Posts

Showing posts from July 15, 2017

PICHA: KELVIN YONDANI APATA JIKO RASMI

Image
TAARIFA njema ikufikie popote ulipo kuhusu beki kisiki wa  Yanga, Kelvin Patrick Yondani  ambaye ameamua kuachana na ukapera. Mkali huyo alianza kwa  Send Off  kisha akamalizia mambo na mzazi mwenzake ambaye ameishi naye miaka mingi. Yondani anaingia kwenye orodha moja na wanasoka kama Emmanuel Okwi, Ibrahim Ajib, Mwinyi Kazimoto ambao ni wanacheza Ligi Kuu Tanzania Bara. Hongera Yondani kwa kuamua kufanya kweli.

Wanafunzi 10 wafutiwa matokeo ( Kidato cha sita) kwa Udanganyifu

Image
Wanafunzi 10 wamefutiwa matokeo yao baada ya kufanya udanganyifu kwenye mtihani wa Kidato cha sita  Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa Necta Dk Charles Msonde  amesema  kuwa kati ya watahiniwa hao kumi, saba ni wa shule na watatu ni wa kujitegemea.  Pamoja na hao kumi, matokeo ya watahiniwa wengine 15 yalizuiliwa kwa kuwa hawakufanya mitihani ya baadhi ya masomo.  Watahiniwa hao walishindwa kufanya mitihani kutokana na matatizo mbalimbali ikiwamo ya kiafya na hivyo kushindwa kufanya baadhi ya mitihani hiyo. ‘Watahiniwa hao wamepewa fursa ya kufanya mitihani ya kidato cha sita, Mei 2018 kama wa watahiniwa wa shule,” imesema taarifa ya Dk Msonde. Pia, wapo watahiniwa 69 wa shule ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mitihani yote, wamepewa fursa ya kufanya mitihani hiyo, Mei 2018. Wanafunzi 10 wamefutiwa matokeo yao baada ya kufanya udanganyifu kwenye mtihani wa Kidato cha sita  Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani

Simba Kuna Makinikia - Wazee Simba

Image
Wazee wa Klabu ya Simba wametuhumu uongozi wa Klabu hiyo kikihuumu Klabu hicho na kwamba wamemtaka rais John Magufuli kuingilia kati hujma hizo. Wakizungumza na Waandishi wa habari leo wazee hao wameeleza kuwa hujuma hizo zinatokana na Uchu wa madaraka na tamaa ya fedha kwa viongozi hao. Felex Makuwa Mratibu wa wazee hao ameeleza kuwa Serikali kupitia Mamlaka zake iwakamate wahusika na Iwachukulie hatua  

BREAKING NEWS : ANGALIA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA ACSEE 2017

Image
  Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokoe ya mtihani wa kuhitimu elimu ya sekondari kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita. Bonyeza HAPA kufatilia matokea ya shule zote Tanzania. BOFYA HAPA KUYAONA

Profesa Jay Afunguka Wema Kukacha Harusi Yake

Image
Mbunge wa Mikumi kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Haule ‘Profesa Jay’akifanya yake na mke wake Grace Mgonjo baada ya kufunga ndoa. BAADA ya Jumamosi iliyopita Mbunge wa Mikumi kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Haule ‘Profesa Jay’ kufunga ndoa na mchumba’ke wa kitambo, Grace Mgonjo katika Kanisa la Mtakatifu Joseph lililopo Posta jijini Dar na sherehe kufanyika ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, ameibuka na kufunguka suala la Miss Tanzania 2006/07, Wema Sepetu kuikacha harusi yake. Staa wa Bongo, Wema Sepetu. Taarifa za awali kutoka kwa chanzo makini zilieleza kuwa, Profesa Jay na Wema ambaye alihamia Chadema miezi kadhaa iliyopita wana bifu kali japokuwa haijulikani chanzo ni nini, ndiyo maana mwanadada huyo hakuhudhuria kwenye harusi hiyo. “Unajua Wema na Jay hawana uhusiano mzuri tangu ahamie kwenye chama hicho yaani wana bifu ndiyo sababu hata Wema hakuhudhuria kwenye sherehe ya harusi ya Jay

CHAI, KARANGA NA MTINDI KWA HESHIMA YA NDOA!

Image
WAPENDWA wasomaji wangu, bila shaka mko poa mnaendelea vyema na majukumu yenu kama kawaida. Leo kwenye safu hii nitazungumzia umuhimu wa chai kwa mwanamke ili kudumisha uhusiano wako na ndoa kwa ujumla. Nafanya hivi kwa kuwa, wengi wamejikuta wakipoteza ndoa zao kwa kupoteza mvuto na kupuuzia mambo madogomadogo. Sasa leo nakupa tipu juu ya namna chai ya rangi, maziwa ya mtindi, karanga na supu ya pweza vinavyoweza kuinogesha ndoa yako hasa katika eneo la faragha. Mwanamke fanya hivi; kunywa chai kutwa mara tatu. Kumbuka kazi ya chai ni kukupatia joto mwilini. Ukijua kuwa muda wa kukutana na mwenza wako faragha unakaribia, pata kikombe chako cha chai ya moto kisha jirushe uwanjani uone mechi itakavyokuwa bomba. Chai hiyo itakupa nguvu na hivyo kuweza kumudu mikikimikiki ya mwenza wako. Na nikuambie tu kwamba, ukiwa umepata chai yako hiyo, neno; ‘nimechoka mume wangu’ haliwezi kuwepo, labda achoke yeye. Unaachaje sasa kuitumia chai ambayo hata haina kazi kuiandaa