Posts

Showing posts from October 7, 2017

CHADEMA JIMBO LA IRINGA MJINI GIZA NENE, MADIWANI WALIOJIUZULU WATIMKIA CCM.

Image
Na Fredy Mgunda,Iringa. Chama cha mapinduzi (CCM) manispaa ya Iringa kimeendelea kujiimalisha kwa kuvuna wanachama watano kutoka chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) manispaa ya Iringa wakiwa na mikakati ya kuja kulikomboa jimbo la Iringa mjini ambalo lipo chini ya chama cha CHADEMA. Akizungumza wakati wa kuwapokea wanachama hao kutoka kata ya kitwiru mwenyekiti wa CCM manispaa ya Iringa Said Rubeya aliwapongeza wanachama kwa kutambua kazi inayofanywa na chama cha mapinduzi chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano DR John Pombe Magufuli. “Mimi nimefurahi sana nyie kurudi nyumbani maana mtakuwa na msaada mkubwa sana katika kukijenga chama hapa manispaa ya Iringa ili tuweze kulikomboa jimbo hili katika uchaguzi ujao nah ii ndio mikakati yetu”alisema Rubeya Rubeya  aliwaambia wanachama hao kuwa sasa wapo katika mikono salama ya kisiasa tofauti na walipokuwa kwenye chama cha awali na kuwasihi wasiwe waoga katika kufanya kazi za kukije

Mbowe ampongeza Rais Magufuli

Image
Babati.  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amepongeza kitendo cha Rais John Magufuli kuitenganisha Wizara ya Nishati na Madini kwa kuwa kwa zaidi ya miaka saba kambi hiyo ilikuwa inaishauri Serikali kufanya hivyo. Mbowe amesema hayo leo Jumamosi kwenye mazishi ya marehemu Philip Gekul, baba mzazi wa Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul yaliyofanyika kata ya Dareda. Amesema kwa mujibu wa kumbukumbu za Bunge zinaonyesha kuwa kambi rasmi ya upinzani ilikuwa inashauri wizara hiyo itenganishwe lakini ushauri wao haukufanyiwa kazi. "Wizara ya Nishati na Madini ni wizara nyeti mno na mara nyingi tumekuwa tukiishauri Serikali iitenganishe wizara hiyo kwani ni kubwa na nyeti ila sasa wameona ushauri wetu unafaa na kuzitenganisha," amesema Mbowe. Amesema suala siyo nani anafaa kuwa waziri na nani hafai kuwa waziri au ukubwa wa wizara ila suala ni kuona namna gani ya kuendesha Serikali ya Awamu ya Tano. er 07, 2017 No comments Babati.  Mwenyekiti wa Chadema,

FT: TANZANIA 1-1 MALAWI kKUTOKA UWANJA WA UHURU

Image
Kikosi cha timu ya Taifa Stars kilichoanza dhidi ya Malawi leo Uwanja wa Uhuru Dar. Kikosi cha timu ya Malawi. MPIRA UMEKWISHA Dk 90+4 Samatta yuko chini anatibiwa baada ya kugongana na beki wa Malawi wakati akijaribu kufunga, wote wametolewa nje kutibiwa Dk 90+2 Muzamiru analambwa kadi ya pili ya njano na kuwa nyekundu ya pili kwa Taifa Stars Dk 90 nafasi nyingine ya Taifa, lakini kipa wa Malawi anaokoa Dk 90 nafasi nyingine ya Taifa, lakini kipa wa Malawi anaokoa Dk 88 Mbaraka Yusuf anapoteza nafasi akiwa yeye na lango, kazi nzuri ya Samatta ameshindwa kuitumia Dk 85, Nyoni amepewa kadi nyekundu, mwamuzi anamtuhumu kumpiga mwenzake kiwiko lakini mchezaji huyo wa Malawi, hakuadhibiwa kwa kuwa alimvamia Nyoni Dk 83 Abdul Hilal anayecheza Tusker ya Kenya anaingia kuchukua nafasi ya Simon Msuva anayecheza Difaa Al Jadid ya MoroccoDk 78, inaonekana mashambulizi ya Malawi kutoka upande wa mashariki ni hatari kwa afya ya lango la Tanzania Dk 70, Taifa Star

