Posts

Showing posts from January 9, 2018

BREAKING NEWS: Rais Magufuli afanya mazungumzo na Lowassa Ikulu

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 09 Januari, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, Ikulu Jijini Dar es Salaam. Baada ya mazungumzo hayo Mhe. Edward Ngoyai Lowassa amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya na ametaja baadhi ya maeneo ambayo kazi kubwa imefanyika kuwa ni kutoa elimu bila malipo, ujenzi wa mradi wa uzalishaji wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge), ujenzi wa viwanda na ujenzi wa reli kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) ambavyo vinazalisha ajira nyingi kwa Watanzania. “Nimepata faraja sana kuja hapa Ikulu kuonana na Mhe. Rais, tumezungumza nae na nimempongeza kwa kazi nzuri anayoifanya, lazima tukiri anafanya kazi nzuri na anahitaji kutiwa moyo. “Moja kubwa ambalo ni la msingi sana ni la kujenga ajira, katika kuanza ujenzi wa reli ya kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro hapo anajenga ajira, na kwenye nchi yoyote ina

Chid Benz Adakwa na ‘Unga’

Image
NGULI WA wa Hip Hop nchini Rashid Makwiro ‘Chid Benz anashikiliwa tena  na jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya na hii inakuwa mara ya tatu kwa msanii huyu kukumbwa na sakata hili. Akithibitisha taarifa hizo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, SACP, Giless Muroto amesema kwamba ni kweli msanii huyo alikamatwa na taarifa kamili zitatolewa hapo kesho. Kamanda Muroto amesema; “ Ni kweli Chidi Benz mnamo Desemba 30, 2017, tulimkamata akiwa yeye na mke wake na vijana wawili. Tumemkamata akiwa na dawa za kulevya zidhaniwayo kuwa ni Heroine. jalada lake lipo tayari kwa Mwanasheria wa wa serikali linafanyiwa uchunguzi na muda wowote watapelekwa mahakamani “ Aidha ameongza kuwa watuhumiwa wote bado wako mahabusu.

Hizi ndizo sababu nyimbo za Lady Jaydee kutochezwa Clouds

Image
Lady Jaydee ameeleza kuhusu nyimbo zake kushindwa kuchezwa Clouds Media wakati ilionekana tayari wameshamaliza bifu lao. Akiongea na Dizzim Online msanii huyo amesema, hajawahi kukataza nyimbo zake kuchezwa na kituo hicho hata hivyo walisharuhusiwa na Seven lakini hakuna kilichofanyika. “Ilisemekana kuwa mimi ndio nilikataza nyimbo zangu kupigwa, jambo ambalo sio kweli. Mimi sikukataza nyimbo zangu kupigwa na hakuna sehemu yoyote niliyoandika nyimbo zangu zisipigwe, wao ndio waliamua kwa sababu kuongea kwangu kule kwamba nyimbo zisipigwe. Baada ya hapo walisema akitoa ruhusa nyimbo zake zipigwe zitapigwa. Seven aliongea na akatoa Go ahead je walipiga? Kwa hiyo hapo sio tatizo langu mimi, hapo inadhihirika wazi kabisa kuwa tatizo liko wapi na mtu anaweza kuongea kitu sio kwa kumaanisha,” amesema Jide. Mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka 2016 Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba alipokuwa akiongea na kipindi cha XXL alisema

Kumbe aliyejiunganishia bomba la mafuta ni mstaafu wa Tazama

Image
Aliyejiunganishia bomba la mafuta nyumbani kwake Samwel Kilanglani(63) amejulikana kuwa ni mfanyakazi mstaafu wa bomba la kusafirisha mafuta Tanzania na Zambi (Tazama). Kilanglani anatuhumiwa kutoboa bomba la mafuta ya dizeli la Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) na kujiunganishia kwenye mantaki mawili yakiwa ndani ya nyumba yake iliyopo Tungi Kigamboni. Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, Kaimu Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amesema mtuhumiwa huyo alijiunganishia na bomba la TPA kwa njia ya kuchomelea na kuunganisha moja kwa moja kwenye mantaki yake mawili yaliyochimbiwa chini ndani ya nyumba yake. Kitalika amesema mtuhumiwa alijiunganishia katikati na bomba kuu hivyo mafuta yanapopelekwa sehemu husika mengine yanaingia kwake hivyo hayafiki kama yalivyokusudiwa. "Mafuta yanaweza yakapelekwa lita 4,000 sehemu husika lakini hayafiki yote mengine yanaenda kwa mtuhumiwa huyu matokeo yake wanajiuliza haya mengine yameenda wapi,&

