Posts

Showing posts from August 17, 2013

HUYU NI BINADAMU ALIYETAJIRIKA KUFUATIA KUJIBADILISHA MWILI WAKE NA KUWA KAMA MJUSI HUKO KWA WENZETU.

Image
Jina alilopewa na wazazi wake ni Erik Sprague, ing awa Ulimwengu unamfaham kama Lizardman, huku akiwa na vipindi zaidi vya Television kibao akionesha jinsi alivyoweza kuubadilisha mwili wake huo.   Mabadiliko hayo yanajumuisha kuchonga meno na kuwa makali, Tattoo mwili mzima ikiwa ya rangi ya kijani na magamba, Ulimi kupasuliwa kati na kuwa pacha, Manundu maalumu usoni na hivi karibuni hadi midomo yake imekuwa ya kijani yote.   Kumekuwa na Uvumi kwamba huenda nyota huyo wa moenesho ya vipindi mbali mbali vya kutisha angefanya mpango aoteshwe mkia, lakini mwenyewe amekanusha na kusema jambo hilo haliwezekani. Mbali na shows kibao amekuwa mwandishi mzuri wa jinsi ya kuubadilisha mwonekano mwa mwili kupitia Body Transformation E-Zine   Lizard Skynyrd ndo jina la Bendi yake ambayo imekuwa ikizunguka sehemu tofauti tofauti duniani kwa matamasha mbali mbali. CHANZO http://www.folclassic.com

MWANARIADHA WA UGANDA STEPHEN KIPROTICH AFANYA KWELI HUKO MOSCOW

Image
2012 Olympic Gold Medalist and now the #IAAF World Chapion; Stephen Kiprotich in pictures during the #IAAF World championships men's marathon race in Moscow today.

AVUNJA REKODI YA KUWA BINADAMU MWEUSI ZAIDI DUNIANI !.

Image
INASEMEKANA huyu mwanadada ndiye aliyevunja rekodi ya watu weusi duniani maana maranyingi watu walisubiri atabasamu ili waamini kwam ba ni mwanadamu, Meno ndio yalimtambulisha kwamba ni mtu  Yani amemfatilia dada huyu hadi kugundua kwamba kuna kampuni mpya ya kutengeneza vipodozi iliobuni krimu ya kujichubua na kumbadilisha mwanadada huyu ngozi yake kuwa nyeusi . Hii ilikua ni katika majaribio ya kujaribu mafuta hayo kama yanaweza au laa ?. Ndugu msomaji wangu huwezi amini mlimbwende huyu ni mzungu lakini sasahivi du !.  Haya sasa kwa wakina dada watakaohitaji mkorogo huu bomba wa kukufanya uwe black beauty Endelea kutembelea masai nyotambofu blog siku sio nyingi utakuta tangazo la vipodozi hivyo !.  TUNZA RANGI YAKO IKUTUNZEE

WAISLAMU MSIKITI WA MTAMBANI 'WAMTEKA' ASKARI POLISI

Image
Baadhi ya waumini wa Kiislamu Msikiti wa Mtambani wakiwa wamemzunguka askari Polisi, Jonathan Tossi (katikati aliyeshika kamera) wakimuhoji baada ya kumshikilia kwa muda, hata hivyo walimuachia kwa masharti ya kumtaka afute picha zote alizopiga eneo hilo. Askari Polisi wakizunguka doria eneo la Msikiti wa Mtambani jijini Dar es Salaam kuhakikisha kuna amani.

POLISI FEKI AJITETEA......ADAI KUWA NJAA NDO ILIMFANYA AJIFANYE TRAFFIC

Image
MKANDA mzima wa askari bandia wa Kikosi cha Usalama Barabarani (trafiki), James Juma Hussein (45)  aliyekamatwa saa 1:30 asubuhi ya Agosti, 14, 2013 maeneo ya Tabata Kinyerezi Mnara wa Voda, jijini Dar es Salaam akiwa ndani ya sare zake za kazi, umepatikana....   Kwa nini James alikamatwa? Asubuhi hiyo, afisa mmoja wa trafiki mwenye cheo cha ukaguzi alikuwa akipita eneo hilo kwenda kazini, alipomwona James alisimamisha gari, akashuka kwenda kumsalimia.  Lakini alishangaa kuviona vifungo vya shati lake ni vya kawaida (vya polisi vinatakiwa kuandikwa police force yaani ‘jeshi la polisi’), akamtilia shaka.    Afisa huyo Alimkamata ‘askari feki’ huyo  mkazi wa Kimara Matangini, Dar na kumfikisha kwenye Kituo cha Polisi Stakishari, wilayani Ilala, Dar akafunguliwa jalada namba STK/RB/15305/2013 KUJIFANYA ASKARI ili taratibu za kisheria zichukuliwe juu yake. Ndani ya kituo cha polisi, James alihojiwa haya: Askari: Wewe mtu wa wapi? James: Mnya