Posts

Showing posts from November 27, 2013

ANGALIA NAFASI ZA KAZI KUTOKA SERIKALINI .ZIPO NAFASI 2,748.

Image
Serikali kupitia Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inawatangazia watanzania wenye sifa na uwezo kujaza jumla ya nafasi wazi za kazi 2,748 kwa ajili ya waajiri mbalimbali Nchini. Kwa mujibu wa Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi nafasi hizo za kazi ambazo zinapatikana katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira ambayo ni  www.ajira.go.tz  ni kwa ajili ya waajiri mbalimbali wa Ofisi za Umma. Daudi alitaja nafasi za kazi zinazotangazwa kuwa ni :- Afisa Uvuvi daraja la ii, Mvuvi msaidizi daraja la ii, Afisa Mifugo msaidizi daraja la ii, Afisa mifugo daraja la ii, Mteknolijia wa  samaki daraja la ii, Daktari wa mifugo daraja la ii,Afisa utafiti Mifugo daraja la ii, Daktari utafiti Mifugo daraja la ii, Fundi sanifu Maabara Mifugo daraja la ii, Mkufunzi Mifugo daraja ii, Mkufunzi wa Mifugo msaidizi na Daktari Mifugo. Kada nyingine ni Mkufunzi daraja la ii, Mtekinolojia wa Samaki

HII NDIO HABARI KUHUSU GARI JIPYA KABISA LINALOJIENDESHA LENYEWE:

Image
Taarifa ikufikie kutoka Samukawa, Kanagawa Japan ambako stori kwenye headlines ni kampuni ya Nissan kupata furaha kubwa baada ya kufanikiwa kwa jaribio la gari walilolitengeneza ambalo linajiendesha lenyewe. Unaambiwa limetembea umbali wa kilometa 2.3 likijaribiwa kwenye mikikimikiki ya aina mbalimbali barabarani kama vile kuovertake, kufata alama za barabarani, taa za kuongozea magari na hata sehemu za watu kuvuka barabara. Nissan wamesema wanalengo la kuanza kuliuza hili gari miaka saba kutoka sasa, hiyo itakua mwaka 2020 ambapo gari hili lina kamera maalum pamoja na sensors zinazofanikisha kulipa taarifa ya tukio husika kwa wakati huo ndio maana linaweza kufanya kama inavyotakiwa mfano kushika breki, kukanyaga mafuta na vitu vingine. Kingine cha kushangaza, kwa mfano kwenye miji mikubwa ambayo parking ni tatizo unaweza kuliacha likajiendesha lenyewe kwenda kutafuta parking wakati wewe unawahi mahali alafu ukimaliza shughuli zako unalikuta linakusubi

ANGALIA PICHA ZA MTOTO MDOGO APASULIWA VIBAYA USONI

Image
  Wakati Dunia ikipinga vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto hapa nchini Bado vitendo hivyo vimeonekana vikiendeleea ambapo MTOTO Mmoja BENSON TOLE mwenye umri wa miaka Mitano mkazi wa Ruhuwiko mjini Songea mkoani Ruvuma, amenusurika kifo baada ya kukatwakatwa kwa kitu chenye ncha kali sehemu za usoni na Mzee mmoja LONGINUS HAULE mwenye miaka 51 akimtuhumu mtoto huyo kumuibi a matunda aina ya Mapera shambani kwake.   EMMANUEL MSIGWA kutoka mjini Songea  Mtoto BENSON TOLE kwa sasa amelazwa katika hospitali ya mkoa mjini Songea katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU), Madaktari wanaendelea kunusuru uhai wa mtoto huyu baada ya kupata mashambulio makali ya kucharangwacharangwa na kitu chenye ncha kali sehemu za usoni na mtuhumiwa mmoja LONGINUS HAULE mkazi wa Polisi Lizaboni mjini Songea. Mzee HAULE anatuhumiwa baada ya kumfanyia unyama wa kutosha mtoto huyo na kisha kupoteza fahamu akimtuhumu kumuibia matunda aina ya mapera shambani kwake a

Neno Fupi La Leo: Tumekuwa Manabii Wa 'Siku Za Mwisho Za Upinzani..'

Image
" Kipofu akinivamia na kuniumiza, nikakasirika kwa sababu ya maumivu aliyonitia, ni jambo la kibinadamu. Lakini, nikijitoboa macho ili na mimi nimvamie na kumwumiza haitakuwa nimefanya jambo la busara". - Julius Nyerere. Ndugu zangu, Kuna mawili yamenisikitisha ; maandiko ya ndugu yangu Julius Mtatiro na katuni ya ndugu yangu Marco Tibasima. Julius Mtatiro anaandika kwa masikitiko; " Na migogoro yote huwa inafurahiwa na vyama dola" . Julius amezungumzia juu ya migogoro katika vyama vya upinzani inavyoumiza vyama na demokrasia. Namfahamu Julius, nimekaa na kuongea nae mara kadhaa. Ni kijana anayeifikiria zaidi Nchi aliyozaliwa. Najua kuwa yanayotokea yanamwumiza sana. Na katuni ya Marco inajieleza. Inahuzunisha pia.   Na jioni hii kwenye redio ya Ujerumani mtangazaji ameniuliza juu ya hatma ya upinzani kuelekea 2015. Jibu langu; ni mapema mno kuzungumzia ya 2015 kwa kuangalia kinachotokea leo katika Chadema. Lakini, ni ukw

UTAFITI WABAINI KUWA: "SODA NI SUMU"

