Posts

Showing posts from August 30, 2016

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 30.08.2016

Image

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI LEO TAREHE 30/8/2016

Image

Lema Apandishwa Kizimbani kwa Kesi Mbili Tofauti, Aachiwa kwa Dhamana

Image
  Dar es Salaam. Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema amepandishwa mahakamani leo katika kesi mbili tofauti. Kesi ya kwanza namba 351/2016 anatuhumiwa kumtumia ujumbe wa simu wa uchochezi Mkuu wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo wenye maneno kuwa “Karibu tutakudhibiti kama mashoga walivyodhibitiwa Uarabuni” Kesi ya pili namba 352/16 Lema anatuhumiwa kuhamasisha maandamano Septemba Mosi kinyume cha sheria. Hakimu amepinga hoja za wakili wa Serikali,  Vincent Njau kuzuia dhamana kwa sababu za kiinterejensia kwa usalama wake. Baadaye vurugu ziliibuka mahakamani wakati polisi wanataka kumpeleka Lema magereza kwa madai kuwa wanadhani wamechelewa, lakini mbunge huyo alipinga hatua hiyo kwa maelezo muda wa mahakama saa 9.30 ulikuwa bado. Baada ya kusomewa kesi hiyo, Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imemuachia Mbunge wa Arusha, Godbless Lema kwa dhamana baada ya kulala mahabusu kwa siku tatu bila kula

Mbowe, Lowassa, Mnyika na Dkt. Mashinji Wakamatwa na Polisi, Dar

Image
Kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichokuwa kinafanyika katika Hoteli ya Giraffe iliyopo Mbezi jijini Dar, kimezingirwa na jeshi la polisi huku viongozi wake wakikamatwa na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano. Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema waliokamatwa na polisi kwa ajili ya mahojiano ni Edward Lowassa, Freeman Mbowe, John Mnyika, Dk Vincent Mashinji na  Said Issah “Tulikuwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichojumuisha wajumbe na wabunge kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya chama. Jumla ya wajumbe walikuwa 170. Tukiwa kwenye kiako walikuja watu wanasema tunatakiwa polisi kwa sababu tumekiuka agizo la lilitokataza mikutano.”

UVCCM WAAHIRISHA MAANDAMANO YAO,WATII AGIZO LA JESHI LA POLISI

Image
Agosti 22, 2016 Umoja wa Vijana wa CCM tuliutangazia umma na dunia kwamba ifikapo Agosti 31 mwaka huu tutaitisha maandamano ya amani nchi nzima yenye lengo la kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli kwa utendaji wenye tija, ufanisi na uliorudisha imani na matumaini kwa wananchi. Msimamo na dhamira ya kufanya maandamano hayo ya amani yenye maudhui na kusudio hilo, bado uko pale pale ingawaje si kwa tarehe tuliopanga na kutangaza awali yaani Agosti 31 mwaka huu. Jumuiya yetu kama mjuavyo ni ya Vijana wa CCM, (UVCCM) inapata malezi kwa karibu mno na Jumuiya ya Wazazi ya CCM. Wiki ya jana Mwenyekiti wa Wazazi Taifa Nd. Abdallah Bulembo alikutana na waandishi wa habari akitutaka UVCCM tuahirishe maandamano ya Agosti 31 mwaka huu hadi wakati mwingine. Kwa mujibu wa Katiba ya Chama Cha Mapinduzi, Jumuiya ya Wazazi ndiyo Msimamizi wa Malezi, Maadili na Adabu kwa Vijana wote nchini, sisi UVCCM tunaamini kuwa siki

BREAKING NEWS .... Mtatiro Aula CUF ... Afunguka mazito

Image
NIMEUPOKEA UTEUZI..... Ndugu zangu, nimepokea majukumu niliyokabidhiwa na Baraza Kuu la chama changu. Siwezi kuepuka majukumu haya muhimu kwa wakati huu ambapo chama kinahitaji mchango wangu. Niko IMARA sana, natambua nimepewa majukumu wakati gani na nianze na mguu upi kwenda mbele. Uongozi ni MZIGO na si kazi nyepesi, nahitaji kusaidiwa, kushauriwa, kuombewa na kuungwa mkono na watu wenye nia njema na siasa za mabadiliko ya kweli hapa nchini, walio ndani na nje ya CUF. Natambua kuwa wapo wana CUF wenye sifa, uwezo, vigezo na busara kunishinda, lakini kwa sasa chama kimeona naweza kuuungana na wenzangu kukisimamia. Naahidi kuwa ntatoa uongozi wa KISASA wenye kushughulikia MASUALA. Ntatimiza wajibu wangu bila hofu yoyote kama kawaida yangu na ntatoa UONGOZI WA PAMOJA (Collective Leadership) kwa kila mwenye nia safi na CUF na mabadiliko. Nitakuwa mhimili imara katika kipindi hiki cha mpito, kuhakikisha CUF inafanya kazi zake na inaimarika ili kujenga uwezo wa ndani, k