Posts

Showing posts from August 29, 2017

BREAKING NEWS: Lissu Awaongoza Mawakili Kugoma Kuingia Mahakamani

Image
Tundu Lissu akiakiwa na mawakili wengine wakati wakizungumza na wanahabari katika Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Dar. RAIS wa Chama cha Mawakili Tanzania (TLS), Tundu Lissu amewaongoza mawakili nchini kugoma kuingia mahakamani kwa muda wa siku mbili Agosti 29 na 30, 2017 wakilaani tukio la kushambuliwa kwa ofisi za Kampuni ya Mawakili ya IMMMA Advocates iliyolipuliwa kwa bomu usiku wa kumakia Jumamosi iliyopita. “Mengi wamefanyiwa mawakili lakini hili la juzi tumesema hatukubali kukaa kimya wakati mawakili wetu wanashambuliwa. Kwa busara za TLS tuliona tufanye maamuzi ya kusimamisha kazi kwa siku mbili ili kupeleka ujumbe kuwa jambo hilo si jema,” alisema Lissu. Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu LHRC Dr. Hellen Kijo Bisimba akizungumza na wanahabari . Kuhusu endapo mawakili wote wamegoma Lissu alisema hawezi kulizungumzia kwa sasa, hadi jioni ambapo ripoti kamili itakuwa imepatikana kwa kuwa kuna mawakili wengine walikuwa na kesi as

Mbunge wa Tunduma atakiwa kukamatwa

Image
Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Momba mkoani Songwe imeagiza kukamatwa mara moja kwa Mbunge wa Jimbo la Tunduma kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mh.Frank Mwakajoka kwa tuhuma za kuwadhihaki wateule wa Rais. Kamati ya Ulinzi na usalama wilayani ya Momba imeagiza kiongozi huyo kukamatwa baada ya kumdhihaki Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Chiku Galawa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Momba Mhe. Juma Said Irando.

Manara alalamikia Bodi ya ligi

Image
Afisa habari wa klabu ya Simba, Haji Manara Afisa habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amefunguka kwa kuwatupia lawama Bodi ya Ligi (TPLB) ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuwa wanachokifanya siyo sawa wanabidi wabadilike. Manara ameeleza hayo baada ya Bodi hiyo kufanya mabadiliko ya ratiba za mechi zinazoshiriki katika Ligi Kuu ili kupisha mechi ya kirafiki baina ya Tanzania na Botswana iweze kuchezwa mnamo Septemba 2 mwishoni mwa juma hili. "Nimesikitika sana kuona kwamba ratiba ya Ligi Kuu imebadilishwa, mechi hizi zipo kwenye kalenda ya FIFA. Mnapanga ratiba mechi ya pili tu mnaanza kubadilisha ratiba kwa hiyo sisi mechi yetu na Azam FC haitakuwepo ?", alisema Manara Pamoja na hayo, Manara ameendelea kwa kusema "mnatupunguza ile nguvu tuliyoanza nayo, hili jambo nilishalisema sana kwa nini mnavyopanga ratiba zenu bodi ya Ligi msiwe mnaangalia kalenda ya FIFA. Hivi mshawahi kusikia wapi duniani mtu anabadilisha ratiba la

Tshirt na Jinsi ya Manji yazua gumzo

Image
Huku akitia huruma, baadhi ya wananchi jijini hapa wameibua gumzo kuhusiana na nguo anazovaa mfanyabiashara maarufu, Yusufu Manji ambaye ana kesi mbili zinazomkabili. Manji ambaye alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Februari 17, mwaka huu amekuwa akikabiliwa na kesi mbili, moja ikihusu uhujumu uchumi na ya pili ni madai ya matumizi ya dawa za kulevya. Baadhi ya wananchi wamekuwa wakidai kwamba wamekuwa wakimshuhudia Manji akija mahakamani akiwa amevaa tisheti ya rangi nyeusi kwa zaidi ya mara kumi, jambo ambalo limeleta gumzo kwa kuwa wanaamini ana nguo nyingi. “Hatujui sababu, huyu bwana ni tajiri sana lakini kila akifika mahakamani anavaa tisheti nyeusi ileile, kwa nini?” alihoji mwananchi mmoja. Wapo waliomuonea huruma na kudai kwamba inawezekana anafanyiwa figisufigisu kwa kutoruhusiwa kupelekewa nguo na wengine wanadai kwamba inawezekana ameamua mwenyewe awe hivyo kama alivyoamua kutonyoa ndevu. UWAZI liliamua kumtafuta mtaalamu wa utabiri (Astrologer

FAIDA ZA UGALI WA DONA

Image
MARA nyingi baadhi ya watu huwahimiza watu wengine kutumia unga wa mahindi au nafaka zingine usiokobolewa bila ya kubainisha hasara ya unga wa aina hiyo. Watu wengi (bila shaka hata wewe msomaji wa makala haya), hawako tayari kutumia unga usiokobolewa maarufu kama dona. Kuwalazimisha watu wa aina hiyo kutumia unga usikobolewa (unga wa dona) ni sawa na kuwaweka watu hao katika hatari ya kuwa na lishe duni. UNGA WA MAHINDI Unga wa mahindi, ulezi, uwele, mtama na kadhalika ni chanzo kikubwa kwa watu wengi barani Afrika cha virutubisho kama vile wanga, protini, madini na vitamini. Hata hivyo, namna ya usagaji na matumizi ya unga wa mahindi na nafaka hizo inaweza kuukosesha mwili faida ya virutubisho vilivyomo katika nafaka hiyo. UNGA ULIOKOBOLEWA Mahindi yaliyokobolewa yaani sembe au nafaka zingine zikikobolewa kama mtama, ulezi n.k hupoteza sehemu fulani ya nafaka hizo. Kama mahindi au mtama na ulezi utasagwa bila kukobolewa unga wake huitwa unga wa dona (whole-g

Zitto Kabwe: Rais Magufuli Akiniteua Nitakataa!

Image
Rais Magufuli (kulia) akisalimiana na Zitto Kabwe, kushoto ni Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete. KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema kuwa hatokubali endapo Rais Dkt Magufuli atamteua kushika nafasi yoyote ya uongozi kwani hatakuwa na fursa ya kukijenga chama chake ili kiwe tayari kushinda uchaguzi na kushika dola. Zitto ambaye chama anachotoka tayari kimetoa viongozi wawili ambao ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Prof. Kitila Mkumbo na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Elisha Mghwira alisema endapo atateuliwa, atamshukuru Rais na kukataa uteuzi huo. Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini aliyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na gazeti la Mwananchi wakati akijibu swali kuhusu uteuzi wa viongozi wa chama chao ambao mmoja alikuwa mshauri wa chama na mwingine alikuwa mwenyekiti wa chama hicho kichanga Tanzania. “Sitakubali uteuzi kwa sababu jukumu langu na viongozi wengine wa ACT- Wazalendo ni kujenga chama ili kupata ushawis

Msukuma amjibu tena Tundu Lisu

Image
Siku moja baada ya Rais wa TLS na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kutoa wito kwa Mawakili wote ambao ni Wanachama wa chama hicho kususia shughuli za Mahakama, Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Msukuma amejitokeza na kumpinga. Licha ya kusikitishwa na kitendo cha kuvamiwa na kulipuliwa kwa Ofisi za IMMMA Advocates, Msukuma amesema kitendo cha Chama cha Mawakili kutangaza mgomo ni kutowatendea haki wateja wao kwa siku zote watakazoamua kususia shughuli za Mahakama. ”Watanzania kwa pamoja tunalaani kitendo kilichofanywa kwenye Ofisi za IMMMA Advocates kwa sababu ni kitendo cha kinyama na kihalifu. Tunamuomba IGP Sirro afanye juu chini kuhakikisha watu hawa wanakamatwa. “Nilishtushwa sana na matamko yaliyotolewa na Rais wa TLS, Tundu Lissu jana kwamba anatangaza mgomo wa Wanasheria kuanzia kesho na keshokutwa. Najiuliza kama Tundu Lissu anatangaza mgomo wa Wanasheria, hiyo ndiyo hukumu ya kumpata mvamizi? “Nadhani Wanasheria waisaidie Polisi kumgundua ni nan

Jerry Muro Amtolea Povu la Mwaka Tundu Lissu

Image
Jerry Muro. ALIYEKUWA msemaji wa Klabu ya Yanga, Jerry Muro amemtolea povu Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Tundu Lissu kutaka wanachama wote wa TLS kususia kwenda mahakamani kwa siku mbili. Muro ameyaandika haya. Tundu Lissu, TUNDUNI  Na Jerry C. Muro  Nianze kwa kutoa pole kwa jumuiya nzima ya wanasheria nchini, pole yangu sio ya tukio la IMMA Advocates, bali pole yangu ni ya kuchagua Rais wa TLS chama chenu ‘MAHIRI’ cha wanasheria Tanganyika – TLS Ndugu Tundu Lissu ambae AMEDHIHIRISHA kuwa ameanza rasmi safari ya kuizika TLS, kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari kuhusiana na tukio la IMMA Advocates. Nianze kwa kuweka msingi wa HOJA yangu kuwa sifurahishwi na kilichotokea kwenye IMMA advocates, ila pia SIFURAHISHWI zaidi na “AKILI NDOGO” za Rais wenu katika hatua za AWALI za kushughulikia suala hili. Mimi ni Profesional communicator kama mwandishi wa Habari, na Nyinyi wanasheria ni Profesional kwenye Sheria, ukisoma na Kusikiliza