Posts

Showing posts from August 18, 2015

BREAKING NEWS: PROF. KITILO AKATAA KUGOMBEA URAISI ACT, BARUA YAKE HII HAPA

Image
Ndugu Wazalendo, Naomba niwashukuru nyote kwa imani kubwa mliyo nayo juu yangu katika kukiwakilisha chama katika nafasi ya Rais. Naishukuru pia Kamati Kuu kwa imani yake kwangu hata kufikia hatua ya kupitisha azimio la kuniomba nigombee urais kwa chama chetu. Jana Kamati Kuu ilituma ujumbe maalumu nyumbani kwangu kwa ajili ya kuzungumza na familia na jamaa zangu juu ya ombi hili. Aidha, Nimekuwa nikilitafakari jambo hili tangu Alhamisi nilipoombwa rasmi kutafakari uwezekano wa mimi kugombea baada ya juhudi zetu za kutafuta mgombea kushindikana. Nimefanya mawasiliano mapana katika familia, ndani ya chama, chuoni ninapofanyia kazi, Kanisani kwangu,na kwa watu na taasisi mbalimbali ninazohusiana nazo. Baada ya tafakari na mawasiliano  CONSULTATIONS  mapana nasikitika kusema kwamba sina utayari na maandalizi ya maana ya kisaikolojia, kifamilia, na kisiasa kuniwezesha kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi huu. Najua nimewaangusha sana katika uamuzi wangu huu

HIVI NDIVYO MABASI YA MWENDO KASI YALIVYO ZINDULIWA JIJINI DAR

Image
Moja ya mabasi yaendayo mwendo wa haraka yakiwa barabarani katikati ya jijini Dar es Salaam leo. Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadiki akizungumza katika uzinduzi wa semina ya mafunzo ya madereva wa mabasi yaendayo haraka (BRT) leo jijini Dar es salaam, juu ya kuanza kwa kipindi cha mpito cha mradi huo Oktoba mwaka huu, Semina itakayofanyika Agosti 23 mwaka huu jijini Dar es salaam. Waziri Mkuu, tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na mgeni rasmi Hawa Ghasia akizungumza katika uzinduzi wa mafunzo ya madereva wa mradi wa mabasi yaendayo haraka (BRT) waliokaa mbele, kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadiki na kulia ni Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi. Waziri Mkuu, tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na mgeni rasmi Hawa Ghasia aliyeshika mkasi akikata utepe kuzindua mafunzo madereva wa mabasi yaendayo haraka (BRT) jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa mafunzo yayo ya madereva. Baadhi ya viongozi wa jesh

RAIS KIKWETE AMPA MAKAVU LOWASSA

Image
  Wakati wa sherehe ya kumuaga Rais Kikwete iliyoandaliwa na Wizara ya Ujenzi, Rais kikwete alimpa somo Lowasa kwa kueleza kuwa mtu akiwa Waziri hapaswi kujisifia kuwa amelifanya jambo Fulani yeye binafsi katika nchi wakati Waziri hufanya kazi kwa niaba ya Rais. Alitolea mfano huo alipokuwa anamsifia Waziri Pombe Magufuli ambaye pamoja na kazi nzuri ya ujenzi wa Barabara lakini wakati wote amekuwa hajisifii kuwa anafanya yeye binafsi. Uchunguzi unaonesha kuwa Rais alikuwa anampa somo hilo Lowasa ambaye anajitapa kuwa alijenga UDOM wakati wazo hilo ni la JK mwenyewe binafsi wala halikuwa ktk ILANI YA CCM

NAPE ATAKA GARI LA WAGONJWA LIPELEKWE KWA LOWASSA MAPEMA

Image
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesisitiza kuwa kitashinda Uchaguzi Mkuu mwaka huu kwa sababu kina mtandao mkubwa wa wanachama kuanzia ngazi ya chini na kwamba kufurika kwa wananchi katika mikutano ya Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa sio ushindi, kikisema kura ni mahesabu. Aidha, kimesema kuwa mgombea huyo wa Chadema na umoja wa vyama vinne vya upinzani (Ukawa), amedanganywa na wapambe wake kuihama CCM na kumkejeli ikisema gari la wagonjwa linapaswa kuwekwa nyumbani kwake siku ya uchaguzi kwani CCM itapata ushindi wa uhakika asubuhi. Akitoa taarifa kuhusu kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika jana katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisisitiza kuwa ushindi wa chama hicho tawala na kikongwe hauna shaka kutokana na mtandao wake kuanzia ngazi ya chini. Akijibu swali kuhusu kufurika kwa wananchi katika mikutano ya mgombea huyo wa Chadema, Nape alisema:  “Kwa walioanza si

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 18.08.2015

Image