Posts

Showing posts from March 20, 2017

MBUNGE ZITTO KABWE AMPONGEZA KAMANDA TUNDU LISSU BAADA YA USHINDI WAKE

Image
CHAMA cha ACT-Wazalendo kinachoongozwa na Zitto Kabwe, kimempongeza Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, kwa kushinda kiti cha urais wa Chama cha Wanasheria (TLS) katika uchaguzi uliofanyika juzi jijini Arusha. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Msafiri Mtemelwa, alisema Lissu anastahili pongezi kwa kufanikiwa kushinda nafasi hiyo kutokana na changamoto zilizomkumba katika kuisaka. Alisema kuwa licha ya kupitia misukosuko mingi iliyokuwa inaonyesha njia ya kumkwamisha kufikia malengo yake, Lissu hakukata tamaa na alionyesha ujasiri. Mtemelwa alisema kupata nafasi hiyo kwa kiongozi kutoka upinzani ni dalili njema na kipimo kwa wapinzani na kwamba anapaswa kuitendea haki nafasi hiyo kwa ustawi wa vyama hivyo vya upinzani. “Mimi niseme tu kwamba, Lissu anastahili pongezi," Mtemelwa alisema. "Tunahitaji watu kama hawa, watu majasiri. Pamoja na kwamba ali

Nape aunda tume kuchunguza uvamizi wa Makonda Clouds

Image
Dar es Salaam. Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye ameunda kamati ya kuchunguza kuhusu tukio lililofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kutaka apewe matokeo ndani ya saa 24. Nape ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari  mara baada ya Mkurugenzi wa Vipindi na Uaandaji wa Clouds Media Groups, Ruge Mutahaba kuthibitisha kuwa Makonda alivamia kituo hicho, Ujumaa usiku akiwa na polisi wenye silaha.  “Matukio kama haya hutokea pindi nchi inapotaka kupinduliwa, lakini kama Rais yupo na nchi haijapinduliwa  basi kuingia ndani ya chombo cha habari na silaha, huku ni sawa na kunajisi uhuru wa habari,” alisema Nape

RUGE MUTAHABA AFUNGUKA YOTE JUU YA RC MAKONDA KUVAMIA KITUO CHAO

Image
Stori iliyotrend jana siku nzima kuhusu Mkuu wa Mkoa Paul Makonda Kuvamia kituo cha Polisi na Bunduki usiku wa Ijumaa imedhibitishwa leo na Mkurugenzi wa Kituo hicho Ruge Mutahaba akiongea katika kipindi cha 360 Ruge Mutahaba amefunguka A to Z na Kuelelezea tukio lilivyotokea mpaka Mkuu huyo wa mkoa kuchukua recordings za dada ambaye alirekodiwa na Shilawadu lakini hawakuweza kurusha kwa vile stori haukubalance.... Ruge Amedai Makonda ni Rafiki yake lakini kwa hilo inabidi aombe radhi Watanzania Kwa vile Radio ya Clouds inasikilizwa na watu wengi Tanzania...