ZITTO KABWE AFUNGUKA KUHUSU BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI

Image
Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama cha ACT -Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe, ametoa maoni yake juu ya Baraza jipya la Mawaziri lililofanyiwa mabadiliko hii leo, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli. Kwenye ukurasa wake wa Facebook Zitto Kabwe ameandika ujumbe akiwapongeza Mawaziri hao walioteuliwa ambao wengi wao ni vijana, huku akiwataka kuchapa kazi kwa bidiiUteuzi wa vijana kushika nafasi za juu ni hatua nzuri, naona vijana wengi wamepewa majukumu makubwa, ninawaombea watekeleze majukumu kwa weledi mkubwa”, ameandika Zitto Kabwe. Leo Rais Magufuli amefanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na kuongeza wizara mpya mbili, baada ya kuzivunja baadhi ya wizara ambazo zilikuwa na vitengo vingi.

JPM Ateua Mawaziri Wapya, Lugola, Shonza Ndani, Maghembe, Kashililah Out

Image
Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri nchini huku akizigawanya baadhi ya wizara zikiwemo Wizara ya Kilimo na Mifugo, Nishati na Madini na kuongeza wizara mpya mbili na kufikisha jumla ya wizara 21. Katika Mabadiliko hayo, Mawaziri wawili na manaibu waziri wameongezwa. Aidha Rais Magufuli ametangaza mabadiliko na kuteua Katibu mpya wa Bunge huku akieleza kuwa aliyekuwa Katibu wa Bunge, Thomas Kashilila atapangiwa kazi nyingine. ORODHA. Wizara ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu: Naibu Waziri – Stella Alex Ikupa Wizara ya Mifugo na Uvuvi: Waziri – Luhaga Mpina, Naibu Waziri -Abdallah Hamisi Ulega. Wizara ya Maji na Umwagiliaj: Waziri- Mhandisi Isack Kamwelwe, Naibu Waziri – Jumaa Hamidu Aweso. Wizara ya Nishati: Waziri – Dk. Medard Kalemani, Naibu Waziri – Subira Khamis Mgalu. Wizara ya Madini: Waziri – Angellah Kairuki, Naibu Waziri -Stanslaus Haroon Nyongo. Wizara ya Maliasili na U

BREAKING NEWS: JERRY MURO AJIBU TUHUMA NZITO ZA CHADEMA, AMVAA MAZIMA LEMA

Image
      KADA maarufu wa Chama Cha Mapinduzi, ambaye pia aliwahi kuwa Msemaji wa klabu ya yanga, Jerry Muro ameibuka na kuwaponda viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) huku akiwataka waache porojo na badala yake wajikite katika kuwaletea maendeleo wananchi wao.Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Muro amewataka viongozi wa Chadema wanaodai kuwa wanafuatiliwe na watu ili wauawe, waseme wanafuatiliwa na akina nani?“ Nimemsikia baadhi ya wabunge wa Chadema wakisema kuna watu wanawafuatilia, dada yangu kule Bunda (Ester Bulaya) akisema anafuatiliwa na watu waliovaa kininja, nani awafuatilie nyie? Kwani mmeiba makinikia?“Lema naye anasema wamefungua nati za gari lake, pia anadai akiwa kwenye mwendokasi aliona watu wanamfuatilia akaruka kwenye gari akamwachia usukani mkewe, hivi kweli gari lipo kwenye mwendokasi unarukaje kichakani? Acheni maigizo jamani…” Nani akutafute wewe Lema? Mbona husemi wakati ukiwa na nywele za rasta ulikuwa un