Posts

Showing posts from January 22, 2020

Kigwangalla: “Walipanga Kuniangamiza, Walitaka Nitumbuliwe”

Image
WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dkt Hamis Kigwangalla, ameeleza kuwa kwa sasa anaishi kwa hofu na tahadhali kubwa juu ya uhai wake kutokana na kuwepo kwa kundi la watu wanaomuwinda wakitaka kumuangamiza huku wengine wakimfanyia mipango ya kumuharibia ili atumbuliwe uwaziri. Kupitia akaunti yake ya instagram Kigwangala ameweka wazi kuwa hata alivyopata ajali aliwekewa ulinzi mkali wodini ili wabaya wake wasiweze kummalizia kwa namna yoyote. Kupitia instagram yake ameandika hivi; Sikusudii kufanya press conference. Watu wengi wamenishauri niishie hapa. Team yangu imefanya kazi nzuri, imenipa uthibitisho wa majina ya wanaotaka nichafuliwe ili niondolewe uwaziri. Bahati mbaya hakuna cha kunichafua nacho, wanapika hadithi za kitoto na kurudia tu. Walidhani ningekaidi maelekezo ya Mhe. Rais juu ya mgogoro wa ndani ya Wizara yetu ili Rais achukie aniondoe, wakakwama. Sikukaidi. Wakaona wafanye mwendelezo kupitia gazeti, sijataka kujibishana nalo, tutakutana mahakamani ambapo m

Shiza Kichuya Aanza Kazi Simba SC leo

Image
BAADA ya kuvuna pointi sita muhimu katika michezo miwili ya Ligi Kuu Bara huko Kanda ya Ziwa, kikosi cha Simba leo kinaingia kambini kujiandaa na mchezo wa Kombe la FA, huku kiungo mshambuliaji Shiza Kichuya akiwemo kati yao. Simba inajianda na mechi ya Mwadui FC ya mkoani Shinyanga itakayopigwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, Jumamosi hii. Katika mchezo huo, Simba wataingia uwanjani wakiwa na hasira za kufungwa katika mchezo wa ligi uliopigwa Uwanja wa Kambarage huko Shinyanga ambao ulimalizika kwa Mwadui kushinda bao 1-0. Akizungumza na Championi Jumatano, Meneja Mkuu wa timu hiyo, Patrick Rweyemamu alisema kuwa kikosi chao kitaingia kambini leo jioni huko Ndege Beach nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Rweyemamu alisema kuwa maandalizi ya mchezo huo yanakwenda vizuri na wachezaji wote wataingia kambini tayari kwa kuwawinda Mwadui kwa ajili ya kulipa kisasi cha kufungwa katika ligi. Aliongeza kuwa kiungo wao wa zamani Kichuya huenda akawa katika sehemu y

Mshitakiwa Afariki Mahakamani

Image
SHUGHULI zilisimama kwa muda katika Mahakama Kuu mjini  Mbale  nchini  Uganda  baada ya mtuhumiwa kuanguka na kufariki dunia. Simon Mayuya  mwenye umri wa miaka 54 ambaye ni mkazi wa kijiji  Buyobo  Wilaya ya  Sironko  nchini  Uganda,  alifariki dunia muda mfupi baada ya kuanguka katika chumba cha watuhumiwa kabla ya kupandishwa kizimbani. Mayuya alikuwa amekaa miezi sita rumande katika gereza la  Maluku  ambapo alikua anakabiliwa na tuhuma za jaribio la mauaji. Anatuhumiwa kwa jaribio la kumuua binamu yake ambaye amemuajiri kama dereva wa lori. Mwanasheria wa  Mayuya  aitwaye  David Moli  amesema mteja wake alikuwa anasumbuliwa na maumivu ya uti wa mgongo kutokana na kunusurika kwenye ajali ya gari aliyopata kabla ya kukamatwa na kuwekwa rumande. Moli ameongeza kuwa kabla hali ya mteja wake kuwa mbaya aliiomba mahakama kumpa dhamana ili apelekwe hospitali kupatiwa matibabu kabla ya kurejea tena gerezani. “Leo tulitakiwa kuwepo mahakamani kwa ajili ya kusikili

Amkata Kichwa Bosi Wake Kisa Kutomlipa Mishahara

Image
FUNDI makenika wa Halmashauri ya Wilaya ya  Sumbawanga  mkoani Rukwa,  Cathbert Mwangalaba  (47) ameuawa kwa kukatwa mwili wake na kiwiliwili chake, kutenganishwa na kichwa na kitu chenye ncha kali. Mlinzi ambaye alikuwa ameajiriwa na marehemu anadaiwa kumuua mwajiri wake huyo kwa kumchinja na kiwiliwili chake kutenganishwa na shingo yake. Anatuhumiwa kutenda ukatili huo, baada ya bosi wake huyo kushindwa kumlipa msh ahara wa miezi sita unaofikia Sh 360,000. Baada ya kumuua, mwili wake ulifukiwa katika shimo lililochimbwa shambani mwake katika Kijiji cha Kaondo Manispaa ya Sumbawanga. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Justine Masonje alithibitisha matukio hayo. Alisema kwamba mauaji ya kikatili ya Mwangalaba, yanadaiwa kufanyika saa 3:00 asubuhi Januari 17, mwaka huu shambani mwake kijijini Kanondo. Mwili wa marehemu ulibainika ukiwa umeviringishwa katika mfuko wa sandarusi, ukiwa umefukiwa katika shimo lililo ndani ya uzio wa shamba hilo. Baada ya kuchunguzwa, mwil

TCU Yavifutia Usajili Vyuo 9 Tanzania

Image
TUME ya Vyuo Vikuu ( TCU ) imefuta hati za usajili wa vyuo vikuu vishiriki vitano, vyuo vikuu vitatu na chuo kikuu kishiriki kimoja. Akizungumza jana Jumanne, Januari 21, 2020, jijini Dar es Salaam Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa,  amesema vyuo hivyo vimeshindwa kujirekebisha na hata vingepewa muda zaidi visingeweza. Amesema vyuo vishiriki ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu Yakobo (AJUCO), Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Kardinali Rugambwa (CARUMUCo) na Chuo Kikuu cha Theofilo Kisanji (Teku-Dar es Salaam), Chuo kikuu cha Mtakatifu Yohana cha Tanzania Kituo cha St Marks na Chuo Kikuu cha Jomo Kenyatta cha Kilimo tawi la Arusha (JKUA). “Kufuatia mashauriano na maombi yaliyofanywa na wamiliki wa vyuo na tume katika kikao chake cha 97 kilichofanyika Januari 20, 2020,  imeridhia maombi ya wamiliki hao kusitisha utoaji wa mafunzo, hivyo tume imefuta hati za usajili wa vyuo hivyo vishiriki na kuvifutia vibali,” amesema Profesa Kihampa. TCU pia imefuta hat