Posts

Showing posts from November 10, 2016

Mwili wa Samuel Sitta Ulivyopokelewa Uwanja wa Ndege Dar

Image
Mwili  wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samuel Sitta umewasili jioni hii katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam ukitokea nchini  Ujerumani ambako alikuwa akitibiwa hadi mauti yalipomfika.  Mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege mwili wa Marehemu Sitta utapelekwa nyumbani kwake Msasani, Dar es Salaam.

RAIS DKT MAGUFULI ATEMBELEA WAGONJWA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

Image
 Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimjulia hali mke wake, Mama Janeth Magufuli, ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016  Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimjulia hali mke wake, Mama Janeth Magufuli, ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016.  : Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimjulia hali Waziri wa Zamani Balozi Ramadhani Mapuri ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016.   Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwashukuru na kuwapongeza kwa kazi nzuri baadhi ya madaktari na wauguzi kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Tai

Rais Magufuli Amlilia Mungai

Image
RAIS wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John  Pombe Magufuli leo amemlilia aliyewahi kuwa waziri katika awamu zote nne za uongozi nchini, Marehemu Joseph Mungai ambaye mwili wake umeagwa leo katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Rais Magufuli akiwaongoza Watanzania katika kuuaga mwili wa Mungai, alishindwa kuficha hisia zake wakati wa kuaga mwili wa marehemu na kutokwa na machozi, jambo lililopelekea kutoa kitambaa cha mkononi na kujifuta. Mbali na rais,  wengine walioshindwa kujizuia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Lawrence Masha na viongozi wengine. Viongozi wengine waliofika kuuaga mwili wa Mungai ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa, Makamu wa Rais Mstaafu, Dk. Ghalib Bilal, Mama Salma Kikwete, Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Daniel Lubuva, Jaji Joseph Warioba, Mzee Kingunge, Mzee John Cheyo, Steven Wassira, Spik

Moto Wateketeza Godauni la Matairi Mikocheni Dar

Image
DAR ES SALAAM: Moto mkubwa ambao mpaka sasa bado unawaka umeteketeza godauni la  kuhifadhia matairi la Kampuni ya 7 General linalomilikiwa na Wahindi lililopo karibu na Chuo Kikuu cha Tumaini eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam. Tovuti hii imefanikiwa kufanya mahojiano na mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo aitwaye Shaban Salum ambaye ameeleza kuwa chanzo cha moto huo mkubwa na wa aina yake ambao unaonekana ni vigumu kuuzima ni shoti ya umeme. Timu ya Kikosi cha Zimamoto imewahi kufika eneo la tukio ikiwa na magari takribani matano na kufanya juhudi za kuuzima moto huo lakini hawajafanikiwa. Mpaka sasa maji yameisha na magari mengine yamefuata maji mengine kwa ajili ya kuendelea na zoezi la uzimaji. Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda yupo eneo la tukio ili kuona jinsi ya kuongeza nguvu katika zoezi la uokoaji mali pamoja na kuzima moto huo. PICHA ZOTE NA HILALY DAUD / GPL