Posts

Showing posts from October 21, 2018

Breaking News: Polisi Yakanusa DCI, Mambosasa Kuondolewa

Image
Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa. MSEMAJI wa Jeshi la Polisi nchini, Barnabas Mwakalukwa, amekanusha taarifa zinazozagaa mitandaoni zinazohusu jeshi la polisi kufanya mabadiliko na kuomba wananchi kuzipuuza. Taarifa ya msemaji hiyo imeeleza kuwa mkuu wa jeshi hilo, IGP Simon Sirro,  amewataka wananchi kuzipuuza taarifa hizo zenye lengo la kupotosha umma na kuwataka kuacha kutumia mitandao ya kijamii na badala yake waitumie kupeana taarifa za kuleta maendeleo. “Serikali na vyombo vyake ina utaratibu maalum wa kutoa taarifa kwa umma,” ilisema taarifa ya Mwakalukwa. Taarifa ambazo si za kweli  zilidai Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Boaz, wamepangiwa majukumu mengine. Ziliongeza kusema kuwa Mambosasa amerejeshwa makao makuu kwenye kamisheni ya ushirikishwaji jamii,  na Charles Kenyela amekuwa DCI mpya huku Mkuu wa Chuo cha Polisi Moshi, SACP Ramadhan

Ajali mbaya yatokea Singida, Watu watano wameripotiwa kupoteza maisha

Image
Watu watano wameripotiwa kupoteza maisha kwenye ajali ya gari iliyotokea eneo la Njirii wilayani Manyoni mkoani Singida leo Oktoba 21. Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, kamishna msaidizi wa polisi Sweetbert Njewike, amesema kuwa ajali hiyo imehusisha magari mawili ikiwemo gari dogo mali ya Wizara ya Kilimo na Chakula iliyokuwa na watu watano pamoja na lori. Kamanda Njewile amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari ndogo iliyokuwa katika mwendokasi ikijaribu kupishana na lori. "Gari ndogo mali ya Wizara ya Kilimo na Chakula ilikuwa ikitokea Dodoma kwenda Shinyanga ikiwa na watumishi wa wizara hiyo, ilikuwa katika mwendokasi na kugongana uso uso na Lori", amesema Kamanda Njewile. Kamanda amewataja waliofariki kuwa ni wanawake wawili na wanaume watatu na wote wamehifadhiwa katika hospitali ya Wilaya ya Manyoni.