Posts

Showing posts from July 25, 2017

TRA yaanika deni la Acacia, ni sawa na 'bajeti ya miaka 13'

Image
Mamlaka ya Mapato (TRA) imeitaka Kampuni ya Acacia kulipa zaidi ya Sh424 trilioni kutokana na ukwepaji kodi ilioufanya kuanzia mwaka 2000. Kwa kutumia bajeti ya sasa, fedha hizo ni sawa na bajeti ya Tanzania ya miaka 13. Deni hilo, ambalo ni sawa na dola 190 bilioni za Kimarekani limetokana na hesabu zilizopigwa kwa kutumia taarifa iliyotolewa na kamati mbili zilizoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza usafirishaji wa mchanga wa madini unaofanywa na kampuni hiyo kutoka migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi. Taarifa iliyotolewa jana na kampuni hiyo imekataa kulipa deni hilo kwa maelezo kwamba haijapewa ripoti ya kamati zote mbili. “Hatuyakubali makadirio haya. Kampuni itaangaalia haki na namna zote zilizopo kuhusu suala hili,” inasema taarifa hiyo. Kwa mujibu wa Acacia, deni hilo limeelekezwa kwa kampuni zake tanzu ambazo ni Bulyanhulu Gold Mine (BGML) inayoendesha mgodi wa Bulyanhulu, na Pangea Minerals (PML) inayosimamia mgodi wa Buzwagi. Taarifa hiyo iliyo

Masanja Alivyokutana na Majeruhi wa Lucky Vicent nchini Marekani

Image
Emmanuel Mgaya, Maarufu kama Masanja Mkandamizaji akiwa nchini Marekani amekutana na kuzungumza na watoto Sadia na Wilson ambao ni majeruhi ya ajali ya shule ya Lucky Vicent ya jijini Arusha wanaopatiwa matibabu nchini humo.  Masanja pia kupitia ukurasa wake wa instagram amethibisha kukutana na watoto hao: MUNGU AMENIPA NEEMA YA KWENDA KUWAONA WADOGO ZETU WALIOPATA AJALI SADIA NA WILSON NA KUWEPO MAREKANI KWA MATIBABU….. IMEKUWA SIKU NJEMA KWETU SOTE TUMEFURAHI PAMOJA NAO KULA NAO NA KUMTAFAKARI MUNGU KWA PAMOJA. LAKINI PIA NIMEZUNGUMZA NA WENYEJI WAO WALIOFANIKISHA SAFARI YA WAO KUJA MAREKANI!! HAKIKA MUNGU NI MWEMA WAMEENDELEA KUIMARIKA NA WANAENDELEA VIZURI!! SHUKRANI KWA MADAKTARI NA KILA ALIYETENGA MDA WAKE KUWAOMBEA!! WAZAZI WAO WANAWASALIMU NA WANAWASHUKURU KWA USHIRIKIANO NA MAOMBI YENU..🙏🏾🙏🏾🙏🏾 Tazama picha:

TCU Yataja Vyuo Vilivyozuiliwa Kudahili Wanafunzi 2017/18

Image
Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imetoa orodha ya vyuo vilivyozuiliwa kufanya udahili wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa masomo 2017/18. Orodha hii imetolewa wakati wahitimu wa kidato cha sita wakiwa wanaendelea na mchakato wa kutuma maombi vyoni.  

Rihanna ‘The Bad Gal’ Uhuni, Usela Vinampa Mkwanja Mnono

Image
Rihanna. UKIMTAZAMA mwonekano wake jinsi alivyo mrembo, mwenye haiba nzuri ya kike, mvuto wa asili na sauti yenye utamu wa aina yake, huwezi kumdhania kwamba nyuma ya pazia ni mhuni na ‘msela’ aliyepitiliza! Jina lake halisi anaitwa Robyn ‘Rihanna’ Fenty, anapenda zaidi ukimuita Riri au The Bad Gal, mwanadada asiyechuja kutoka Visiwa vya Barbados, anayefanya poa kinoma kwenye anga la muziki wa kimataifa, maskani yake yakiwa nchini Marekani. Jina lake ni miongoni mwa wasanii wachache wa kike wanaoitingisha dunia kwa sasa, akichuana vikali na Beyonce Knowles, ingawa wapo baadhi ya watu wanaosema si sahihi kuwapambanisha wawili hao kwani Beyonce ni mkongwe na ana mafanikio zaidi ya Rihanna. Miongoni mwa matukio ya hivi karibuni yanayodhihirisha jinsi Rihanna ‘alivyopinda’, ni kwenye video ya Wimbo wa Wild Thoughts wa DJ Khaled , akiwa amemshirikisha mwanadada huyo na chalii mwingine, Bryson Tiller. Ukiisikiliza ngoma hii iliyoachiwa mwishoni mwa mwezi uliopita,

ZARI THE BOSS LADY AIBUA MAZITO TENA BAADA YA KIFO CHA MAMA YAKE,WASEMA ANA ROHO NGUMU

Image
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na mama yake, Halima Matovu Hassan ‘Mama Zari’ enzi za uhai wake. Kifo cha mama mzazi wa staa ambaye ni mjasiriamali Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Halima Matovu Hassan ‘Mama Zari’ (58) kilichojiri Alhamisi iliyopita nchini Uganda, kimeibua gumzo ambalo si la nchi hii.Gumzo hilo kutoka nyumbani kwa mama Zari huko Busunju, Munyonyo jijini Kampala, Uganda lilihitimishwa wikiendi iliyopita na vyombo vya habari za mastaa nchini humo baada ya mazishi ya mama Zari yaliyofanyika mchana wa Ijumaa iliyopita, kuwa, Zari ana roho ngumu aisee!Kwa mujibu wa vyombo hivyo, wakati wa kifo cha aliyekuwa mume wa Zari, Tycoon Ivan Ssemwanga ‘Don Ivan’ aliyefariki dunia Mei 25, mwaka huu, mwanamama huyo, kabla, wakati na baada ya mazishi ya baba watoto wake huyo alikosolewa juu ya tabia alizozionesha wakati wa msiba huo.Ilielezwa kuwa, baadhi ya mambo aliyoyafanya wakati ule ikiwemo kuposti vitu mitandaoni, mara akik