Image
*Utafiti wabaini ina kiwango kikubwa cha kemikali hatari mwilini mwa binadamu AFYA za mamilioni ya Watanzania wanaotumia vinywaji vya aina ya soda ipo hatarini, baada ya kugunduliwa uwepo wa chembechembe zenye kemikali za sumu ndani ya vinywaji hivyo, Utafiti uliofanywa na Muungano wa Waandishi wa Habari za Uchunguzi Tanzania (Investigative Journalists Union of Tanzania- IJUTA) pamoja na tafiti zilizofanywa na wataalamu waliobobea katika afya ya umma duniani, umebaini kuwa vinywaji baridi aina ya soda ni hatari kuliko utumiaji wa sigara inayosababisha maradhi ya kansa katika mwili wa binadamu. Kwa mujibu wa utafiti wa wanasayansi mbalimbali duniani, yapo madhara makubwa ya utumiaji wa vinywaji vya aina ya soda katika mwili wa binadamu. Utafiti huo unaonyesha kuwa zipo sababu nane kuu zinazokiweka kinywaji aina ya soda kwenye kun

ALICHOKIANDIKA MH ZITTO KABWE KATIKA UKURASA WAKE WA FACEBOOK

Image
Ni post ya facebook kwenye page ya Mbunge huyu wa Kigoma Kaskazini saa nne asubuhi.

MTOTO ARUDISHA PENZI LA MONA, TYSON

Image
                                                    Stori: Imelda Mtema NDOA ya mastaa wa filamu Bongo, George Tyson na  Yvonney Chery ‘Monalisa’ iliyovunjika kitambo, ilirejewa na uhai wa saa kadhaa katika shughuli ya kumpongeza binti yao mpendwa Sonia baada ya kupata kipaimara. George Tyson akimlisha keki Yvonney Chery ‘Monalisa’ wakati wa sherehe hiyo. Mwandishi wetu aliwashuhudia wawili hao wakionekana dhahiri kuweka tofauti zao pembeni na kujali shughuli ya binti yao iliyofanyika Jumapili iliyopita nyumbani kwa mama mzazi wa Monalisa, Suzan Lewis ‘Natasha’,  Yombo –Buza, Dar. Monalisa akimnywesha kinywaji Tyson. Muda wote walionekana wenye furaha na waliketi kwenye meza moja huku Monalisa akionesha heshima wakati wa kumlisha keki Tyson kwa kupiga magoti. “Hawa jamani wanapendezana sana wakiwa pamoja. Jamani... mtoto wao amerudisha penzi lao. Ingefaa wakafikiria upya na kuona kuna umuhimu wa kurudiana na kumlea pamoja mtoto wao,” mmoja wa wageni waalikwa

RAIS KIKWETE AMSIFU DIAMOND NA MAREHEMU MICHAEL JACKSON KWA KUWANA NIDHAMU

Image
Rais Jakaya Kikwete amewataka wasanii wa muziki kuwa na nidhamu ya kazi ambayo itawajenga kimaendeleo ya sanaa pamoja na maisha yao na kuwatolea mfano Diamond Platnumz na marehemu Michael Jackson. Akizungumza jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es salaam katika semina ya fursa, Rais Kikwete alisema wasanii wasipojitambua na kujifunza watakuwa wakilaumu kila siku na kumtolea mfano Michael Jackson aliyeweza kufanikiwa mapaka akawa Mfalme wa Pop. “Kitu nilichojifunza kutoka kwa Michael ,nidhamu, kwa pale anapopanda kwenye jukwaa ,hakuna masihara,anaingia wimbo moja, anaingia wimbo mwingine,nonstop,kwamba ile ameifanya ni kazi lakini nimekaa nae akasema hivi,’tukishamaliza ile show ya siku ile,siku inayofuata muda tunautumia wote ni kuangalia video ya show yetu ile ya jana, tumekosea wapi,tuboreshe wapi,hatimaye ndio ajira yangu’. Sasa ile nidhamu aliyokuwanayo kwa ile kazi ndio maana akawa King of Pop,” alisema Kikwete.

MAKUBWA HAYA ... KIJANA MIAKA 32 ANASWA NA BIBI KIZEE MIAKA 80 ..

Image
KUNA mengi ya kushangaza duniani lakini hili la kijana Hamad Issa (32) kunaswa faragha na bibi kizee Adela Mkalau (80) linaongeza rekodi ya mambo yanayoshangaza, Risasi Mchanganyiko lina kila kitu. Hamad Issa (32) akiwa amejilaza kitandani kwa bibi Adela Mkalau (80). Tukio hilo la kustaajabisha limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita, nyumbani kwa bibi huyo, Yombo –Buza, jijini Dar es Salaam ambapo wajukuu wa bibi huyo ndiyo waliomnasa. Kwa mujibu wa chanzo chetu, wajukuu wa bibi huyo walifedheheshwa na kitendo hicho hivyo kuwawekea mtego na kuwanasa kisha kumfikisha Hamad katika Kituo cha Polisi Chang’ombe kwa tuhuma za ubakaji. Bibi Adela Mkalau (80) akiwa katika pozi. BIBI: SIJABAKWA Katika kutafuta uhakika wa madai ya wajukuu hao, polisi wa Chang’ombe waliagiza bibi yao aitwe ili athibitishe madai hayo wakati upelelezi mwingine ukiendelea. Sosi wetu alisema kuwa bibi aliwaacha hoi polisi baada ya kufika kituoni hapo na kukataa maelezo ya wajukuu zake, h