Posts

Showing posts from June 11, 2014

SOMA JINSI WANAWAKE WANAVYO-SHAMBULIWA NA U.T.I

Image
U.T.I  kirefu chake ni Urinary Tract Infection ni maambukizi ya bakteria mbalimbali wanaoshambulia  mfumo wa mkojo, yaani kwenye figo (kidney), kibofu cha mkojo na mifereji inayotoa mkojo (urethra) Mifereji inayotoa mkojo kwenye figo (ureter) na mfereji unaotoa mkojo nje, mara nyingi bakteria hushambulia sehemu za chini za mfumo wa mkojo yaani urinary bladder na kitaalamu kuitwa bladder infection. Bakteria hao baada ya kumuingia binadamu hupona mara moja  pindi mgonjwa anapoanza dozi lakini kama wadudu hawa hawatatibiwa vizuri wanaweza kupanda na kushambulia figo na mshipa unaounga sehemu hiyo uitwao renal pelvis na kuleta madhara makubwa, hivyo kusababisha ugonjwa wa figo. Kuna wadudu wanaotoka kwenye utumbo mkubwa wa binadamu ambao kila binadamu anaishi nao, hawa husaidia kulinda mwili na kitaalamu hujulikana kama  normal flora na huwa ni askari wa mwili. Vijidudu hivyo hushuka hadi kwenye mlango wa  haja kubwa na kuenea mpaka sehemu za s

MAJAMBAZI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KIMANZICHANA NA KUUA ASKARI

Image
Mnamo tarehe 11/06/14 majira ya 0100hrs huko kituo kidogo cha Kimanzichana Pwani,watu wasiojulikana waliojifanya kuwa ni raia wema waliingia kituo kidogo cha Polisi Kimanzi Chana huku wakikimbia wakiwa na silaha za jadi kiasi cha askari wa zamu kuamini kuwa ni watu wanaohitaji msaada.  Cha kushangaza watu hao walimvamia askari mwenye silaha ambaye amefahamika kwa jina la JOSEPH NGONYANI na kuanza kumkatakata mapanga na hatimaye kupora silaha aina ya SMG ikiwa na risasi 30. Ndipo walipoanza kushambulia kwa risasi askari wengine na kufanikiwa kupora SMG ya pili na risasi 30. Hatimaye watu hao wakapora risasi za akiba 41 na kutoweka kusikojulikana. Askari Ngonyani alifariki dunia alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye hospitali ya wilaya ya Mkuranga. Askari mwingine aitwaye VENANCE amejeruhiwa mgongoni kwa risasi ambayo bado imo ndani, na kwenye paja la mguu wa kulia. Mgambo Mariam alijeruhiwa kichwani, shingoni na kuvimba bega kutokana na kupigwa sana mateke na kujeru

KITUKO CHA LEO BUNGENI: MH. LUGOLA ATINGA NA BANGO LA KUOMBA KURA BUNGENI DODOMA LEO.

Image
 Mh. Lugola baada ya kuingia Bungeni akiwa amevalia bango la kuomba Kura kwa wabunge wenzake  Mh . Lugola akiwa anavua bango lake Baada ya Mbunge Mh. Mchungaji Msigwa kuomba muongozo wa Mh. Spika na kuamuliwa avue bango hilo   Mh. Lugola baada ya kuvua bango hilo na kuendelea na kuomba Kura. Picha zote na Dodoma yetu Blog

MDADA ALIYEONEKANA KATIKA PICHA NA KOMBA AFUNGUKA, AZIMIA

Image
SIKU  chache zimekatika baada ya tukio la kusambaa mitandaoni kwa picha tata zenye pozi kati ya mheshimiwa Komba na mrembo aliyejulikana kwa jina moja la Angel.   Angel Kissanga, mkazi wa Kinondoni jijini Dar anayedaiwa kupiga picha tata na mheshimiwa Komba. Hatimaye mrembo huyo ameibuka na kuanika mambo mazito kama si makubwa, Risasi Mchanganyiko linakudadavulia. Awali katika gazeti hili toleo la Jumamosi iliyopita ukurasa wa mbele kulikuwa na habari hiyo ikiwa na kichwa; KHAA! KOMBA! Katika habari hiyo picha zilizomuonesha mheshimiwa Komba akiwa na mrembo huyo zilipamba ukurasa huku mwenyewe (Komba) akidai ni picha za kutengeneza). OFM YAINGIA MITAANI Kwa vile Komba alikataa picha si zake huku baadhi ya vyombo vya dola kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) vikitangaza kuingia kazini kumtafuta sosi wa picha hizo, ilibidi timu makini ya Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ kutoka Global Publishers iingie kazini kumsaka mrembo huyo kwa udi na u

Kiongozi wa kiislamu aliyeuwawa Kenya.

Image
Kiongozi wa wahubiri wa kiislam nchini Kenya ameuawa kwa kupigwa risasi katika mji wa mwambao wa Mombasa, yakiwa ni mauaji ya hivi karibuni.Sheikh Mohammed Idris, mwenyekiti wa Baraza la Maimamu na Wahubiri wa Kenya, ameuawa karibu na msikiti uliopo karibu na nyumbani kwake na kundi la vijana wenye silaha.Taatifa zinasema kuwa hapo awali amekuwa akipata vitisho kutoka kwa baadhi vijana wa kiislam na kuhofia maisha yake.Waislam kadhaa maarufu wenye msimamo mkali wamekua wakiuawa kwa kupigwa risasi katika hali isiyoelezeka miaka ya hivi karibuni. Wengine walikuwa wakituhumiwa kuwa ni viungo wa kundi la kiislam la Al-Shabab la nchini Somalia ambapo wafuasi wao wamekua wakiishutumu serikali kuhusika na mauaji hayo, shutuma ambazo mamlaka imezikataa.Hivi karibuni Idris, alilitaka jeshi la polisi kupambana na vikundi vyenye muelekeo wa kijeshi katika msikiti wake, na kupelekea wengine kumuona kama msaliti.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 11.06.2014.

Image
n       MAGAZETI YA UDAKU LEO MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

JIJI LA MBEYA LAWEKA HISTORIA YA KUZINDUA LIFTI YA KWANZA JIJINI HUMO

Image
Hapa Lift ikiwa imezinduliwa Rasmi kwa ajili ya matumizi Mdau Geofley Ananiah akiwa katika uzindunduzi huo  Jengo la Chama cha walimu Baadhi ya watu wakiwa wanaingia katika Lift hiyo kwa ajili ya uzinduzi huo.Chanzo Mbeya Yetu Blog