Posts

Showing posts from April 21, 2018

Zari Amlilia Masogange, Akumbuka SMS Zake

Image
Video vixen, Agness Gerald ‘Masogange’ enzi za uhai wake. MPENZI wa zamani wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ ametoa salamu za pole kufuatia kifo cha video vixen, Agness Gerald ‘Masogange’, kupitia akaunti yake ya Snapchat. Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’. Zari ameeleza kuwa Masogange alikuwa akimtafuta kupitia simu kila mwezi akimuulizia maendeleo ya watoto wake ingawa hawakuwa marafiki sana. Kupitia Mtandao wa Snapchat Zari ameandika; We were not friends as such but ever since you got my number you’ve been dropping me a text every month and i mean no month passed without you asking how are the kids. in peace sis.

Kipimo Cha Mimba Cha Nyumbani rahisi Kutumia

Image
       Kipimo cha mimba cha nyumbani ni rahisi sana kukitumia wewe mwenyewe kwa wakati wako ikiwa unajihisi umjamzito au kuhisi mwenzi wako ana ujauzito. Unachotakiwa kuwa nacho ni moja, Kipimo hichob‘Pregnancy Test’ ambacho kinapatikana katika maduka yote ya madawa ya Binadamu, na pili mkojo wa anahisiwa au kuhisi ana mimba. mara nyingi ni rahisi zaidi kupata majibu ya uhakika ukitumia mkojo wa kwanza kabisa asubuhi kisha uweka kwenye kikopo kidogo na kisha fuata maelekezo ya kwenye picha hii:- Hatua; 1.    Fungua pakiti iliyo na kipimo cha mimba. 2.    Tofautisha sehemu ya kushika na sehemu utakayotumbukiza kwenye kikopo chenye mkojo. 3.    Acha kwa dakika zipatazo 3, bila kuzidisha sehemu yenye mstari uliyoandikwa MAX. 4.     Toa na kisha soma majibu yaliotokea. Majibu yatatoka kama ilivyo katika picha hii inayofuata ya vipimo viwili tofauti vilivyofanyiwa majaribio:- 1.    Mistari miwili humaanisha ‘POSTIVE’ – Mimba imetunga.

Siri 6 Kiba Kumuoa Mkenya Zaanikwa!

Image
Ali Saleh Kiba ‘King Kiba akiwa na Mkewe Amina N YUMA ya tukio kubwa na la kihistoria kwenye ulimwengu wa burudani, lililogubikwa na kufuru ya fedha la staa wa Bongo Fleva wa Afrika Mashariki, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ kumuoa mrembo mkali kutoka Mombasa nchini Kenya, kuna siri sita (6), Risasi Jumamosi linazianika.  Juzi alfajiri ya Aprili 19, mwaka huu, Kiba alifunga ndoa na mrembo Amina Khaleef katika Msikiti wa Ummul Kulthum uliopo mjini Mombasa, Kenya. Ndoa hiyo ilifungishwa na Sheikh Mohamed Kagera. Hakika ilikuwa ni furaha, shangwe, nderemo na vifijo kwa maharusi hao, wanafamilia na mashabiki wa Kiba mjini Mombasa mara baada ya ndoa hiyo kufungwa. Mara baada ya kufungwa kwa ndoa hiyo, mitandaoni kulichafuka ambapo baadhi ya mashabiki wa Kiba walikuwa wakihoji ni kwa nini mkali huyo wa Wimbo wa Seduce Me ameacha warembo kibao Bongo na kwenda kwa Amina wa Mombasa? Kufuatia wengi kutaka kujua Amina ni nani au ana nini cha tofauti kilichomteka Kiba, R

Kajala amkimbiza mke wa P Funk

Image
   Muigizaji wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja amedaiwa kusababisha mke wa prodyuza mahiri Bongo, Paul Matthysse, Samira afungashe virago vyake tayari kwa kurudi kwao. Mke huyo wa P Funk amedaiwa kufikia uamuzi huo baada ya mwanaume huyo kuonekana kurudisha majeshi kiaina kwa Kajala aliyewahi kuwa mchumba’ke zamani huku picha na video mbalimbali za kimalovee zikivuja. Mtu wa karibu na mke wa P Funk alivujisha kuwa, Samira amefikia hatua hiyo baada ya kushuhudia matukio mbalimbali ya P Funk na Kajala na kukosa majibu yaliyonyooka. “Unajua P Funk kila alipokuwa akielezwa kuhusu Kajala alikuwa hanyooshi maelezo ingawa machoni alionesha kumpenda Kajala. “Mkewe ambaye kwa sasa ni mjamzito, ameishi kwenye kipindi kigumu sana. Anashindwa kumuelewa P Funk kwani watu kibao wanampigia na kumuambia wamemuona mumewe akiwa na Kajala,” alidai mtu huyo wa karibu. Akizidi kushusha data, mtu huyo wa karibu na Samira alidai kuwa, mara kadhaa P Funk amekuwa akielezwa kuh

TCRA Yaanza Rasmi Usajili wa Blogu, Redio na TV za Mtandaoni

Image
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetangaza kuanza rasmi zoezi la usajili wa wamiliki wa Blogu, Majukwaa ya Mtandaoni (Online Forums), Redio pamoja na Televisheni za mtandaoni kuanzia leo Jumamosi, Aprili 21, 2018 kwa mujibu wa sheria.

Masogange kuagwa Leaders, kuzikwa nyumbani kwa.

Image
Video queen maarufu Bongo Agnes Gerald maarufu Kama Masogange anatarajiwa kuzikwa nyumbani kwao jijini Mbeya ambako ndiko wazazi wake waliko. Akizungumza na www.eatv.tv dada wa Agnes anayejulikana kama Emma Gerald, amesema mwili wa Agnes  utaagwa jijini Dar es salaam kwenye viwanja vya Leaders,  na kisha kusafirishwa kuelekea mkoani Mbeya kwa mazishi “Tutaaga kesho asubuhi saa 3 pale Leaders, na kisha tutasafirisha kuelekea Mbeya kwa mazishi”, amesema Emma Gerald. Sambamba na  hilo muigizaji Steve Nyerere ambaye yuko karibu na familia ya Agnes amewataka wasanii kujitokeza kwa wingi leaders jioni ya leo, ili kujadili utaratibu wa mazishi na mengineyo. Agnes Masogange amefariki jana April 20, kwenye hospitali ya Mama Ngoma baada ya kulazwa kwa muda wa siku nne mpaka kifo kilipomkuta kwa tatizo la pneumonia