Posts

Showing posts from December 28, 2017

Polisi: Tutamkamata na Kumhoji Askofu Kakobe kwa Uchochezi

Image
Licha  ya kutokiri moja kwa moja juu ya taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusu kumkamata Askofu Zakaria Kakobe wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGFC) lililoko Mwenge jijini Dar es Salaam, Jeshi la Polisi limesema ni lazima litamhoji kiongozi huyo wa kiroho. Kuhojiwa huko kumetokana na kauli yake dhidi ya serikali aliyoitoa wakati wa ibada ya Krismasi. Jana, kulienea taarifa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kueleza kwamba askofu huyo alitiwa mbaroni jana asubuhi na askari wa Jeshi la Polisi huku sababu za kukamatwa zikielezwa kuwa ni ujumbe alioutoa wakati wa mahubiri yake ya ibada ya Krismasi. Akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na ukweli wa taarifa za kutiwa mbaroni kwa Askofu Kakobe, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alisema kuwa ni kweli walishakuwa katika harakati za kumkamata. “Ametoa maneno ya kashfa katika mahubiri yake, lakini sina taarifa kama amekamatwa,”  Kamanda Mambosasa alisema na kuongeza: “Taarifa

BABA MZAZI ,ALIYENASWA GESTI NA, MWANAYE WA KUMZAA KIMENUKA!

Image
Fadhil Mshamu, mkazi wa Kibaha mkoani hapa anakula Krismasi na Mwaka Mpya wa 2018, akiwa na stresi kufuatia kusomewa shitaka la kumdhalilisha binti yake wa kumzaa jina linahidhiwa kwa sababu za kimaadili. Kesi hiyo ilitajwa wiki iliyopita ambapo itaanza rasmi kusikilizwa mapema Mwezi Januari, mwakani katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani. Mshamu alikutwa na kasheshe hilo baada ya miezi kadhaa kunaswa akiwa na binti yake wa kumzaa kwenye nyumba moja ya kulala wageni (gesti) huko Kibaha huku kukiwa na madai ya kumtaka kingono. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Mshamu alinaswa akiwa na binti yake huyo baada ya kuwekewa mtego kufuatia taarifa za kumsumbua kwa muda mrefu akidaiwa kumtaka kimapenzi. Kwa mujibu wa chanzo chetu kutoka ndani ya familia ya Mshamu, baada ya kunaswa kwenye mtego huo uliowashirikisha polisi na ndugu wa familia hiyo, Juni 26, mwaka huu, Jeshi la Polisi lilimfungulia Mshamu jalada la uchunguzi ambalo lilipelekwa kwa Mwendesha Mas

Mkurugenzi Mtendaji CRDB Atangaza Kung’atuka

Image
MTENDAJI Mkuu wa CRDB Bank, Dr Charles Kimeo, leo ametangaza kustaaafu ifikapo Mei 2019. Dkt. Kimei aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kwamba hatua hiyo ni kwa ajili ya kuanzisha mchakato wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo kupata mtu atakayeshika nafasi yake kwa mujibu wa taratibu na kanuni zilizopo. Kabla ya kujiunga na benki hiyo, Dk Kimei alifanya kazi Benki Kuu ya Tanzania kama Mkurugenzi Mfawidhi wa Shughuli za Benki, Mkurugenzi wa Sera, Uchumi na Utafiti, Meneja wa Idara ya Utafiti wa Uchumi na Sera na nyadhifa nyingine mbalimbali katika Idara ya Utafiti. Hivi sasa ni Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki Mabenki nchini. Amewahi pia kufanya kazi katika bodi mbalimbali ikiwemo ya Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Mamlaka ya Elimu nchini, Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kampuni ya Huduma za Mikopo Midogo ya CRDB na tawi la CRDB nchini Burundi. Dkt. Kimei ana Shahada ya Uzamivu katika Uchumi aliyoipata Chuo Kikuu cha

Ikulu Haina Taarifa ya JPM Kushinda Tuzo ya Mandela

Image
IKIWA ni siku moja baada ya taarifa kusambaa mitandaoni kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. John Pombe Magufuli ametunikiwa Tuzo ya Amani ya Mandela (Mandela Peace Prize) huko nchini Afrika Kusini, huku kukikosekana taarifa rasmi kutoka kwa waandaaji wa tuzo hizo. Leo Alhamisi, Desemba 28, 2017 kupitia kipindi cha Joto la Asubuhi cha Radio  E-FM, Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Gerson Msigwa amesema kuwa hana taarifa yoyote juu ya tuzo hiyo. “Mimi sina taarifa zozote kwa sababu mtu anapotoa tuzo sio lazima awasiliane na mtu anayempa tuzo, wao wanakuwa na vigezo vyao kadri ya watu walivyowapima viongozi.“ amesema Msigwa. “Mimi sina information zozote kwa hiyo ni vizuri mngewatafuta hao Nelson Mandela wenyewe hicho chuo waweze kuwaeleza tuzo hizo taarifa wanakuwa nazo vyuo wenyewe,“ amesisitiza Msigwa. Hata hivyo tayari Wakfu wa Nelson Mandela nchini Afrika Kusini umebainisha kuwa haukuandaa, kusimamia wala kutoa tuzo

Mwanajeshi Apigwa Risasi na Mpenzi Wake, Afariki

Image
ASKARIwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika Kikosi cha Makambako (KJ 514) ambaye amefahamika kwa jina la Neema Masanja amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mchumba wake ambaye ni askari wa Jeshi la Polisi Makambako mkoani Njombe. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Prudensiana Protas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo mapema jana na kusema kuwa Askari wa jeshi la polisi Makambako mkoani Njombe ambaye anafahamika kwa jina la Zakayo Dotto alifanya tukio hilo la mauaji kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi. Jeshi la Polisi linaendelea na msako wa kumtafuta mtuhumiwa Zakayo Dotto ambaye baada ya kufanya tukio hilo la mauaji alikimbia kusikojulikana.

Wema: Tunajivunia Kumpata RC Mwenye Akili Nyingi

Image
QUEEN wa Bongo Movies, Wema Sepetu ambaye amerejea Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivi karibuni akitokea CHADEMA , amefunguka ya moyoni kuhusu utendaji mzuri wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda. Wema ambaye amekuwa karibu na RC Makonda tangu arejee CCM, amepost picha ya Makonda kupitia Instagram yake na kuandika ujumbe unaowataka wakazi wa Dar es Salaam kujivunia mkuu huyo kutokana na utendaji wake wa kazi. “Tanzania Kwanza. Katika vitu ambavyo Dar pia inatakiwa kujivunia ni kupata RC mwenye akili nyingi… Mungu akakutangulie katika kazi zako za lengo la kuijenga Tanzania yako izidi kuwa zaidi ya ilipo sasa,” aliandika Wema. Aliongeza, “Ipo siku wataelewa tu, The Man Himself… Call Him Mr Dar-es-salaam… Viva RC wangu…. Viva Rais wangu…. #UzalendoKwanza … cc @paulmakonda May everything you wish well for your Nation Be…. We support you fully,” Muigizaji huyo bado anakabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya baada ya kudaiwa kukutwa na msokoto wa bangi n