Posts

Showing posts from December 11, 2016

Meli Yenye Malori 600 ya Kiwanda cha Dangote Yawasili Mtwara

Image
MTWARA: Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Dangote Cement Industries ya jijini Mtwara, ambaye pia ni bilionea namba moja Barani Afrika, Alhaji Aliko Dangote jana Desemba 10, 2016 alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Dk Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam alimthibitishia kuwa hana lengo la kufunga kiwanda chake kama inavyodaiwa badala yake anatafuta fursa nyingine za kuwekeza hapa nchini. Katika kuthibitisha hilo, Mfanyabiashara huyo alisema jana kuwa meli yenye malori mapya 600 kwa ajili ya kusambazia saruji yake mikoani, itawasili nchini. Aliongeza kuwa lengo la kufanya biashara hapa nchini mbali na kutengeneza faida pia ana lengo la kuisaidia serikali ya Tanzania kutengeneza ajira hivyo hana sababu ya kuagiza mali ghafi toka nje ya nchi ambazo zinapatikana nchini. Baada ya kufanya mazungumzo hayo, meli yenye magari hayo 600 ilitia nanga katika bandari ya Mtwara ambapo ndipo kiwanda cha Saruji cha Dangote kilipo. Aidha, imeelezwa kuwa w

Baada ya Waziri Mkuu Majaliwa Kukabidhiwa Pembe, Mapya Tena Yaibuka Kifo cha Faru John

Image
Dar es Salaam. Kifo cha Faru John aliyehamishiwa Hifadhi ya Creta ya Ngorongoro kimeendelea kupunguza idadi ya wanyama hao ambao wanatafutwa kwa udi na uvumba na majangili kutokana na pembe zake kuuzwa ghali kwenye magendo, mara tatu zaidi ya dhahabu au dawa za kulevya aina ya cocaine. Hivi karibuni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliliibua sakata la kutoweka kwa Faru John katika Hifadhi ya Sasakwa Black Rhino Sanctuary akidaiwa kufa. Kutokana na utata wa sehemu alipokuwa Faru huyo, makachero saba walifika Ngorongoro kufanya uchunguzi na kuwakamata maofisa watano waliotajwa kuhusika katika kumhamisha faru huyo. Hata hivyo, juzi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alikabidhiwa pembe ikiwa ni kithibitisho kuwa Faru John amekufa. Pia, alipewa taarifa kuhusu utaratibu uliotumika kumhamisha kutoka Ngorongoro kwenda Sasakwa. Kilichosababisha Waziri Mkuu awe mbogo baada ya kuwapo kwa utata wa alipo faru huyo, ni upekee wake, thamani yake kiutalii na kuwa n

Mchungaji Awanywesha Waumini Dawa ya Kuua Bakteria “Dettol”

Image
MCHUNGAJI maarufu kwa jina la Rufus Phala kutoka kanisa la AK Spiritual Christian lililopo Makgodu, Limpopo, Afrika Kusini amewashangaza watu kwa kitendo cha kuwanywesha  Dettol waumini wake ilihali ina madhara kwa binadamu. Kwa mujibu wa Daily Sun SA, mchungaji huyo alifanya kitendo hicho kwenye ibada za kawaida kanisani kwake akiwataka waumini wenye matatizo na wanaohitaji maombi wanywe Dettol aliyokuwa ameishika mkononi mwake huku akiwambia watapona shida zao ikiwemo magonjwa. “Nafahamu kuwa Dettol ni sumu, lakini Mungu ameniagiza niwape na muitumie. Mimi nilikuwa wa kwanza kuinywa,”   – Mchungaji. Pia alisema kuwa amepokea meseji za WhatsApp kutoka kwa watu waliokunywa na wamethibitisha kupona. Baada ya kuwepo kwa taarifa hizo, amehojiwa Daktari kutoka Afrika Kusini, Dr Mabowa Makhomisane, ambaye amekiri kuwa Dettol ina madhara inapotumika tofauti na maelekezo ikiwemo kuinywa “Mtu akinywa Dettol na ikafika tumboni, kimsingi hupunguza m

Kamati Kuu ya CCM: Leo ni Kikao cha Kwanza kwa Mwenyekiti JPM, Yatakayojadiliwa Yapo Hapa

Image
Dar es Salaam. Kamati Kuu ya CCM inakutana leo huku kaulimbiu ya “Hapa Kazi Tu” ikitarajiwa kutawala kikao hicho cha kwanza kwa mwenyekiti John Magufuli, ambaye ameonyesha dalili za kufumua sekretarieti wakati huu wa kuelekea uchaguzi wake mkuu. Kikao hicho cha siku mbili kitachofuatiwa na kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa, pia kinatarajiwa kujadili mambo mengine nyeti, kama maandalizi ya uchaguzi utakaofanyika mwakani kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa kwa kuchagua kamati Kuu mpya na suala la uchaguzi wa meya wa Kigamboni ambayo sasa ni wilaya. Pia kikao hicho kinatarajiwa kujadili chaguzi ndogo za mbunge wa Dimani na madiwani pamoja na ripoti ya wasaliti ambayo Magufuli alikabidhiwa na mtangulizi wake, Jakaya Kikwete Julai 23 baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti. Suala jingine linalotarajiwa kuchukua nafasi ni hali ya kisiasa nchini, ikijumuisha suala la Zanzibar, upigaji marufuku mikutano ya hadhara, hali ya kiuchumi ambayo inalalam

ALI KIBA, LADY JAYDEE NA DJ BONNY LOVE WANG'ARA TUZO ZA EATV 2016

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akikabidhi Tuzo ya Heshima kwa DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love baada ya kutangazwa mshindi wa heshima katika tuzo za EATV AWARDS 2016 zilizofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam. Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akimsikiliza DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love alipokuwa akitoa shukurani zake mara baada ya kupokea tuzo yake ya heshima iliyotolewa na EATV. Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Lady Jay Dee akipongezwa na Mpenzi mara baada ya kupokea tuzo yake katika hafla ya utoaji wa tuzo za EATV AWARDS zilizofanyika kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam. Mwanamuziki Ali Kiba akipokea tuzo yake ya ushindiwa Wimbo Bora wa Mwaka kutoka kwa Nandi Mwiyombela kutoka kampuni ya Vodaco Tanzania katika Tuzo za Muziki za EATV AWARDS zinazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam. Msanii wa Muzi