Muslim Hassanali Ajiunga CCM Akitokea Chadema

Image
Muslim Hassanali, aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Ilala 2015. ALIYEKUWA mgombea ubunge Jimbo la Ilala kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu wa 2015, Muslim Hassanali, amejiunga na Chama Cha Mapinduzi  (CCM)  na kupokelewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula na viongozi wengine wa CCM katika ukumbi wa Checkpoint Pugu jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula (katikati)akiwa na viongozi wengine. Kujiunga kwa Hassanali ni mwendelezo wa mfululizo wa viongozi wa upinzani wakiwemo wabunge na madiwani kuondoka na kwenda CCM. Muslim Hassanali (kushoto) akirudisha fomu ya kugombea ubunge Jimbo la Ilala kwa tiketi ya Chadema katika uchaguzi mkuu wa  2015. Viongozi kadhaa wakiwemo wabunge na wapinzani wamejiunga na CCM wakitokea upinzani kwa sababu mbalimbali  ikiwemo ya kuunga mkono serikali ya Rais John Magufuli.

Siri 3 Dereva Wa Lissu Kutimkia…

Image
Simon Bakari akiongea na Freeman Aikaeli Mbowe. SIRI tatu za dereva wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), Simon Bakari (pichani) kwenda Ubelgiji na bosi wake zimevuja. Mbunge mmoja ndani ya chama hicho aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini kwa kuwa siyo msemaji wa chama wala familia, alisema kamati maalum inayoratibu matibabu ya Lissu iliyokutana jijini Nairobi, Kenya iliona ni vema Simon aongozane na bosi wake pamoja na mkewe mbunge huyo, Alicia kwa kuwa ndiye aliyefanya kazi kubwa ya kumuuguza akiwa Nairobi akisaidiana na Mkuu wa Idara ya Uenezi, Hemedi Ali. Tundu Lissu (Chadema). “Pamoja na ukweli kwamba dereva Simon alikuwa ana matatizo ya kisaikolojia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana akiwa na Lissu mkoani Dodoma Septemba 7, mwaka jana, alijitahidi kutoa huduma zisizo za kitabibu pamoja na Hemedi (Mkuu wa Idara ya Habari na Uenezi, Chadema) Nairobi ndiyo maana kamati maalum ya kuratibu tiba ya mbunge huyo ikaona ni vema

Mfungwa afufuka akiwa mochwari

Image
Mfungwa mmoja amezinduka na kujikuta yupo kwenye chumba cha kuhifadhia maiti baada ya madaktari watatu kuthibitisha kuwa alikuwa amefariki, vyombo vya habari Uhispania vimetoa taarifa hiyo. Gonzalo Montoya Jiménez alikuwa ni mfungwa katika gereza Asturias na alizinduka saa chache  kabla ya kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kugundua chanzo cha kifo chake. Gonzalo yupoa chini ya uangalizi wa madaktari katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Oviedo. Mmoja wa ndugu zake ameliambia gazeti la La Voz de Asturias kwamba Gonzalo  “alikuwa amewekewa alama ya kufanyiwa upasuaji, tayari kupasuliwa”. Wataalamu wamesema hali hiyo inaitwa ‘catalepsy’ ni hali ambayo ishara muhimu za uhai hufifia kwenye mwili wa binadamu kiasi cha kutoweza kutambulika kama yupo hai.

Kingunge Ataka Kujua Hali ya Tundu Lissu

Image
Aliyekuwa mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu wa 2015 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Edward Lowassa (wa pili kushoto), akiwa na Mwenyekiti wa Chadema,  Freeman Mbowe,   wakimjulia hali  Kingunge Ngombale Mwiru aliyelazwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili. MWANASIASA mkongwe , Kingunge Ngombale Mwiru, ambaye amelazwa katika hospitali ya Muhimbili kufuatia kung’atwa na mbwa amemkumbuka na kutaka kujua haliya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, ambaye amesafirishwa kutoka hospitalini Nairobi, Kenya,  kwenda Ubelgiji kwa matibabu zaidi. Kigunge ameulizia hali ya Tundu Lissu baada ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa aliyekuwa amefuatana na Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,  Edward Lowassa,  walipomtembelea leo Januari 8, 2018 katika hospitali ya Muhimbili. “Vipi hali ya  Tundu Lissu? Nimeona mimi jinsi wanavyonifanyia hapa (madaktari),  nimewauliza mimi tu niliyeng’atwa na mbwa mnanifanyia hivi, je Lissu mmemfany