Posts

Showing posts from May 4, 2018

Rais Magufuli: Bora Kula Sumu Kuliko Fedha za Serikali

Image
Rais Magufuli leo Ijumaa ameweka jiwe la msingi la Barabara ya Kidatu – Ifakara. Sherehe hizo zimehudhuriwa na Wabunge wote wa Chadema na CCM mkoani Morogoro. Moja ya kauli ambazo Rais amezungumza leo; “Kuna maeneo ambayo wakandarasi wamekula hela za miradi, wamekula sumu. Hela ya Serikali ya awamu ya tano hailiwi bora ule sumu kali. Waliokula fedha waanze kujiandaa, kurudisha fedha na kutekeleza miradi au kukumbana na sheria ya mwaka 97.” “Haiwezekani mimi nitafute hela halafu wewe uzile tu nikwambie umeula wa chuya. Kama makandarasi watakuwa wamekimbia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, polisi na Takukuru wawatafute popote. Watazitapika hizo fedha wanazozitafuna,” amesisitiza Rais. Amesema hatojali fisadi ametoka CCM, Chadema wala CUF au nje ya nchi, atawashughulikia. Mbunge wa Kilombero, Lijualikali(CHADEMA) “Ukiniambia leo uwape zawadi gani watu wa Morogoro maana kuna mengi lakini naomba watu wote ambao wamechukua ardhi yetu na hawaifanyii kazi basi naomb

MAAMUZI YA JOHN HECHE BAADA YA MAZISHI YA MDOGO WAKE

Image
MBUNGE wa Tarime Vijijini kupitia (CHADEMA), John Heche amesema kutokana tukio la kuuawa kwa mdogo wake Suguta Chacha kwa kuchomwa kisu na askari polisi haturudi nyuma kupigania haki za watu ili haki na usawa kushamiri katika nchi. Heche amesema hayo leo Ijumaa, Mei 4, 2018 ikiwa ni siku moja baada ya mazishi mdogo wake huyo na kusema mdogo wake ameuawa kinyama, na kifo hicho kinazidi kumpa nguvu na sababu ya kupigania haki. “Nakuombea, upumzike kwa amani Suguta, kifo chako cha kinyama kinanipa sababu zaidi ya kuendelea kupigania. Utawala wa sheria haki na usawa katika taifa letu. Sitarudi nyuma nitapambana mstari wa mbele wakati wote kwa heshima yako na kwa heshima ya Watanzania wote wanaopenda kuona nchi yetu inaongozwa vizuri,” alisema Heche.  Aidha, Heche amewashukuru waombolezaji waliojitokeza kumzika mdogo wake huyo kwenye nyumba yake ya milele na kusema kuwa wamewapa faraja sana.  “Asanteni Watanzania wote na Wanatarime kwa jinsi ambavyo

Rais Magufuli ampigia simu Prof. Kitila mbele ya Wananchi

Image
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amempigia simu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Prof. Kitila Mkumbo kufuatia malalamiko ya wananchi kuhusu kero ya maji katika eneo la Kidodi Morogoro. JPM amemtaka Prof. Kitila afike eneo hilo mara moja kushughulikia kero hiyo. Aidha, Rais Magufuli ameagiza Mkandarasi wa Maji Kata ya Kidodi, akamatwe mara moja kwa kushindwa kukamilisha mradi wa maji ndani ya wakati uliopo kwenye makubaliano ya utekelezaji wa mradi huo. “Ninafahamu kuna mradi wa maji wa Tsh. Milioni 800, mkandarasi alipewa lakini mpaka sasa maji hayajafika kwa wananchi, nilidhani mbunge wenu atauliza achukuliwe hatua gani lakini hajauliza, sasa mkandarasi kama alikula hela atazitapika, naomba mumfikishie huu ujumbe,” alisema Rais Magufuli.

