Posts

Showing posts from March 12, 2018

Kesi ya Madawa: Shahidi Afunguka Alichokikuta Chumbani kwa Wema

Image
Msanii wa filamu, Wema Sepetu (katikati) akiwa na mama yake mzazi Miriam Sepetu (kulia)  wakitoka kusikiliza kesi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Mama mzazi wa Wema Sepetu akishuka ngazi za mahakama baada ya kusikiliza kesi inayomkabili mwanaye. Wema Sepetu na mama yake, Miriam Sepetu  wakijadili jambo baada ya kusikiliza kesi nje ya mahakama. MJUMBE wa Shina Namba 39, nyumbani anakoishi msanii wa filamu, Wema Sepetu, Steven Alphonce ambaye ni shahidi katika kesi inayomkabili staa huyo, amedai wakati wa upekuzi walikuta kipande cha sigara wala si bangi. Alphonce amesema hayo leo Jumatatu, Machi 12, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, wakati akitoa ushahidi wake katika kesi ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili Wema na wenzake wawili na kusema alishiriki katika upekuzi nyumbani kwa Wema na kukuta kipande hicho cha sigara jikoni na chumbani kwa

ASLAY HATIMAYE AANIKA UKWELI KUHUSU KUTOKA NA NANDY,AFICHUA YOTE

Image
Msanii wa muziki Bongo, Aslay amefunguka kuhusu ukaribu wake na Nandy kwa sasa. Muimbaji huyo wa ngoma ‘Natamba’ ameiambia FNL ya EATV kuwa kinachowaunganisha ni kazi tu hakuna mahusiano ya kimapenzi kama inavyokuwa ikiripotiwa. Nafikiri mashabiki zangu ambao wananifuatilia wanajua ni mtu ambaye nina mtoto, kuna mwanamke ambaye nimezaa naye. Nandy tupo kwenye kazi tu, tunafanya lakini hamna chochote kinachoendelea kati yangu na Nandy,” amesema. Aslay na Nandy kwa sasa wanafanya vizuri na ngoma ‘Subalkheri’ ikiwa ni ngoma yao ya pili kutoa pamoja baada ya Mahabuba.

MAUWAJI YA KUTISHA TENA ,MTOTO ATEKWA NA KUUAWA KINYAMA

Image
MASKINI MTOTO HUYU! Atekwa na Kuuawa, Mama Mzazi Hoi! Maskini mtoto wa watu! Ndivyo walivyosikika mashuhuda wa tukio la mwanafunzi, Doricka Majeshi, anayesemekana kutekwa kisha kukutwa akiwa ameuawa na watu wasiojulikana ndani ya nyumba inayoendelewa kujengwa na kuibua simanzi nzito. Kwa mujibu wa mashuhuda hao, mtoto Doricka mwenye umri wa miaka nane aliyekuwa anasoma darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Lukobe mjini hapo alidaiwa kukutwa na mkasa huo tangu Jumanne ya wiki iliyopita kisha kusakwa kwa siku tatu bila mafanikio, kabla ya mwili wake kukutwa ukiwa na majeraha Alhamisi iliyopita nyuma ya nyumba hiyo

Naibu Katibu Mkuu wa BAVICHA Ajiuzuru

Image
Naibu Katibu Mkuu Baraza la Vijana Chama cha Demokrasia na Maendeleo – Chadema (BAVICHA), Getrude Ndibalema amesema amejiuzuru nafasi hiyo na kubaki mwanachama wa kawaida ili kutimiza majukumu binafsi.

WAZIRI MWAKYEMBE AFUNGUA MKUTANO WA 14 WA MAAFISA HABARI, MAWASILIANO NA UHUSIANO SERIKALINI

Image
    Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakati wa ufunguzi mkutano wa 14 wa kikao kazi cha Maafisa hao kilichoanza leo Jumatatu tarehe 12-16 Machi, 2018 Jijini Arusha. Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Susan Mlawi akizungumza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakati wa ufunguzi mkutano wa 14 wa kikao kazi cha Maafisa hao kilichaonza leo Jumatatu tarehe 12-16 Machi,2018 Jijini Arusha.  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini kilichaonza leo Jumatatu tarehe 12-16 Machi,2018 Jijini Arusha.  Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gabriel Daqqaro akuzungmza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini wakati wa ufunguzi mkutano wa 14 wa kikao kazi cha Maafisa hao kilich