Posts

Showing posts from February 10, 2015

Je, WAJUA WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII

Image
Habari za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza kunikutanisha na nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine nazungumzia juu ya mada mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila siku. Wiki hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa. Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha. Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri. Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sif

ANGALIA IVORY COAST WAPOKELEWA NA MWALI WAO WALIVYOPOKELEWA KISHUJAA ABIDJAN

Image
HIVI NDIYO IVORY COAST MAARUFU KAMA TEMBO WALIVYOPOKELEWA NYUMBANI KWAO KATIKA JIJI LA ABIDJAN.

MAJONZI TELE DAR: MOTO WATEKETEZA WATU 6 WA FAMILIA MOJA,YUMO ASKARI WA JWTZ

Image
  Watu sita wa familia moja akiwamo Kapteni mstaafu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ), wamekufa papo hapo baada ya kuteketezwa kwa moto jijini Dar es Salaam. Janga hilo la moto limetokea jana saa 10:30 alfajiri katika eneo la Kipunguni A, Ukonga Banana, wilayani Ilala. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki alisema kuwa moto huo ulizuka ghafla katika nyumba inayomilikiwa na mstaafu huyo wa Jeshi, David Mpira anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 55 na 60. Alisema wengine waliokufa katika ajali hiyo ni mke wa marehemu, Selina Yegela anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 50 na 55, ambaye pia ni mstaafu wa iliyokuwa Kampuni ya Kuhudumia Ndege (DAHACO), sasa Swissport. Aidha, moto huo pia umesababisha vifo vya watoto wawili wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 na 30 ambao ni, Lucas Mpira na Samwel Yegela. Kamanda Nzuki alisema wajukuu wa marehemu nao wamekufa katika ajali hiyo, ambao ni Selina Emmanuel (9) mwanafunzi wa da

PICHA:Penzi la Wema Sepetu na Ommy Dimpoz lazidi kuchanua, Watupia picha wakiwa kitandani!

Image
Baada ya kuwa ni wazi sasa kuwa wawili hao wapo kwenye Le Project  flani Amazing..sasa wameamua kutupia picha kwenye kurasa zao za mitandaoni wakiwa kitandani. Alianza Ommy na badae akafuta Wema ambae aliweka picha hizo jana usiku na kuwatakia followers wake usiku mwema. Penzi la watu hawa linaendelea kuzua mvutano mkali kati ya wale ambao wanaona sawa na wale ambao wanaona kama sio sawa, wanaosema sawa wanasema kuwa baada ya watu kuachana kila mmoja ana haki ya kula maisha na anaempenda hivyo hakuna dhambi kwa wema kula raha na alikuwa shemeji yake, huku wengine wakisema wawili hao wanakosea kwasababu Ommy na Diamond ni marafiki wa karibu sana na kutilia mashaka kuwa pengine inawezekana walikuwa wakitamaniana toka enzi za Wema alipokuwa na Diamond. Ila team Wema wengi wanasema sasa ndio muda wa bidada nae kupata kitumbo…tena Ommy ni HB kushinda jamaa….

Mtoto Afungwa kwa Kutumia Mnyororo Kwenye Kitanda cha Chuma kwa Muda wa Miaka Miwili

Image
Tukio hilo limetokea jana Iringa Mjini maeneo ya Kihesa,baada ya majirani kutoa taarifa kwenye serikali ya mtaa kuwa kuna babu anamfungia ndani na kumnyima chakula mtoto wake mwenye miaka kumi ambaye ni mlemavu wa akili. Picha kama mnavyoiona hapo, dada wa kazi wa binti babu huyo sasa bado yupo kituo cha polisi hapa mjini kwa mahijiano zaid i

NGASSA AJUTA KUWATOSA EL MERREIKH, AOMBA MSAMAHA MASHABIKI WA SIMBA, ADAI YANGA WAMEMGEUKA

Image
Mrisho Ngassa Na Richard Bakana, Dar es salaam MSHAMBULIAJI wa klabu ya Yanga na Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mrisho Ngassa, amejutia uamuzi wake wa kukataa kujiunga na El Merreikh ya Sudan akisema kuwa yalikuwa ni mapenzi yake makubwa kuichezea Yanga. Akiongea na  Shaffihdauda.com  baada ya mchezo wa jana alipoibuka shujaa kwa kuifungia Yanga bao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar, Ngassa alisema kuwa baada ya kugundua alifanya makosa makubwa kuwagomea Simba na Azam FC ambao ndio walitaka kumpeleka El Merreikh, alipofunga mabao hayo alilazimika kuwaomba msamaha mashabiki kwa uamuzi ambao sasa anaujutia. “Nilifanya makosa kutokwenda El Merreikh ndio maana hata leo nilipofunga magoli ilibidi niombe msamaha kwa sababu Simba na Azam walitaka kunipeleka El Merreikh, Nilifanya kama kuwakosea na kwasababu nilikuwa naipenda Yanga ilibidi niichezee” Amesema Ngassa kwa hari ya uchungu ajijuta kosa alilofanya katika maisha yake la kukataa kwenda kucheza mpira wa kulip