Posts

Showing posts from October 27, 2013

Hatimaye sababu za Wema Sepetu na Diamond kurudiana zajulikana, soma mchezo mzima ulivyokuwa!

Image
Baada ya kimya kirefu juu ya tetesi za kurudiana kwa mwanadada Wema Sepetu na Diamond kuzagaa kwenye mitandao hasa baada ya picha za wawili hao waliokuwa wamechana kuonekana wakila “bata” pamoja maeneo ya Hong Kong huko kwenye bara la Asia, sababu na ukweli wa namna wawili hao walivyorudiana umewekwa waza baada ya hivi karibuni msanii diamond platnumz kuzungumza na mtandao wa GPL na kuelezea jinsi tukio hilo zima lilivyokuwa. Katika mazungumzo hayo Diamond alitaja mambo haya makuu matano yaliyosababisha mpaka aamue kurudisha vikosi kwa mwanadada Sepetu. Sababu ya kwanza (1) – UKARIMU WA WEMA Diamond alisema kuwa alipotua Hong Kong alishangaa kukutana na mapokezi ya Wema kwenye uwanja wa ndege jambo ambalo hakulitegemea. “Alinionesha ukarimu wa hali ya juu mno. Wakati tulipokuwa hapa Bongo tulikuwa hatusalimiani. “Kuna vitu vingi vya ajabu vilitokea huko nyuma kati yangu na Wema. Sikufikiria wala kuwaza kama anaweza akawa mkarimu kwangu kiasi kile. A

Diamond, Davido, Mohombi na Nay wa Mitego kufanya show ya bure Leaders Club leo saa tisa mchana

Image
Kutokana na kutokea hitilafu ya umeme Alfajiri ya leo kwenye show ya Serengeti Fiesta Dar, iliyopelekea baadhi ya wasanii waliokuwa wakitarajia kupanda jukwaani kutumbuiza akiwemo Davido, Mohombi, Diamond, Nay wa Mitego na wengine kushindwa kupanda, leo kuanzia saa tisa, wasanii hao watapanda tena jukwaani kuzikonga nyoyo za mashabiki wao bila kiingilio chochote. Ni katika uwanja ule ule, jukwaa lile lile la Serengeti Fiesta Dar es Salaam ambapo Diamond,Davido,Mohombi pamoja na Nay wa Mitego watapanda kuanzia saa 9 jioni mpaka saa 12. Show hiyo ya bure itapambwa pia na bendi ya Twanga Pepeta. -Habari kwa hisani ya bongo5

Tamasha la Serengeti Fiesta 2013 lilivyowasha moto usiku jana ndani ya viwanja vya Leaders Club

Image
KAMA ULIKUWEPO ULISHUHUDIA KAMA HUKUWEPO USIJALI PATA MATUKIO KWA PICHA HAPA , NA USISAHAU KULIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK