Posts

Showing posts from December 7, 2016

Mongela Atinga Mitaani Kuhimiza Usafi wa Jiji la Mwanza

Image
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela akikatiza katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza kuhimiza usafi. Mhe. John Mongela akitoa maelezo kuondoa vitu vilivyowekwa nje ya duka la mkazi wa Mwanza. Wakazi wa Mwanza eneo la soko kuu wakiondoa uchafu katika mtaro uliopo eneo hilo. Mwananchi huyu akiondoa takataka zilizopo kwenye mtaro uliopakana na duka lake.    Zoezi la kusafisha Jiji la Mwanza likiendelea. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela ametembea mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza kuhimiza watu kufanya usafi katika maeneo wanayofanyia kazi pamoja na kutoa muongozo wa namna wafanyabiashara watakavyoendesha biashara zao. Ziara hiyo imefanyika baada ya kumaliza zoezi la kuondoa wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika maeneo yasiyoruhusiwa na kuwapeleka maeneo mbalimbali ambayo yalitengwa kwa ajili ya wafanyabiashara hao. Katika ziara hiyo iliyokuwa imeambatana na viongozi mbalimbali wa serikali walipita maeneo ya Makoroboi, Liber

Trump Kusitisha Uagizwaji wa Ndege Mpya za Air Force One

Image
Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump amesema anataka kufuta ombi la ununuzi wa ndege mpya za Air Force One ambazo hutumiwa na marais wa Marekani. Wiki sita kabla ya kuchaguliwa, aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter kuwa: “Boeing wanaunda ndege mpya aina ya 747 Air Force One za kutumiwa na marais siku zijazo, lakini gharama yake imezidi, zaidi ya $4 billion. Futa oda hiyo!” Serikali ya Marekani iliingia kwenye mkataba na kampuni ya Boeing ili kutengenezwa kwa ndege hizo mbili au zaidi za kuwabeba marais. Ndege hizo zilitarajiwa kukamilika na kuanza kutumiwa mwaka 2024. Hisa za kampuni ya ndege ya Boeing zilishuka kwa zaidi ya 1% baada ya ujumbe huo wa Trumpp kwenye Twitter, ingawa zilijikwamua baadaye. Trump hatarajiwi kutumia ndege hizo mpya, iwapo hatashinda uchaguzi wa muhula wa pili wa mwaka 2020.

Serikali Kuanzisha Tuzo za Mitandao ya Kijamii kwa Wanahabari

Image
Mwandishi wa habari wa mtandao huu, Denis Mtima (kushoto) akikabidhiwa kadi ya kujiunga na mfuko wa hiari wa mwanachama wa PSPF na Waziri Nape Nnauye. Nape akimkabidhi mwanadada mwandishi wa habari, kadi ya ATM ya NMB. …Akisisitiza jambo fulani kwa wanahabari. …Akizungumza jambo. Mwakilishi wa wadhamini wa semina hiyo ambaye ni Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Vicky Bishubo, akizungumza jambo kwenye hafla hiyo. Mkurugenzi wa mfuko wa hiari wa mwanachama wa PSPf, Adam Mayingu ambao nao walikuwa wadhamini wa semina hiyo, akizungumza jambo. Vicky Bishubo akimkabidhi Nape zawadi iliyokuwa imeandaliwa kutoka NMB. Taswira ilivyoonekana katika semina hiyo. WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amesema serikali inatarajia kuanzisha Tuzo za Umahiri kwa waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii (blogs na website) kuanzia mwakani 2017. Hayo ameyasema jana wakati akifunga semina kwa mtandao wa wamiliki wa mitandao ya kijamii

Waziri Mkuu Majaliwa Ataka Nyaraka za Faru John Ifikapo Kesho

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameugiza uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya  Ngorongoro (NCAA), kumpelekea nyaraka zote zilizotumika katika kumhamisha faru maarufu kwa jina la John katika hifadhi hiyo ifikapo Desemba 8, 2016. Majaliwa amesema ana taarifa kuwa walimhamisha Faru John Kreta kwa siri na kumpeleka  V I P Grumet  Serengeti Disemba 17, 2015 na waliahidiwa kupewa sh. milioni 200 ambapo  na wamepewa sh.  milioni 100 kwa ahadi ya kumaliziwa sh. milioni 100 nyingine baadaye. Amesema hayo Desemba 6, 2016 alipotembelea Ofisi za makao makuu ya NCAA, zilizoko wilayani Ngorongoro mkoa Arusha  wakati akizungumza na watumishi wa mamlaka hiyo pamoja na Wajumbe wa  Baraza la Wafugaji ikiwa ni  sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani hapa. “Naomba niletewe nyaraka zote zilizotumika kumuomba na kumuondoa faru huyo na barua zilizotumika kujadili suala la faru John. Nasikia amekufa naomba pembe ziletwe ofisini na iwapo itath

Diamond na Zari Wamepata Mtoto wa Kiume Leo Des. 6, Bofya Hapa Kuona Pichaz

Image
Pretoria, Afrika Kusini: TAARIFA njema kwa mashabiki wa msanii wa Bongo Fleva hapa nchini, Nasbu Abdul “Diamond Platnumz” ambaye leo leo Desemba 6, 2016, mpenzi wake Zarina Hassan “Zari The Boss Lady” amejifungua mtoto wa kiume katika Hospitali ya Netcare iliyopo mjini Pretoria nchini Afrika Kusini. Mtoto aliyekuwa akisubiliwa kwa hamu kubwa. k Kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Diamond kupitia ujumbe aliouandika kwenye akaunti yake ya Instagram ameeleza kuwa mtoto wao huyo amezaliwa majira ya saa 8:35 usiku kwa saa za Afrika kusini ambazo ni sawa na saa 10:35 alfajiri kwa saa za Afrika Mashariki. Mbali na Diamond kuposti picha zikionesha miguu ya mtoto huku akieleza kuwa mpaka sasa bado hawajapata jina la kumuita mtoto wao, mpenzi wake, Zari ameposti picha ikionesha mikono ya kichanga chao na kuwashukuru wale wote waliokuwa wakimuombea kwa Mungu ili ajifungue salama. Mtoto huyo anakuwa ni wa pili kwa Diamond kuzaa na mpenzi wake Zari baada ya m