Posts

Showing posts from June 13, 2018

Ujenzi wa kituo cha Afya Dongobesh awamu ya pili waendelea kutekelezwa kwa zaidi ya aslimia 80- Mbulu

Image
muonekano wa jengo la wodi ya mama na mtoto kituo cha Afya Dongobesh likiwa katika hatua ya ukamilishaji Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu inategemea kukamilisha ujenzi wa majengo matano ya kituo cha Afya Dongobesh ifikapo Juni 30 2018, hatua hii imefikiwa ikiwa ni utekelezaji wa   kiwango cha aslimia 80 kilichobainishwa baada ya kufanyika ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa kituo cha Afya Dongobesh,tathimini hiyo ilitolewa na   timu ya Wataalam toka Tamisemi, wakilishirikiana na wataalam toka   Mkoa wa Manyara .   Timu ya wataalam wakiwa katika moja ya majengo mapya ya kituo cha afya wakiendelea na ukaguzi. Timu hizo ziliweza kufanya ukuaguzi wa majengo hayo mapya yanayoendelea kukamilishwa kabla ya Mwezi Juni kukamilika ili kubaini kama   kiasi cha fedha Tsh.   Milioni 400   zilizotolewa   na Serikali ya awamu ya tano kwa ajili ya ujenzi wa majengo hayo unakamilika kwa wakati. Mgawao huo wa fedha uliotolewa ikiwa na mgawao awamu ya pili baada ya maeneo mbalimbali

Breaking News: Moto Mkubwa Waibuka Kariakoo

Image
Moto ukitekeleza ghorofa ya juu ya jengo hilo eneo la Kariakoo. MOTO mkubwa umeibuka Kariakoo katika mitaa ya Livingstone na Aggrey na unaendelea kuteketeza maduka. Tayari vikosi vya zimamoto vipo eneo la tukio kupambana na moto huo unaoendelea kuteketeza jengo la ghorofa ambalo lina maduka katika ghorofa ya chini. Moto huo ulianzia kwenye ghorofa ya kwanza katika jengo hilo lenye ghorofa mbili ambako kulikuwa na stoo ya vitu mbalimbali ambavyo vimeteketea kwa moto huo ambao moto huo ulielekea katika ghorofa ya juu. Chanzo cha moto huo hadi tunakwenda mitamboni kilikuwa hakijajulikana. Vikosi vya Zimamoto vikiendelea na kazi Wakazi wa Dar es Salaam wakishuhudia moto huo.

Je,wajua Rais Kim alisafiri na choo chake mpaka Singapore?

Image
Imebainika kuwa Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un alisafiri na choo chake maalumu wakati wa mkutano wake na Rais Trump nchini Singapore. Sababu ya Kiongozi huyo kusafiri na choo chake imetajwa kuwa ni kuzuia kinyesi cha Kiongozi huyo kufanyiwa upembuzi na watu wa usalama wa mataifa mengine. Aidha imeelezwa kuwa Kiongozi huyo amekuwa na tabia ya kutembea na choo chake kila mahala anapokwenda kwani huwa hapendi kutumia vyoo vya umma. Kwa upande mwingine Kiongozi huyo alibeba gari lake aina ya Limousine ambalo halipitishi risasi pamoja na chakula chake mpaka nchini Singapore.

Ukeketaji Manyara yaongoza

Image
Hali ya Ukeketaji mkoa wa Manyara imefikia asilimia 70.8 kutoka asilimia 58 mwaka jana,hali ambayo ni mbaya zaidi licha ya jitihada za serikali na Mashirika binafsi kutoa elimu juu ya madhara ya kufanya ukeketaji. Hali ya Ukeketaji katika mkoa wa Manyara bado ni tatizo kutokana na watoto wachanga pia kufanyiwa vitendo vya ukeketaji kwa siri pale wanapozaliwa. Anna Emmanuel Fisoo afisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Manyara anaeleza kuwa tatizo la ukeketaji kwa wanawake na watoto bado lipo katika maeneo mengi ya mkoa katika baadhi ya makabila ya wafugaji. Amesema ukatili mwingine wanaofanyiwa watoto ni ulawiti na kubakwa na kwamba kesi nyingi zipo Mahakamani. Amesema ili kutokomeza ukatili huo ni lazima jamii,taasisi za serikali na mashirika binafsi kila mmoja atimize wajibu wake kwa wakati na kwa kufanya hivyo hali hiyo itakuwa imepungua kwa asiliamia 50 ifikapo mwaka 2022. Paskalia Changala Mratibu wa shirika linalojishughulisha na masuala ya kutokomeza ukeke

Lynn: Kuolewa na Diamond Wala Sina Papara

Image
Irene Charles ‘Lynn’ VIDEO Queen Irene Charles ‘Lynn’ ambaye aliwahi kudaiwa kutoka kimapenzi na msanii wa muziki Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amesema ametulia na hana papara kwani kama Mungu amepanga aolewe na msanii huyo, lazima itokee! Akizungumza na Risasi Jumatano, Lynn alisema, hawezi kuleta drama kwenye mitandao kuhusiana na suala lake na Diamond ila anachojua yeye kama Mungu amepanga aolewe naye, itakuwa hivyo na kama siyo basi ataolewa na mwingine aliyepangiwa. “Unajua siku zote ndoa hupangwa na Mungu hivyo kama Dai (Diamond) alipangwa kuwa wangu basi atakuwa wala sina papara, kama hajapangwa kuwa wangu atakuja mwingine,” alisema Lynn.