Breaking News: Mahakama Kuu Yazuia Kanuni za Maudhui Mtandaoni

Image
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mtwara leo Ijumaa Mei 4, 2018 imetoa zuio la muda (Temporary Injuction) dhidi ya tangazo linalowataka wamiliki wa Blogs na Majukwaa ya Mitandaoni (Online Forums) kusajili huduma hizo kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutokana na matakwa ya kanuni mpya za Maudhui ya Kimtandao (Online Content Regulations) ambazo matumizi yake yamekwishaanza na kesho Mei 5, 2018 ndiyo siku ya mwisho ya usajili huo. Maombi ya zuio hilo yaliyowalishwa mahakamani na waombaji sita wakiwemo Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Cente -LHRC), THRDC, MCT, TAMWA, Jamii Media na TEF ambapo katika kesi ya msingi ya mapatio ya kanuni hizo (Judicial review) washitakiwa ni Waziri wa Habari, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (Tanzania Communication Authority -TCRA) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG). Aidha, katika maombi ya msingi, waombaji wameiomba Mahakama kufanya mapitio ya kanuni hizo kwa vigezo vifuatavyo; i) Waziri wa Habari ametumia

John Stephen Akhwari Mwanariadha Shujaa Wa Tanzania

Image
John Stephen Akhwari akikimbia. M CHEZO wa ri­adha ni mchezo wa tatu unaopendwa zaidi na Watanza­nia, ukiondoa soka na ndondi bila shaka riadha ndiyo nam­ba tatu. Ukifungua ukurasa wa Google au YouTube kisha ukaandika John Stephen Akhwari hakika kile am­bacho utakiona kitakufanya utamani kutazama mpaka mwisho. Jina la mtu huyo litajitokeza mara nyingi kwenye kurasa hizo na k a m a u n ­amfa­hamu b a s i itaku­fanya utamani kumtazama na kuona historia yake kwa mara nyingine, kama ni mara yako ya kwanza bila shaka kuna kitu utajifunza hata kama siyo cha kimichezo basi kimaisha. Historia ya tukio lake lililotokea mwaka 1968 nchini Mexico bado ina­kumbukwa hadi leo, taswira ya kile wakati akikimbia kiliwa­fanya Wazungu wengi wakitambue kama ‘The Greatest Last- Place Fin­ish Ever in the Olympic games’. Maana isiyo ras­mi ya sen­tensi hiyo ni kuwa ni mtu wa mwisho bora ku­wahi kumaliza katika michezo ya Olimpiki, yaani alikuwa wa mwisho lakini ni bora kuwahi kut

Simba Kufanya Mkutano wa Dharura Jumapili Mei 20

Image
Uongozi wa Klabu ya Simba unapenda kuwataarifu kwamba, kutakuwa na Mkutano wa Mabadiliko ya katiba utakaofanyika siku ya Jumapili ya tarehe 20/5/2018

Umaskini Utazidi Kukunyemelea Sana Kama Una Tabia Hizi Za Pesa

Image
Kushindwa katika maisha hakuji kwa bahati mbaya bali kuna kuja kutokana na tabia zetu ambazo tunazo kila siku kwenye maisha yetu. Tabia hizo kiuhalisia zinaturudisha nyuma sana kimafanikio kama tunazikumbatia. Kupitia makala haya ya leo nataka nikukumbushe baadhi ya tabia chache tu, na kama tabia hizo utazikumbatia uwe na uhakika unazidi kuukaribisha umaskini ukunyemelee kwenye maisha yako na kukupoteza kabisa. Inatakiwa kuwa makini sana na tabia hizi ambazo zinaweza zikaingilia uhuru wako wa kifedha na kuweza pengine kukuharibia karibu kila kitu kwenye maisha na kukuacha ukiwa mtupu hauna kitu. Tabia hizi ni zipi, twende pamoja tuweze kujifunza;- Tabia 1: Matumizi yako ni makubwa sana. Kama una matumizi makubwa kwa namna yoyote ile huwezi kukwepa kuishiwa. Inatakiwa matumizi yako uweze kuyabana kiasi cha kwamba yapate nafasi ya kukupa pesa ya ziada. Ni vizuri kuwa na daftari la kumbukumbu litakalokusaidia kutunza kumbukumbu zako za matumizi ili kimatumizi u