Posts

Showing posts from February 19, 2015

Balaa la Mchepuko: Mume wa mtu Aumbuka......Baada ya fumanizi Apewa kichapo kizito na kutembezwa Uchi

Image
Mwanaume aliyetambulika kwa jina moja la Joseph amejikuta akiaibika vikali kufuatia kudaiwa kunaswa akiwa na mwanamke mwingine ilhali yeye ni mume wa mwanamke aitwaye Sophia. Kwa mujibu wa mashuhuda, aibu hiyo ilimkuta Joseph, Februari 14, mwaka huu (Siku ya Wapendanao Duniani) kwenye Kitongoji cha Nyihongo wilayani Kahama, Shinyanga wakati wadau mbalimbali walikuwa kila mtu na wake.   Mashuhuda waliliambia Amani kwamba, Joseph ni fundi ujenzi na siku ya tukio alinaswa kwenye nyumba inayojengwa na yeye lakini ikiwa bado kumalizika.   “Jamaa mwenye mke alishajua kuwa Jose anamlia mali zake lakini akavumilia sana. Hakutaka kumuuliza Jose wala mke wake, yeye alitaka amfumanie laivu mwenyewe,” alisema shuhuda. “Sasa siku ya tukio, Jose alionwa na mtu mmoja akiingia kwenye nyumba inayojengwa. Yule mtu alishajua Jose anachepuka na yule mke wa jamaa, akaenda kumwambia ndiyo wakamzukia na kumnasa,” kilisema chanzo.   Chanzo kikaendelea kuweka w