asili za kabila la wamasai wakati aliposimikwa kuwa Mzee wa Simanjiro na kupewa jina la Ole Majaliwa katika mkutano wa hadhara aliouhutubia kwenye uwanja wa Halmashauri ya wilaya ya Simanjiro mji Orkesimet Februari 16, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro mjini Orkesimet Februari 16, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)