Posts

Showing posts from January 7, 2015

Ajifungua pacha wa kike walioungana kifua, tumbo

Image
Musoma. Mwanamke mmoja mkazi wa Kata ya Buhare, Manispaa ya Musoma mkoani Mara, Helena Paulo (20), amejifungua watoto pacha wa kike walioungana eneo la kifuani hadi tumboni wakiwa na uzito wa kilo 4.6 kwa pamoja. Tukio hilo la ajabu katika Mji wa Musoma na mkoa kwa jumla, liliwavutia hisia za wananchi hali iliyosababisha msongamano katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa madhumuni ya kutaka kushuhudia. Akizungumza katika wodi ya wazazi hospitalini hapo, muuguzi wa zamu, Naabu Geraruma alisema mwanamke huyo alijifungua juzi saa saba usiku kwa njia ya upasuaji. Geraruma alisema tukio hilo ni la kwanza katika hospitali hiyo na hali ya afya ya mzazi huyo na watoto inaendelea vizuri na muda wowote atahamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza. Kwa upande wake, Mganga wa Idara ya Magonjwa ya Wanawake, Dk Simon Kamuli alisema baada ya jitihada za kuhakikisha mwanamke huyo anajifungua salama kukamilika, kinachofuatia ni kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando