Posts

Showing posts from May 23, 2015

EXCLUSIVE: JOHARI AJIFUNGUA KWA SIRI

Image
Mshtuko! Baada ya kujulikana kwa wengi kuwa hana mtoto na madai ya kutokuwa na uwezo wa kuzaa, mwigizaji wa kitambo Bongo, Blandina William Chagula ‘Johari’ ameshangaza baada ya siri kuvuja kuwa amejifungua kwa siri ambapo mtoto ana umri wa miezi 7 sasa, jambo lililozua mkanganyiko na mjadala mzito, Risasi Jumamosi linakupa ‘exclusive story’. Mwigizaji wa kitambo Bongo, Blandina William Chagula ‘Johari’ UBUYU WAMWAGWA Mwandishi wetu akiwa katika majukumu yake ya kila siku, ghafla alipigiwa simu na chanzo chake cha kuaminika ambacho ni mtu wa karibu wa Johari na kuanika kila kitu huku kikiomba hifadhi ya jina. Mtoto wa Johari. Sosi: Wewe (kikitaja jina la mwandishi) una habari? Mwandishi: Zimejaa tele lakini hiyo yako inaweza kuwa ya muhimu zaidi. Sosi: Tena ni muhimu kweli, unajua kuwa Johari ana mtoto na sasa anatimiza miezi saba? Mwandishi: Unasema? Kajifungua lini na wapi? Sosi: Kitambo tu, mbona hata kwenye ukurasa wake wa Instagram kaweka hizo picha,

PICHA YA DIAMOND AKILA MISHIKAKI GUMZO

Image
Stori: Musa Mateja PICHA ya staa wa Nasema Nao, Nasibu Abdul ‘Diamond’ inayomuonesha akila mishikika uswahilini imezua gumzo la aina yake mitandaoni. Staa wa Nasema Nao, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akila mishikika uswahilini. Picha hiyo ambayo ilipigwa mwaka mmoja uliopita maeneo ya Tip Top, Manzese jijini Dar, imeibua mjadala mpya juzikati kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengine walimpongeza kwa kitendo hicho wengine wakisema si cha hadhi yake. “Hii ni nzuri kwa mtu kama Diamond akila uswahilini. Anaonesha siyo mtu wa majivuno,” alichangia mdau mtandaoni huku wengine wakidai si sawa kwani anajiabisha. Nasibu Abdul ‘Diamond’. Baada ya chanzo hicho kuipata picha hiyo na kumtumia mwandishi wetu, Mikito Nusunusu ilimtafuta Diamond ili aweze kuizingumzia lakini simu yake haikupatikana lakini Bab Tale alipatikana na kukiri maelezo ya chanzo chetu. “Hakukuwa na ishu zaidi ya kuitamani mishikaki, tukaona tununue, mbona ni ya toka mwaka jana?,” alisema Bab Tale.

FASHION ZAMARADI MKETEMA AFUNIKA KWENYE TUZO ZA WATU 2015

Image
Shukran sana kwa WOTE mlioweza kusupport mpaka siku hii ya leo filamu ya KIGODORO ikaweza kuibuka kama FILAMU BORA kwa mwaka 2014 kupitia TUZO ZA WATU... ni ngumu kutaja mmoja mmoja ila kuna mtu nikimsahau nitakuwa mchoyo wa fadhila... my beautiful FAN marykimodo juhudi zako zimezaa matunda.. nakupenda sana...na WOOOTE walioweza kuchukua muda wao kunipigia kura.. NATHAMINI SANA SANA!! Huu ni ushindi wetu SOTE!!! Na zaidi imenipa changamoto ya kutengeneza kazi nzuri zaidi!! ASANTENI SANA SANA!!

BAADA YA KUPATA UMAARUFU KWA KUFANANA NA WEMA MWANADADA TUERNY SASA AAMUA KUJIMWAGA HUKO INSTAGRAM

Image

ALIKIBA, WEMA, JIDE WAFUNIKA TUZO ZA WATU...DIAMOND CHALI! TAZAMA LIST NZIMA YA WASHINDI HAPA

Image
! Hii ni orodha kamili ya washindi Mtangazaji wa redio anayependwa D’Jaro Arungu – TBC FM Kipindi cha redio kinachopendwa Papaso – TBC FM Mtangazaji wa runinga anayependwa Salim Kikeke – BBC Swahili Kipindi cha runinga kinachopendwa Mkasi – EATV Blog/Website inayopendwa Millardayo.com Muongozaji wa video anayependwa Hanscana Muongozaji wa filamu anayependwa Vincent ‘Ray’ Kigosi Muigizaji wa kike wa filamu anayependwa Wema Sepetu Muigizaji wa kiume wa filamu anayependwa Hemedy PHD Mwanamuziki wa kike anayependwa Lady Jaydee Mwanamuziki wa kiume anayependwa Alikiba Filamu inayopendwa Kigodoro Video ya muziki inayopendwa Nani kama Mama – Christian Bella f/ Ommy Dimpoz Kuna videos 4 za washindi na mastaa wengine walioshiriki tuzo hizo wakiongea baada ya utoaji wa tuzo hizo! KUZICHEKI. BONYEZA HAPA!

Lemutuz: Aliyevuruga Matokeo ya Jana Tuzo za Watu Yupo Busy Pia Kuvuruga Matokeo ya KTMA, Nitamtaja Laivu

Image
lemutuz_nation 'Well, huwa ninaongea na FACTS with   EVIDENCE   toka jana Usiku nimesema I smell fish kama nilivyo smell Fishy kwenye matokeo ya Miss Tanzania ya Mwaka jana kuna wajinga akili ndogo walioanza kunirushia matusi   LE AKILI KUBWAZZZZ   now ninasema jana HAKI HAIKUTENDEKA kuna wanaojaribu kuninyamazisha na matusi...great ninarudia tena sikuenda Shule kuwa mjinga so toka jana niliingia kwenye uchunguzi wa FACTS and   EVIDENCE of WHO IS BEHIND LAST NIGHT MESS   tayari nimeshaanza kupata the TRUTH....tena the   TRUTH   ni aliyevuruga jana yupo busy pia kuvuruga Matokeo ya KMTA....soon nitakuwa na " LE TAMKOZZZ FOUR LIVE"   and I mean it...stay tuned hahahaha U know makelele yangu toka jana yameleta kizungu zungu behind the scene wameshaanza kuvurugana na kunipigia niache hahahaha..now stay tuned   NITAMTAJA ALIYEVURUGA SHOW YA JANA NA FACTS   and EVIDENCE....na   I HOPE NITASAIDIA KUTOVURUGWA KWA KTMA   maana ni huyo huyo gademu mazafantazzz! Na the