Posts

Showing posts from September 24, 2016

Azam Yafungwa Bao 2- 1 Dhidi Ya Ndanda FC

Image
Wachezani wa Azam akiwania mpira na wa Ndanga Fc. (Picha na Maktaba)   Azam FC imepoteza mechi yake ya pili leo baada ya kuchapwa kwa mabao 2-1 na wenyeji wake Ndanda FC.   Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Azam FC ilipoteza mechi hiyo katika dakika za mwisho baada ya kucheza vizuri katika kipindi chote cha kwanza.   Nafasi kadhaa walizopoteza, pia katika kipindi cha pili watazijutia kwa kuwa Ndanda walitumia vizuri nafasi walizozipata.   Nao JKT Ruvu, wamezidi kuonyesha hawataki tani baada ya kuitwanga Mbeya City kwa mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa mkoani Pwani.   Mtibwa Sugar ikiwa nyumbani, baada ya kuongoza kwa muda mrefu imejikuta ikizuiliwa na kukamtwa kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbao FC.   Mtibwa Sugar waliongoza kwa muda mrefu, jioooni wakaruhusu bao hilo la kusawazisha na kuwafanya wapoteze pointi nyingine mbili.

Simba Yaipiga Majimaji Nne Kwa Mtungi

Image
Wachezaji wa Simba wakishangilia. KIKOSI cha Simba, leo kimefanya mauaji ya kutisha mbele ya Majimaji ya Songea baada ya kuichapa mabao 4-0 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar. Simba anayonolewa na Mcameroon, Joseph Omog, ilipata mabao yake kupitia kwa Jamal Mnyate aliyefunga mawili sawa na Shiza Kichuya ambaye naye aliingia nyavuni mara mbili. Kwa matokeo hayo, Simba imeendelea kukalia usukani kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 16 baada ya kushuka uwanjani mara sita ambapo imefanikiwa kushinda michezo mitano sare mmoja. Huko Mtwara Azam FC imebanwa mbavu na kuacha alama tatu mbele ya Ndanda baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1. Kesho Yanga inatarajiwa kucheza na Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

FAHAMU AINA NNE ZA WANAWAKE MICHEPUKO

Image
1.MCHEPUKO LAMI: Huu ni ule ambao hauombi pesa, katulia hana mapepe, uwe naye au usiwe naye maisha yake yanaendelea tu. 2. MCHEPUKO VUMBI: Huu ni ule wa vibomu!! mara ooohhh sina pesa, naomba vocha, sijui simu imekufa, oooh mara nipo saluni nadaiwa elf thelathin, naomba nauli…..n.k! Na hii ndio noma maana njia kuu lazima washtuke mana mchepuko vumbi unachafua na unasumbua full time. 3. MCHEPUKO KOKOTO: Huu ni mkali zaidi ya njia kuu maana kila mara huuliza upo wapi, Uko na nani, why hupokei simu yangu? Kama uko kwako naomba utoke nje tuongee kidogo na leo uwe na mimi tu…Yaani tabu tupu! 4: MCHEPUKO MATOPE: Yaani huu usiombe hata kukutana nao maana wenyewe ndio funga kazi.. Huu bana unajua kuchuna hasa ila pale unapoupa pesa na wenyewe unaenda kuzihonga zote kwa mchepuko wake mwingine yaani hatari tupu

MANCHESTER UNITED WAIBUKIA KWA LEICESTER CITY,WAITANDIKA BAO 4

Image
Manchester United 4-1 Leicester City: Paul Pogba looked to the heavens after scoring his first Manchester United goal and their fourth of the afternoon The £89million signing lost Christian Fuchs and met Daley Blind's corner to send a header into the far corner Pogba celebrated his goal with Jesse Lingard as United ran rampant in the first-half at Old Trafford Pogba soaks up the acclaim of the Old Trafford support after scoring his first goal since returning to the club Marcus Rashford slides in to convert United's third goal from close range following Daley Blind's well-worked corner Juan Mata lashes home United's second goal after a classy move that saw Paul Pogba and Jesse Lingard combine Chris Smalling, Jesse Lingard, Daley Blind and Marcus Rashford rush to congratulate Juan Mata after United's second goal Smalling leaps above the Leicester back line to head home Daley Blind's corner and give United a 22nd-minute

