Posts

Showing posts from July 11, 2016

Watu 3200 wakusanyika na kupigwa picha za utupu!

Image
          Sehemu ya umati wa watu 3,200 waliohudhuria tukio hilo. Hull, Uingereza WATU zaidi ya 3200 wamekusanyika na kusherehekea utamaduni wao wakiwa kwenye huku wakiwa wamevua nguo zao zote (utupu) katika Mji wa Hull, Uingereza ikiwa ni tukio la kusherehekea mji huo kama Mji wa Utamaduni. Katika tukio hilo lilitokea Jumamosi ambapo washiriki walijipaka miili yao rangi ya bluu-baharina kisha kupigwa picha wakiwa katika maeneo mashuhuri jijini humo kama sehemu ya mradi uliopewa jina Sea of Hull. Mradi huo unatekelezwa na mpiga picha Spencer Tunick na unadhaminiwa na taasisi ya Sanaa ya Ferens Art Gallery. Picha zilizopigwa siku ya tukio hilo, zitawekwa na kuoneshwa kwa umma wakati wa tamasha ya sanaa ya 2017 itakayoendelea kwa mwaka mmoja. Tunick, anayetoka New York, amewahi kupiga picha za watu wengi wakiwa uchi Sydney Opera House, Place des Arts mjini Montreal, Mexico City na mjini Munich nchini Ujerumani Germany. Bw Tunick amesema kazi zake “hu

URENO WAITANDIKA UFARANSA NA KUNYAKUA KOMBE A UERO 2016

Image
Usiku wa July 10 2016 wapenda soka duniani kote macho na masikio yao ilikuwa Paris Ufaransa kushuhudia fainali ya 51 ya michuano ya Euro, Paris ulichezwa mchezo wa fainali ya Euro 2016 kati ya timu ya taifa ya Ureno dhidi ya mwenyeji Ufaransaambaye mara ya mwisho kufungwa na Ureno ilikuwa April 26 1975. Huu ni mchezo ambao ulikuwa unachezwa lakini nafasi kubwa ya ushindi ilikuwa inapewaUfaransa kutokana na rekodi yake ya miaka 40 kutofungwa na Ureno, lakini pamoja na uwezo wao waliouonesha katika michuano ya Euro mwaka huu, Ureno matumaini yalipotea zaidi dakika ya 23 baada ya nahodha wao Cristiano Ronaldo kushindwa kuendelea na mchezo kwa kuumia. Mchezo ulikuwa mgumu licha ya Ufaransa kuongoza kwa kumiliki mpira kwa asilimia 54 kwa 46, dakika 90 zilimalizika kwa suluhu, hivyo refa akaongeza dakika 30 zilioenda kuimaliza Ufarasa, Ureno walifanikiwa kuibuka a ushindi wa goli 1-0, goli pekee ambalo lilifungwa na Eder Antonio dakika ya 109, Eder aliingia akitok