Profesa Kabudi: Niliandika barua ya kujiuzulu lakini ilichanwa
FRIDAY JANUARY 24 2020 Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje nchini Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuna wakati aliandika barua ya kujiuzulu lakini alinyangāanywa na ikachanwa. Mbunge huyo wa kuteuliwa na Rais ameeleza hayo leo Ijumaa Januari 24, 2020 Ikulu jijini Dar es Salaam katika hafla ya utiaji saini makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na kamati ya madini ya Barrick. Kabudi anasema alichukua uamuzi wa kuandika barua hiyo baada ya mchakato wa majadiliano na wajumbe wa Barrick kuwa magumu, kwamba aliona aibu kushindwa kazi aliyotumwa. Amemtaja aliyemnyangāanya barua hiyo ambayo haikuifafanua kwa kina ni Kasmir Simbakuki. āNilifikia hatua nikafanya dhambi ya kukata tamaa nikasema jambo hili haliwezekani, niliona ni bora aibu na fedheha hiyo niibebe lakini barua niliyoandika sikufanikiwa kuileta.ā āNilisema sijawahi kutumwa kazi na mkuu wangu wa nchi ikanishinda,ā amesema Kabudi. Amesema wakati huo aliku...