KINANA,NDUGAI WATETA LUMUMBA LEO

Image
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Spika wa Bunge Job Ndugai, wakati Spika alipofika kumsalimia, Ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2016. Kushoto ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka.  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimwongoza kutoka nje Spika wa Bunge Job Ndugai, baada ya mazungumzo yao, wakati Spika alipofika kumsalimia, Ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2016. Nyuma ya Sika ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Msemaji wa CCM Christopher Ole Sendeka, wakisubiri kuondoka Spika wa Bunge Job Ndugai Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2016. (Picha zote na Bashir Nkoromo).

DIAMOND PLATINUMS NA ZARI THE BOSS LADY WATIKISA VISIWANI ZANZIBAR

Image
Leo septemba 23 ni siku ambayo Zarithebosslady anasherehekea siku yake ya kuzaliwakatika kusherehekea siku hii muhimu mpenzi wake Diamond Platnumz, pamoja na mtoto wao Princess Tiffah wameambatana na baadhi ya watu wao wa karibu na kwenda mapumzikoni visiwani Zanzibar. Angalia Picha Jinsi Walivyowasili Visiwani Humo. Diamon Platnumz, Zari, Princess Tiffah na Mwarabau Fighter (Baunsa Wa Mondi) Diamond Platnumz na Mwanae Princess Tiffah.

Zari, Mobeto Kimenuka Tena!

Image
  Mwanamitindo Hamisa Mobeto. DAR ES SALAAM: Kimenuka tena! Ndiyo unavyoweza kusema baada ya mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kutupia picha ya hereni kwenye Mtandao wa Kijamii wa Snapchat huku akitupa dongo kwa kusema aliyesahau vitu vyake aende akavitoe, bifu limeibuka upya mitandaoni.   Mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’. Baada ya kutupia picha ya Snapchat hiyo, mashabiki mbalimbali wa mtandao huo walijiongeza na kuoanisha na picha ya Mwanamitindo Hamisa Mobeto kwa kufananisha hereni alizovaa siku za nyuma zikifanana na hizo alizodai Zari zimesahaulika kwenye chumba cha Diamond, nyumbani kwake, Tegeta-Madale jijini Dar. Mbali na mashabiki hao kujiongeza, mjadala mzito uliibuka pia wakidai ugomvi wa Zari na Mobeto si rahisi kumalizika maana kati yao hakuna anayeweza kuwa mpole na kumwachia mwenzake atambe. “Hili

LOWASSA AISIFU SERIKALI URATIBU MAAFA KAGERA

Image
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa akisalimiana na  Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Generali Salum Kijuu alipomtembela leo ofisini kwake kumpa pole kutokana na athari ya tetemeko la ardhi katika mkoa wake Na Mwandishi Wetu-KAGERA. Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa ameipongeza Serikali kwa namna ilivyojipanga kukabiliana na athari za tetemeko la ardhi lililotokea mkoani humo.Bw. Lowassa amesema hayo kupitia salamu zake alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Generali Salum Kijuu, ofisini kwake kumpa pole kutokana na athari zilizotokana na tetemeko hilo.“Napenda nikupongenze mkuu wa mkoa kwa namna ulivyokabili tukio hili, wala hatukuwa na mashaka wewe ni mtaalam wa majeshi wa siku nyingi kwa hiyo jambo hili limempata mwenyewe mpiganaji na tunaona kwa pamoja mmelishikilia vizuri,” alisema Lowassa. Adha Mhe. Lowassa alisema kuwa suala hili ni kubwa na halipaswi kuiachia Serikali peke yake katika kulikabili nalo kwani madhara yanaonekana ni makubwa