Posts

Showing posts from August 31, 2017

Mahakama imeelezwa Sethi wa IPTL Amewekwa Puto Tumboni

Image
Upande wa utetezi umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Singh Sethi amewekewa ‘Puto’ tumboni kutokana na ugonjwa unaomkabili hivyo asipohudumiwa inavyotakiwa anaweza kupoteza maisha. Mbali ya Seth, mwingine ni Mfanyabiashara James Rugemarila ambapo kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12, yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya TSh 309,461,300,158. Wakili wa utetezi, Joseph Mwakandege amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa mteja wake Seth anatakiwa apelekwe Hospital ya Taifa Muhimbili lakini hadi sasa hajapelekwa na ni dhahiri upande wa mashtaka umedharau amri mbili za Mahakama. ”Ugonjwa uliosababisha Seth atakiwe kwenda Muhimbili ni baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa ambapo tumboni kwake kumewekwa Balloon ‘Puto’ hivyo asipohudumiwa ipasavyo inaweza kusababisha kifo, naomba mshtakiwa apelekwe Muhimbili kwa sababu ni Hospitali ya juu na yenye vifaa na watalaamu wa kuto

Hakimu Akataa Msokoto wa Bangi Kesi ya Wema

Image
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imekataa kupokea ushahidi wa msokoto wa bangi na vipisi viwili vya madawa hayo ya kulevya katika kesi inayomkabili mwigizaji Wema Sepetu . Uamuzi huo umetolewa na Hakimu, Thomas Simba , aliyesema mahakama haiwezi kupokea vielelezo hivyo kwa sababu msokoto wa bangi na vipisi vina kasoro kwa kuwa shahidi hakuvifafanua mahakamani. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 12 mwaka huu.

Serikali yataifisha magari yaliyoingizwa nchini kinyume na sheria

Image
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetaifisha jumla ya magari sita yakiwepo magari matatu aina ya Ranger Rover Sports yaliyoingizwa nchini kinyume na sheria baada ya watuhumiwa hao kukiri kuwa wamefanya kosa hilo. Rais Magufuli mwezi Machi mwaka huu alipokwenda bandarini alikuta kuna makontena yenye magari ndani yake huku wamiliki wa makontena hayo wakidai  makontena hayo yalikuwa na nguo na mabegi  lakini baada ya kufunguliwa zilionekana gari za kifahari zikiwa kwenye makontena hayo, jambo ambalo lilionekana wamiliki wa mahari hayo walikuwa wakiingiza magari hayo kinyume na utaratibu na sheria za nchi. Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, DPP Biswalo Mganga amesema kuwa baada ya mahakama kuwakuta na hatia raia hao wakigeni ambao walidai kuwa kontena hizo zilikuwa na nguo na mabegi wakati ni magari hivyo serikali imetaifisha magari yao na sasa kuwa magari ya serikali. "Rais hao wamekiri makosa yao yote mawili na kutokana na kukiri kwao mahakama ime

‘Masogange’ Ana Kesi ya Kujibu Dawa za Kulevya

Image
Video Queen, Agnes Gerald ‘Masogang aliyevaa gauni la kijani aikitoka mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema kuwa Video Queen , Agnes Gerald ‘Masogange’, anayo kesi ya kujibu kwa kudaiwa kutumia dawa za kulevya, hivyo anapaswa kujitetea. Kesi hiyo ambayo imeunguruma leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, amesema kuwa amekubaliana na hoja za ushahidi wa upande wa mashtaka ambapo mshtakiwa amekutwa na kesi ya kujibu na hivyo ana haki ya kujitetea. Baada ya kauli ya hakimu huyo, Masogange amesema atajitetea kwa njia ya kiapo na atakuwa na mashahidi watatu. Hakimu Mashauri ameiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 12, mwaka huu ambapo mtuhumiwa ataanza kujitetea. NA DENIS MTIMA/GPL

Ridhiwani Kikwete Amvaa Kigwangala

Image
 Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amemvaa Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Khamis Kigwangala na kumwambia anaweza kuwa sehemu ya wachochezi kwa anachokifanya. Ridhiwani Kikwete amebainisha hayo kupitia ukurasa wake wa twitter baada ya  Mhe. Kigwangalla kuonyesha kusikitishwa na kitendo kilichofanywa na Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma katika kuwafanyia usaili baadhi ya wataalamu waliojitokeza kwenye usaili  wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambao umefanyika mapema leo Agosti 30, 2017. "Unaweza dhani unauliza swali kumbe nawe unakuwa sehemu ya wachochezi! Mhe. Waziri unaweza kuwa hujui kusoma lakini picha inatoa jibu sahihi", aliandika Ridhiwani. Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma leo Agosti 30, 2017 ilifanya usaili kwa ajili ya nafasi za kazi katika Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ambapo takribani watu 30,000 walijitokeza huku ikiwa watu 400 pekee ndiyo wanaotakiwa.

Zijue faida za uaminifu katika mahusiano ya Ndoa

Image
Suala la uaminifu katika mapenzi kwa karne hii limekuwa kikwazo kikubwa kwa watu wengi sana, wengi wemekuwa si waaminifu wakati mwingine kupelekea mahusiano hayo kufa. Hivyo uaminifu ni muhimu sana katika mapenzi kwa kuwa katika mahusiano ya kimapenzi kuna faida nyingi kwa mwili na akili. Watu walio katika mahusiano bora ya mapenzi huishi maisha marefu na kufurahia afya njema kuliko wale wasiokuwa katika mahusiano ya aina hiyo. Faida hii haina pingamizi kwa sababu ya ukweli kwamba watu wanaokuwa katika mahusiano ya karibu wanajijengea hisia na nguvu fulani ambayo huwasaidia kusaidiana na kujaliana wakati wa shida. Siyo tu kwamba watu walioko katika mahusiano ya aina hii wanaishi muda mrefu lakini pia ni kweli kwamba wanakuwa na furaha na wanaridhika na maisha kuliko wale wanaoshindwa kukaa katika mahusiano. Pili, kuwa katika mahusiano mazuri ya mapenzi kunasaidia katika mambo mbalimbali ya kimahitaji. Kusaidiana katika mahitaji mbalimbali baina ya wapenzi ni nji

Mobeto Ampukutisha Zari

Image
Hamisa Mobeto. DAR ES SALAAM: Mwanamitindo Hamisa Mobeto amedaiwa kuwa sehemu ya kupungua mwili kwa mwanadada mjasiriamali maarufu, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’. Kwa mujibu wa chanzo makini, tangu Mobeto aanze kuibua mjadala mtandaoni kuhusiana na mtoto wake kudaiwa kuwa ni wa bwana wa Zari, mjasiriamali huyo amejikuta akipungua mwili kutokana na mawazo aliyonayo. “Zari kapungua mwili kweli jamani. Mobeto amemponza. Amemsababishia watu wamtukane sana Zari kiasi ambacho amekosa amani kabisa. Masikini mtoto wa watu kakonda kweli sasa hivi. Zari. “Ukitazama picha za Zari sasa hivi si Zari yule aliyetoka kujifungua. Tena kwa kawaida tunajua mtu ukitoka kujifungua unanenepa lakini kwa Zari mambo yamekuwa tofauti. Ngoja niwatumie picha yake ya sasa muone,” kilisema chanzo. Hata hivyo mwanahabari wetu aliingia kwenye ukurasa wa Instagram wa Zari na kujionea jinsi alivyopungua baada ya kuona picha zake mpya na kulinganisha na picha zake za zamani. Lic